Kikwete, Serikali ichunguzwe suala la Absalom Kibanda!

Hofu ya Al Qaeda Ukerewe

JUMATANO, FEBRUARI 20, 2013

NA MWANDISHI WETU

*Wananchi wakihusisha chuo na ugaidi
*Mbunge ataharuki, aandaa hoja binafsi
*Mkuu wa Mkoa, DC wakwepa kunena

HOFU ya kuwapo kwa magaidi wa mtandao wa Al- Qaeda, imetanda katika Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza, baada ya kuvuja kwa taarifa za kuanzishwa kwa chuo kimoja cha kidini kinachohofiwa kutoa mafunzo yenye mwelekeo wa kigaidi visiwani humo.

Taarifa hizo zimeeleza kuwa chuo hicho kinajulikana kwa jina la Markaz, Aljazeera na kimeanzishwa kwa ufadhili wa raia wa kigeni ambao ni waumini wa dini ya Kiislamu.

Makundi yanayotajwa kufadhili uendeshaji wa chuo hicho ni Al-Qaeda na Al shabab yanayoaminika kuwa na mtandao mkubwa wa ugaidi duniani.

Uchunguzi uliofanywa na Mtanzania Jumatano wilayani Ukerewe, umebaini kuwa chuo cha Markaz kinatoa mafunzo kwa watu wa rika mbalimbali yenye mwelekeo wa kujihami na kushambulia kama Karate na Kung-fu.

Aidha, taarifa nyingine za kiuchunguzi ambazo gazeti hili lilidokezwa na wakazi wa kisiwani humo walioonyesha wasiwasi wa kuwepo kwa chuo hicho, zilidai kuwa, aina nyingine ya mafunzo yanayotolewa katika chuo hicho na kushambuliana kwa silaha aina ya jambia.

Uchunguzi ulibaini zaidi kuwa, wanafunzi katika chuo hicho ni watoto wenye umri wa kati ya miaka saba hadi 10 na pia kuna wanafunzi vijana na watu wazima.

Baadhi ya wakazi wa wilayani humo waliopata kufanya kazi katika chuo hicho, waliliambia gazeti hili kuwa chuo hicho kimekuwa kikipokea mizigo ya aina mbalimbali, ikiwa imefungwa kwenye maboksi ambayo katika udadisi wao walibaini kuwa, baadhi ya bidhaa zinazokuwa kwenye shehena hizo ni kanzu, seti za televisheni, vitabu na silaha za aina mbalimbali.

Walidai kuwa, walianza kukitilia mashaka chuo hicho baada ya kubaini kinapokea silaha katika baadhi ya mizigo yake.

Mbali ya hilo, wakazi hao walilieleza gazeti hili kwamba aina ya wageni wanaoingia na kutoka visiwani humo kwa minajili ya kukitembelea chuo hicho, ni jambo jingine ambalo limekuwa likiwafanya wazidi kukitilia shaka chuo hicho.

Kwa mujibu wa wakazi hao, wageni hao wamekuwa wakiingia kisiwani kwa njia ya mitumbwi wakipita katika njia za panya nyakati za usiku.

Wageni hao kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo la Nansio ni wale wanaodaiwa na kuaminika kutoka katika nchi jirani za Kenya na Uganda ambazo mipaka ya ziwa Victoria inapita.

Wafanyabiashara wanaojihusisha na usafirishaji abiria waliozungumza na gazeti la Mtanzania Jumatano walieleza kuwa, wageni wanaowapakia kuwapeleka chuo cha Markaz au maeneo mengine ya kisiwa hicho huwalazimisha kuondoa misalaba waliyoivaa shingoni au waliyotundika katika magari na pia huwataka wazime redio katika magari yao.

Hofu hiyo ya wakazi wa Nansio ilisababisha gazeti hili kumtafuta Mbunge wa Ukerewe, Salvatory Machemli (Chadema) ambaye naye alikiri kulifahamu jambo hilo.

Akizungumza kupitia simu yake ya kiganjani, Machemli alisema chuo hicho kinatoa mafunzo ambayo wakazi wake wanayahusisha na matendo ya kigaidi.

Mbunge huyo alisema hofu zaidi kuhusu chuo hicho ni kuwapo kwa taarifa zinazodai kwamba, baadhi ya wanachuo ambao wamewahi kupata mafunzo chuoni wanatajwa kuwa wanachama wa makundi ya kigaidi ya Al Qaeda na Al-Shabab.

