Kila akili salama inaamini ulimwengu umeumbwa na Mungu sio buree

safuher

JF-Expert Member
Feb 11, 2019
11,164
15,848
Kama akili zako zinang'amua mambo sawa sawa basi utajua tu kwamba huu ulimwengu wetu umeumbwa na Mungu wala hauja exist tu kwaanbahati mbaya au nature.

Kama mtu hakubali kwamba yale maghorofa ya kariakoo hayajaja yenyewe basi lazima asikubali pia kwamba dunia hii ipo ipo tu kwamba eti hakuna msababishi.

Kila unachokiona kina msababishi wake tena ana akili na malengo ya kufanya.
Simu unayotumia haikuibuka tu lazima kuna aliyesababisha na alikuwa na Malengo yake ambayo ndio wewe unatumia sasa hivi hayo ndio malengo

Hiyo nguo unayovaa sio nature kwamba ati imejitengeza yenyewe tu hapana,kuna mtu alibuni na akasababisha tena kwa malengo maalumu ya watu kujisitiri na kujihifadhi na lengo hilo limeetimia

Kiatu chako nacho hakikuja tu paap kwamba kimeibuka yakhee,lazima kuna aliyesababisha akatumia akili zake akabuni na akatengeneza na malengo yake yakatimia.

Sasa ikiwa vitu hivi vidogo vidogo katika dunia vina msababishi wake tena mwenye akili na ufahamu wa kufikiria mambo sawa sawa je dunia vipi isiwe nna msababishi aliyeiumba tena mwenye akili na ufahamu na akatuumba sisi tuje duniani hapa kwa malengo Maalumu...?

Akili salama lazima ikubali kwamba ulimwengu umeumbwa na Mwenye akili na fikra sawa sawa tena kwa malengo maalumu.

Haiwezekani kwamba kitu kisichokuwa na akili wala fikra kizalishe kitu ambacho kina akili na fikra na malengo

Vijana mnaomkataa mungu mkifa mkamkuta mtakuwa mumepoteza sana,vijana tunaomkubali Mungu tukifa alafu tusimkute tutakuwa hatujapoteza kitu chochote zaidi ya kupata faida.

Wanaoamini Mungu wana dhamana ya kuishi kwa raha hapa duniani na huko akhera kwa sababu wakimkuta walishajiandaa tayari,na kama hawakumkuta (wadaivyo kina Kiranga ) basi hawana cha kupoteza.
.
Mkubali Mungu uishi kwa amani isiyo na wasiwasa kabisa.
Mungu awabariki nyote..
 
hoja iliyopo ni kwamba.

kama hakuna kilichopo kikawepo bila chanzo,basi naye Mungu ana chanzo chake.hawa jama wana hoja sababu Mungu ameamua kujificha kwao makusudi kabisa,ameamua kuwaacha na maswali.
Nani kasema kwamba hakuna kilichopo kikakosa chanzo ni nani...?

Mimi sijatumia hoja ya kuwa kila kilichopo lazima kiwe na chanzo.lsbda ungeuliza kwamba hoja yangu ni ipi juu ya jambo hilo
 
Faraja itatoka wapi Kama shida ziko pale pale? Nilidhani kumuamini Mungu unabarikiwa double double, lakini walokole wengi na wanaojifanya wanamjua sana Mungu ni masikini na wenye matatizo.
Na unasemaje juu ya wale matariji wanaomuamini Mungu wakubwa wakubwa wenye pesa....?
 
Faraja itatoka wapi Kama shida ziko pale pale? Nilidhani kumuamini Mungu unabarikiwa double double, lakini walokole wengi na wanaojifanya wanamjua sana Mungu ni masikini na wenye matatizo.
Sisi tunaoamini Mungu tunapata faraja tukikumbuka kwamba kuna maisha ya raha baada ya kifo hivyo hata tukikosa hapa duniani tutapata huko

Na ambao hawaamini Mungu huoni kama wanakosa faraja kwa sababu wanahisi wakikosa hapa ndo basi tenaa hawapati tena kwa kule kuamini kwao hakuna maisha baada ya kifo hivyo wanaumia zaidi kwa kuamini kwao kwamba hapa ndo fainali wakikosa ndo baaasi..je huhisi hilo.?
 
Sisi tunaoamini Mungu tunapata faraja tukikumbuka kwamba kuna maisha ya raha baada ya kifo hivyo hata tukikosa hapa duniani tutapata huko

Na ambao hawaamini Mungu huoni kama wanakosa faraja kwa sababu wanahisi wakikosa hapa ndo basi tenaa hawapati tena kwa kule kuamini kwao hakuna maisha baada ya kifo hivyo wanaumia zaidi kwa kuamini kwao kwamba hapa ndo fainali wakikosa ndo baaasi..je huhisi hilo.?
Sidhani Kama wanaumia maana wanaamini kuwa ukifa umekufa, Ni kama umelala usingizi vile, why uumie?
 
Back
Top Bottom