KIKWETEISM: falsafa mpya na ya hatari

KIKWETEISM: falsafa mpya na ya hatari

MPIGA ZEZE

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2011
Posts
2,539
Reaction score
2,297
Unawaambia wananchi yale ambayo unajua wanataka kusikia (maisha bora kwa kila mbongo, ambulance za bajaj kwa akina mama wajawazito huko maeneo ya milimani) kisha unajiendea Ikulu na kupiga usingizi mnono (yaani mzigo mzito).

Kesho yake wanakuuliza vipi baba yale uliyotuahidi, unasema siyo kila ahadi lazima itekelezwe na papo hapo unamwaga ahadi nyingine mpya kabisaaa (kilimo kwanza, maji kwanza, flyovers ubungo, nk), na wananchi wa kusadikika wanakupigia makofi. Unarejea Ikulu unajichapia usingizi mnono. Baada ya miaka yako kumi Ikulu unajiondokea mlaini na matrilioni yako!

Basi angaa kwa miaka yako miwili iliyobakia watoe watoto wa shule sakafuni na uwaweke kwenye madawati - utakuwa na kitu cha kukumbukwa katika historia ya nchi hii ya Kusadikika!

tanzania miaka 50 ya uhuru 2011.jpg
Maisha bora kwa kila mtanzania
 
Ameishia kuwaacha viongozi wa CCM wakijimilikisha mashamba ya wananchi - SUMAYE, YONA, na WARIOBA wakijitwalia maelfu ya heka Zinga na makurunge - BAGAMOYO.
"KIJANA wa SENGEREMA" akimiliki shule kubwa kuliko zote ukanda wa PWANI.
 
Ile picha aliyopiga na wasanii huko Mbeya najaribu kuilink na ile aliyopiga na Mwampamba/Shonza, najiuliza kama huu ndio mfumo mpya wa uendeshaji wa chama au ni (usanii)[SUP]2[/SUP]
 
bora kikwete maana ahad za slaa hata akae madarakan miaka 10 hazitekelezek. Nchi iwe na viwanda ndan ya mwaka mmoja, sment bku 5, nk nk. Huyu mzee ndo ana ahad hewa kabisa
 
Hivi hii picha ni ya M4C pamoja daima ?

Ilikuwa wapi na lini ? Mbona ni watu wengi sana, na kwa nini sijaiona before, especially kati ya picha zilizotolewa officially na CDM ? Sio kwamba napinga, lakini kama ni ya kweli, naomba utoe details (nisije nikaanza kushangilia, kumbe nashangilia kitu fake)

Sio mkutano wa injili huu ? Nimejaribu ku-scan angalau alama za CDM (nguo, kofia etc) sijaona.......Na kwa haraka haraka naona wanawake ndio wengi, na nimeona kama mtu mmoja hapo mbele ameinua Biblia...

Kama nilivyosema, sio kwamba napinga lakini nina mashaka. Kama una uhakika kwamba hii ilikuwa M4C naomba utupe details mkuu....

DSCN9712.JPG

M4C INATISHA
 
bora kikwete maana ahad za slaa hata akae madarakan miaka 10 hazitekelezek. Nchi iwe na viwanda ndan ya mwaka mmoja, sment bku 5, nk nk. Huyu mzee ndo ana ahad hewa kabisa

Ccm ndio wezi maana haya yote yanawezekana ila ni umbumbu wa watunga sera wetu katika seriksli ya jk
 
Duh! hili nyomi unataka MACCM wazimie? ilikuwa wapi hiyo mkuu?
 
hivi kwani ni lazima uanzishe uzi? maana naona pumba tu hapa na hakuna cha kujadili.

Unawaambia wananchi yale ambayo unajua wanataka kusikia (maisha bora kwa kila mbongo, ambulance za bajaj kwa akina mama wajawazito huko maeneo ya milimani) kisha unajiendea Ikulu na kupiga usingizi mnono (yaani mzigo mzito). Kesho yake wanakuuliza vipi baba yale uliyotuahidi, unasema siyo kila ahadi lazima itekelezwe na papo hapo unamwaga ahadi nyingine mpya kabisaaa (kilimo kwanza, maji kwanza, flyovers ubungo, nk), na wananchi wa kusadikika wanakupigia makofi. Unarejea Ikulu unajichapia usingizi mnono. Baada ya miaka yako kumi Ikulu unajiondokea mlaini na matrilioni yako!
Basi angaa kwa miaka yako miwili iliyobakia watoe watoto wa shule sakafuni na uwaweke kwenye madawati - utakuwa na kitu cha kukumbukwa katika historia ya nchi hii ya Kusadikika!

View attachment 136944
Maisha bora kwa kila mtanzania
 
Kweli hawa vijana wa BAVICHA mtandaoni wanatapatapa sana,maana hiyo picha inaonyesha kabisa kwa macho ya nyama tu kuwa ni mkutano wa injili,wao wanawadanganya watanzania kuwa eti ni M4C. Hawa BAVICHA wakiachwa hivi watazidi kukiharibu chama na hatimaye kukiua kabisa.Viongozi tafadhalini chukueni hatua dhidi ya hawa BAVICHA,vinginevyo mtaonekana nanyi mmebariki vitendo vyao
 
bora kikwete maana ahad za slaa hata akae madarakan miaka 10 hazitekelezek. Nchi iwe na viwanda ndan ya mwaka mmoja, sment bku 5, nk nk. Huyu mzee ndo ana ahad hewa kabisa
Kama hujui tu na hautajua coz hutaki kujifunza it means mpambafu au ndo elimu ya kivukoni? Dr. Slaa is next level
 
Back
Top Bottom