Kwa mujibu wa mbunge huyo, miongoni mwa hatua ambazo amepata kuzichukua ili kutafuta majibu ya wasiwasi wa wananchi wa Ukerewe ni pamoja na kumsaka mmoja wa watu anayekijua chuo hicho.

"Ni kweli tuna wasiwasi na hatuoni kazi ya umma kinachojihusisha nacho. Niliwahi kumuuliza Diwani wa Kata ya Nansio, Sheikh Ramadhani Mazige (CCM) kuhusu uhalali wa kuwapo kwa chuo hicho kwa sababu alikuwa akisimamia ujenzi wake na nikashauri juu ya umuhimu wa kubadili aina ya mafunzo yanayofundishwa chuoni hapo na jibu lake lilikuwa wenye chuo hawataki.

Alipoulizwa iwapo anawafahamu wamiliki wa chuo hicho, alikana kuwatambua kwa kueleza kuwa, jitihada zake za kuwafahamu hazikufanikiwa baada ya Diwani Mazege kukataa kuwataja.

Machemli alisema kuwa, amepanga kulifikisha suala hilo kama hoja binafsi kwenye Baraza la Madiwani ili kuomba kibali cha kutembelea chuo hicho kuona shughuli zinazofanyika na kwamba iwapo atakwamishwa, atalifikisha suala hilo katika ngazi za juu.

Akizungumza kuhusu raia wa kigeni wanaopitia njia za panya kwa usafiri wa mitumbwi nyakati za usiku kufika chuoni hapo, Machemli alisema hilo hawezi kulipinga.

Kwa mujibu wa Machemli, jiografia ya visiwa vya Ukerewe inavifanya viwe wazi kuhusu mipaka yake na kwamba jambo hilo alipata kulizungumza bungeni ingawa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha alimpuuza.

"Nilizungumza katika mkutano uliopita wa Bunge kuhusu mipaka ya Ukerewe kuwa wazi sana, nililalamika kwamba, wanajeshi wa Kenya na Uganda wanakuja hadi katika kisiwa hicho kufanya mazoezi yake na kuondoka, lakini nashangaa waziri akanipuuza," alilalamika Machemli.

Alipotafutwa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu kwa ajili ya kuzungumzia juu ya hofu hiyo, alisema anaomba apewe muda kwa sababu yeye ni mgeni mkoani humo na huu mwezi wa pili akiwa katika kituo chake kipya cha kazi, hivyo yapo mengi ambayo hayafahamu.

Hata hivyo, Mangu aliliahidi gazeti hili kufuatilia juu ya suala hilo na kulitolea ufafanuzi baadaye.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Mary Tesha alikana kufahamu chochote na badala yake akahoji sababu za mwandishi kumtafuta wakati tayari suala hilo lilisharipotiwa katika gazeti hili hivi karibuni.

Kumekuwa na tetesi za kuwepo kwa vikundi vinavyojihusisha na utoaji mafunzo ya kigaidi hapa nchini, vikiwa vimejificha katika mwamvuli huku lengo halisi likiwa kuhatarisha amani ya kitaifa.

Tayari Rais Jakaya Kikwete amekwishaagiza kusakwa kwa makundi yenye mwelekeo huo yanayohisiwa kuhusika na machufuko na mauaji hapa nchini, wakati akitoa salamu za pole baada ya tukio la kuuawa kinyama kwa Padre wa Kanisa Katoliki Evaritus Mushi huko visiwani Zanzibar.

Maoni --

123
-
-1 #26 Chibwana 2013-02-23 12:24
Hili ni sakata jipya ambalo Gazeti hili linaanzisha kuchochea.
Matokeo yeyote ya hili ni lazima mmiliki na uongozi wa gazeti hili uwe "RESPONSIBLE". Nawasihi acheni kutumia vibaya uhuru muliopewa wa habari kwa kunadi amani ya nchi kupitia idara nyeti kabisa ya IMANI ZA WATU. Musitarajie kuwa uchochezi huu utaishia hapo. It's Shame kwa tasnia ya habari !!!!


-1 #25 ABUBAKARI KARATA 2013-02-23 04:50
Hivi kweli shule kufundisha Karate na Kumfuu ni Ugaidi, Kwa hiyo Wachina na wajapani ni magaidi, Ama kweli tumekosa hoja, na ni kweli kwamba abiria amuamuru mwenye chombo aondoe misalaba, Kweli? Na chuo kutembelewa na wageni ni kosa, mbona tunaona wazungu wanamiminika huku Arusha kutembelea Makanisa, au kwakuwa ni makanisa na hiyo Ni mali ya waislam. Tupime jamani Ni aibu kwagazeti kama hili kuandika mambo ambayo hayana hoja na hayana mashiko kana kwamba waandishi ni mambumbumbu wa kupima mambo.


