voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,885
Mheshimiwa Rais mstaafu,
Tulidhani ukiishastaafu unatoka kwenye siasa Rasmi, laakini umetumia haki yako ya kikatiba kutoa maoni yako.
Ingawa wengine wanazuiwa kutoa maoni yao ila wewe umetumia mimbari hiyohiyo kufanya kile ulichokipinga.
Ulipaswa kutoa hilo tamko nje ya mimbari hiyo maana hilo sio jambo walilokuwa wamekualika kwenda pale kulisema,ukweli ni kwamba waraka ule umegusa maslahi yako!
Wewe ni mwanasiasa na pale ulikuwa kwenye platform ya kidini, kwa maana kanisa la wasabato.
Kwamba tusichanganye dini na siasa.
Je, Wakati ule ukiusaka u-rais nakumbuka mhashamu kardinali Pengo aliwahi kutamka kwamba wewe ni
"Chaguo la Mungu"
Sikusikia mahali kwenye kampeni zako ukilikemea hilo? Pia huko bungeni wako maaskofu na wachungaji kibao wakifanya siasa,na mfano halisi ni Askofu Gwajima-mbunge wa Kawe.
Je, Mbona wako makanisani wanahubiri na kisha jumatatu wanaenda bungeni pia wanahutubia?
Je! hao mbona CCM iliwapokea na kuwatumia kisiasa mpaka sasa?
Na tena wewe mheshimiwa umenufaika sana kupitia hilo kanisa hadi kukwea na kufikia hapo ulipofika leo.
Bandari isitufanye tukaondoa utu wetu hapa Duniani.
Sauti ya Watu ni sauti ya MUNGU!
Pia, soma
Tulidhani ukiishastaafu unatoka kwenye siasa Rasmi, laakini umetumia haki yako ya kikatiba kutoa maoni yako.
Ingawa wengine wanazuiwa kutoa maoni yao ila wewe umetumia mimbari hiyohiyo kufanya kile ulichokipinga.
Ulipaswa kutoa hilo tamko nje ya mimbari hiyo maana hilo sio jambo walilokuwa wamekualika kwenda pale kulisema,ukweli ni kwamba waraka ule umegusa maslahi yako!
Wewe ni mwanasiasa na pale ulikuwa kwenye platform ya kidini, kwa maana kanisa la wasabato.
Kwamba tusichanganye dini na siasa.
Je, Wakati ule ukiusaka u-rais nakumbuka mhashamu kardinali Pengo aliwahi kutamka kwamba wewe ni
"Chaguo la Mungu"
Sikusikia mahali kwenye kampeni zako ukilikemea hilo? Pia huko bungeni wako maaskofu na wachungaji kibao wakifanya siasa,na mfano halisi ni Askofu Gwajima-mbunge wa Kawe.
Je, Mbona wako makanisani wanahubiri na kisha jumatatu wanaenda bungeni pia wanahutubia?
Je! hao mbona CCM iliwapokea na kuwatumia kisiasa mpaka sasa?
Na tena wewe mheshimiwa umenufaika sana kupitia hilo kanisa hadi kukwea na kufikia hapo ulipofika leo.
Bandari isitufanye tukaondoa utu wetu hapa Duniani.
Sauti ya Watu ni sauti ya MUNGU!
Pia, soma
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete: Msijaribu Kuchanganya Dini na Siasa Hata Kidogo
Kikwete watumishi wa Mungu hawezi kutofautisha siasa na dini kwa sababu siasa ni dini na dini ni siasa
Mch. Mbarikiwa ahoji iwapo kiongozi wa dini kukemea uovu wa viongozi wa kisiasa ndiyo kuchanganya dini na siasa? Amtaka Kikwete kufafanua hoja yake
Barua ya Wazi kwa Jakaya Kikwete: Hoja ya Kuchanganya Dini na Siasa
Wacha nimpe darasa kidogo Mzee Jakaya Kikwete
Askofu Desmond Mpilo Tutu wa Afrika ya Kusini hakukaa kimya kuwatetea watu weusi (Dini vs Siasa)
Baba Askofu Stephen Munga: Acheni kucheza karata ya Udini, hoja ijibiwe kwa hoja