-1 #24 chorobi 2013-02-23 02:41
NASAHA KWA WASOMAJI HEBU TUANGALIE VYOMBO HIVI VYA HABARI AMBAVYO VINATOA HABARI ZA UCHOCHEZI KWANI LITAKALOTEKEA HAKUNA ATAKWYE SALIMIKA MTANZANIA PAMOJA NA WAANDISHI WAKE WATATUANGAMIZA NDANIN YA NCHI HII KINACHONITIA SHAKA KATIKA HABARI KAMA HIZI JINA LA MWANDISHI HAWALIWEKI HII NI KUONYESHA KUWA HABARI ZAO HAZINA UHAKIKA NA HAWAJIAMINI PIA SI ZA UKWELI KWANINI WAWEKE NA MWANDISHI WETU?INAMAANA HABARI HIYO MWANDISHI WAKE HANA JINA KUNA KILA JITIHADA ZA WASOMAJI KUFAHAMU KUWA MTANZANIA HAITAKII MEMA NCHI HII NA TAMBUENI KUWA UISLAM NA UGAIDI NI TOFAUTI KABISA NI SAWA NA MASHARIKI NA MAGHARIBI HIVYO TAMBUENI KUWA WAISLAM HAWAHUSIKI NA UGAIDI HATA SIKU MOJA KWANI DINI YAO IMEWAELEZA KILA KITU JINSI YA KUISHI NA NDUGU ZAO KATIKA ADAMU TAHADHARINI SAAAANA WASOMA JI WA GAZETI HILI TUTANGAMIA KUTOKANA NA KALAMU HIZI ZA WAANDISHI AMBAO HAWAITAKII MEMA TANZANIA HIII


-1 #23 chorobi 2013-02-23 02:32
Hakuna asiyefahamu kuwa gazeti la mtanzania ni gazeti ambalo lina agenda za siri na waislam kwa maana habari zake zote zinazotoka za kiislam ni dhahiri za kiuchochezi baina ya serikali kuna habari nyingi saana ukifuatilia hazina maaana yoyote nashukuru kuna chombo kimoja cha habari(RADIO IMAN)Waliweza kuwatafuta viongozi wote wa ukerewe ambao mwandishi wa habari hizo alisema walimpa ushahidi na kulifahamu tukio hilo na wao viongozi kukataa na kuonyesha kuwa chuo hicho kinatoa mafunzo yanayohusu dini pekee na hakuna mwananchi ambaye alishalalamika kuhusu chuo hicho TAHADHARI KWA WAISLAM KWANZANI KULISUSIA GAZETI HILI LA MTANZANIA KWANI HALINA MAANA KWETU NA NI WACHOCHEZI SANA


0 #22 Raia Mwema 2013-02-22 11:28
Bwana Mohamed Hamad, kwa nini unahamaki sana na kuhukumu kuwa mtanzania ni waongo. Wewe umetoa wapi huo ukweli mara hii? Nilitaraji ungeamua kufanya na wewe utafiti kama alioufanya mwandishi wa Mtanzania, then uje na matokeo tofauti yatusaidie. Lakini unaposhuka na nyundo bila altenative tukueleweje hapo. Kwamba na wewe ni mmoja wao?


+1 #20 Mohammed Hamad 2013-02-22 06:30
Mtanzania linajulikana kwa kuandika habari za kichochezi na zenye chuki, ni gaazeti linalotumikia watu wenye maslahi yao binafsi nasema hivi kwa kuwa hakuna asiejua walichomfanyia mzee Salim Ahmed Salim wakati wa uchaguzi wa mwaka 2005! Hawa ndio Mtanzania sijui watfaidika na nini ikiwa machapisho yao yatasababisha uvunjifu wa amani nchi. Wewe mwandishi unadhani utaandika tena? Unajiita "Mwandishi Wetu" kwanini usiweke jina lako bayana? wewe ni mwoga na woga unao kwa kuwa unajua habari uliyoandika ni majungu. Tumeishi na kuzaana na wakristo wa madhehebu mbalimbali. Nina marafiki wengi niliosoma nao ambao ni wakristo na wengine wamekuwa kama ndugu! Habari zenu kama hizi haziwezi kuwafanya wanione adui kwa sababu ya dini yangu sana sana watawaona wapumbavu! Acheni fitina andikeni habari zenye kuleta tija kwenye taifa hili njaa zitawaua.
 
Moja ya tabia ya utawala mkongwe uliochoka ni mambo ya umafia kama haya,udini,ukabila,ukanda na ujinga mwingi ambao wananchi masikini na wajinga wanabakia kujishughulisha na mambo madogo kama haya,wakisahau mambo ya msingi ktk maisha yao.
 
good analysis
nakupongeza kwa mwono wako usi na shaka
nami nakutunuku uandishi bora unafaa kuwa mchambuzi wa habari katika media zetu
 
Jana usiku limetokea tukio baya la kuvamiwa na kushambuliwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri na Mhariri Mtendaji wa New Habari Corporation, Ndugu Abdalom Kibanda.
Tukio hilo ambalo limesababisha sintofahamu kubwa miongoni mwa watanzania wanahabari, wapenda uwazi na ukweli na wale wenye kusimamia misingi ya Amani na utulivu katika nchi hii.
Aina ya tukio lenyewe na upekee wa utokeaji wake umegubikwa na utata mkubwa kiasi kwamba akili yangu ikanituma kutafakari kwa kina na kuyaandika haya, ikiwa ni miongoni mwa YAWEZEKANAYO kuwa ndiyo yaliyosababisha tukio ilo la kusikitisha kutokea kwa Mtanzania mwenzetu huyu kipenzi cha wanahabari.
a) 14th November 2012, Baada ya kuundwa kwa sekretarieti mpya ya chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Kibanda akiwa ni Mhariri wa Gazeti la Tanzania Daima ambalo linafahamika wazi kuwa ni chombo cha propaganda cha Chadema chini ya Mbowe, aliandika makala ambayo ilikuwa ikisifu safu hiyo mpya ya uongozi ya CCM,
huku akinukuu kauli mbalimbali za viongozi wa upinzani akiwemo Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Znz, Mhe. Maalim Seif Sharif. Baada ya tukio hili wakuu wa gazeti hilo walimuita na kumuonya juu ya makala yake hiyo.
Lakini katibu Mkuu wa Chadema hakuishia na kuridhishwa kwa kuonywa kwa Kibanda bali alienda mbele zaidi na kumjibu
b) Lakini mara tu ya jibu hilo la Slaa kwa Kibanda, Mhariri huyo kwa ufundi mkubwa aliandika makala nyingine ambayo ilikuwa ikimsifu zaidi Katibu Mkuu mpya wa CCM, ndugu Abdulrahaman Kinana, ambae Slaa alimkosoa katika majibu yake dhidi ya Kibanda.
Baada ya Makala hiyo ya pili, ulizaliwa mgogoro wa haja ndani ya kampuni hiyo ya freemedia uliomuhusisha Kibanda na wamiliki wa kampuni na Chama kinacholitumia gazeti hilo. Mgogoro ambao ulipelekea Kibanda kuihama Freemedia na kuhamia katika New Habari Corporation ambayo kimsingi ni ya wadau wa Chama Cha Mapinduzi na kampuni ambayo kwa namna moja ama nyingine inaruhusu kuandikwa habari katika mandhari na tafsir ya HABARI bila propaganda wala upendeleo. Kwa maana nyingine ni kuwa Ndugu Kibanda alikuwa akihariri habari ambazo zinasema ukweli wa mazuri ya chama cha Mapinduzi na kuimwagia sifa kwa mipango yake ya kuiletea nchi Maendeleo lakini pia kwa kasi ya utekelezaji wa Ilani ya chama.
Baada ya Uamuzi huo wa Kibanda kuhamia New Habari Corporation na kuiandika habari zenye mlengwa wa Kati, wakuu wa Free media walimuita ili kufanya nae mazungumzo ya kumtaka kurejea katika kampuni yao, hasa baada ya Gazeti lao la Tanzania Daima kuanza kupoteza dira na kuandika habari ambazo hazina mvuto hivyo kulifanya kushuka kimauzo na kipropaganda dhidi ya Chama Cha Mapinduzi. Lakini Kibanda aliendelea kukataa kurudi na kuwa pamoja na viongozi hao wasiojua nini maana ya kuwa kiongozi, hawaheshimu taaluma wala hawataki kuruhusu fikra huru kuchukua nafasi katika chama na Kampuni zao. - with Sambala Ole Comrade and 16 others.

Bwana Kageuka, Japo kwa mujibu wa kipachiko chako si wewe uliyeandika maneno hayo bali umeripoti tu kile ulichokiona FB, naomba nitoe ufafanuzi mfupi wa hoja zilizowekwa hapo. Mara kwa mara, tumemwona Dk. Slaa akitoa matamko mbalimbali dhidi ya CCM. Je kwa nini tamko hili lionyeshwe kama tamko la kumjibu Kibanda na wala si tamko kama matamko mengine ayatoayo?

Kuhusu yeye kuondoka Tanzania Daima, naomba nikuwekee hapa nukuu ya kauli ya Absalom Kibanda mwenyewe, baada ya yeye kuondoka Tanzania Daima na baada ya watu kuanza kuongea maneno dhidi yake. Nukuu hii aliitoa tarehe 18 Disemba, 2012 saa tatu kasoro kumi na moja usiku. Nukuu yake hiyo hapo chini:


Wana jamvi

Yamesemwa mengi mema na mabaya kuhusu mimi Absalom Kibanda. Wengine tena wana habari na wakiwamo wahariri wenzangu, wakitumia kivuli cha majina bandia wakafikia hata hatua ya kutoa matusi ya wazi na kebehi juu yangu. Ni kweli nimeondoka Free Media Ltd na kujiunga na New Habari Corporation kwa mkataba mahususi. Wako waliosema ningeanza kazi Desemba Mosi na mwingine akazusha kwamba nilianza kazi Jumamosi iliyopita. Wote hao hawakuwa wakweli. Nimeanza kazi rasmi jana Jumatatu na nikatambulishwa leo Jumanne asubuhi.

Nimeondoka Tanzania Daima kwa heri na wala si kwa shari. Natambua na kuheshimu kwamba kila mmoja anao uhuru wake wa kutoa maoni kuhusu jambo lolote analoona linafaa. Namshukuru Mungu kwamba uamuzi wangu wa kuondoka Free Media umeibua hoja na mijadala mingi mikali. Sikujua kwamba naweza nikavuta hisia kwa wema au kwa ubaya kwa kiwango hicho. Sikupata kujua hata siku moja kwamba kupitia uhariri wangu, msimamo wangu katika baadhi ya mambo na pengine makala zangu niliweka alama katika maisha ya watu wengi ambao ama walikuwa wakiniunga mkono au walikuwa wakikerwa nami. Naamini nimetimiza wajibu wangu.

Nilijiunga Free Media Ltd si kwa sababu nilikuwa muumini, shabiki au mwana Chadema la hasha, bali nilifanya hivyo kwa sababu naamini katika mabadiliko ya kifikra na kimfumo. Nimekuja huku pia kwa sababu hizo hizo. Nilipokwenda Tanzania Daima mwaka 2006 nikitokea Mwananchi baadhi yenu mliniponda mkisema nimejiunga na kipeperushi cha Chadema. Nafurahi kwamba nimeondoka pale huku baadhi yenu mkiwa mashabiki wa kile mlichokiita kipepeushi. Zama hizo kwa wengi wenu Chadema ilionekana kuwa mwanasesere.

Leo Chadema kimekuwa chama makini cha upinzani na kwa kiwango kikubwa kazi hiyo ilichagizwa na maono ya Tanzania Daima nililokuwa nikiliongoza. Maono yetu ya kuchochea mabadiliko yaliijenga Chadema. Bado ningali ninayo maono yale yale ya mabadiliko. Ni wazi nina ajenda na maono binafsi katika mambo kadha wa kadha. Yote hayo yanapaswa kujengwa na kuaminiwa. Kazi hiyo nitaifanya nikiwa hapa New Habari Corp. Nikikwama nitaondoka kama nilivyoondoka Habari Corp (1999), Mwananchi (2006) na Tanzania Daima (2012).
 
Umefunguka poa KAMANDA,mipini sio mipini,misumari sio misumari,imesimama vyema na ukipita inachoma panapostahil.OLE WAO HAWA WANAKUSOMA HAPA NA KUJIFANYA HAWAELEWI YA KWAMBA WATU WANATESEKA NA KUDHALILISHWA NA UTAWALA HUU HARAM,DHALIM NA WA KIDIKTETA WAJA NA VIHOJA VYAO DHAIFU VISIVYOJAA KIGANJA KWA DHAMIRA YA KUWALAMBA MIGUU WATAWALA WALIOJAWA DAMU HADI KWENYE VIGANJA VYAO VYA SALAM NA KULIA CHAKULA CHA DHULMA KWANI SIKU ZAO ZAHESABIKA***Watalia na kusaga meno huku watu wakishangilia bila huruma.
 
Mitandao ya kijamii inaweza isisaidie sana, tunatakiwa tuende kuhamasisha wale watu waliopo vijiweni wasio na kazi na wale wananchi wa vijijini wasiokuwa na uhakika hata wa chakula. Hawa wa kwenye mitandao ya jamii wengi wao wanaandika humu wakiwa wameshiba na hata ukiwaambia kesho kuna maanandamano ni wachache sana watakaoshiriki, maana wengi wao wana kazi zao, au biashara zao ambazo zinawakeep busy.

Na hapa ndipo ambapo hata CHADEMA inakengeuka. Utakuta viongozi wao wamejaa tele kwenye facebook wakibadilisha status zao kila kuchapo, badala ya kwenda vijijini kuwaelewesha wale wananchi wenye njaa kwamba njaa yao inatokana na CCM, na kwamba njia ya kuiepuka ni kuikataa CCM. Vivyo hivyo, tunatakiwa tuchukue hatua kama hizo iwapo tunataka kuikataa serikali.
Kama unataka kuwa MKWELI basi andika ukweli.Ni viongozi wangapi na muda kiasi gani wanutumia katika FB? Hivi operation Sangara,M4C zimefanyika mjini tu? Hivi Mwangosi aliuawa wapi,mjini au kijijini?

Katika dunia ya leo ni lazima kila njia itumike na hapa JF tumeshuhudia tuhuma nyingi zikitolewa na ya karibuni ni elimu ya Mnyika. Jiulize hivi Mnyika angetoa maelezo yake kijijini Kwedizandu waandishi wa habari wangeyapa kipaumbele kama yalivyopata hapa JF?

Naamini CDM inajitahidi sana kwenda vijijini lakini shida kubwa ni uelewa wa watu na umaskini.

Huwezi kuhamasisha watu waikatae CCM wakati tayari ipo madarakani kwa kura,unachotakiwa ni kuwatia sumu wapiga kura wajue udhaifu wa CCM ili wasiipe kura.

Tukiegemea kuhamasisha kuikataa serikali iliyopo madarakani kuna watu watakuwa rumande kwa UHAINI kabla ya 2015 na sheria itawafunga!!!!!!
 
Hivi kuna ushahidi gani thabiti zaidi ya ule anaotoa mhanga wa tukio? ww unatumia akili kuandika haya uliyoweka hapa? Dk Uli alitaja majina, simu za wahusika zinajulikana, hao mbwa unaowatetea nini walichofanya hadi leo, ni ajabu na kuudhi sana hawa washennzi wanaoishi kwa kodi zetu kazi yao imebaki moja tu kutetea upumbavu na kulinda chama cha siasa, tutaona mwisho wenu endelea kujidanganya na miwani yako ya mbao, hatuna usalama wa taifa nchi hii this is a dead weight organ we are carrying!
Binafsi naamini UWT wapo na wana uwezo kubwa wa kufanya kazi yao ila Uzalendo hawana na kwa kuwa system yote ni corrupt naamini wanaangalia zaidi maslahi yao na si UTAIFA tena.Wameingiliwa na wanasiasa na kama utakumbuka miaka ya nyuma katika uteuzi wa mkuu wao wa sasa kuna watu walilalamika kuwa kateuliwa ki ushkaji zaidi kuliko kiutendaji.
Pia tukumbuke kuwa yule mkuu wa ICC alikuwa hapa,na wakubwa hawajatueleza alikuja kufanya nini lakini naamini matukio haya hayatapita bure katika wakati huu,tuombe uhai tutaona mengi!
 
Kikwete's government is a blood thirsty vampire, so to speak. Yana mwisho haya, the blood he has spilt won't let him go unpunished..
 
TATIZO SERIKALI YA CCM WAOWAO WACHEZAJI, WAOWAO MAREFA, WAOWAO MAKAMISAA.
NI LAZIMA MATOKEO WAYAPANGE WAO HATA MFANYEJI.Dawa yao ni the hague
 
Nawalaumu sana Dr Mwakyembe na Dr ulimboka ,kwani hawa ni waathirika walituahidi kuwataja wahusika pindi watakapo toka kwenye matibabu.Ukimya wao ndio unatumaliza.
Ukila nyama ya mtu huachi.J.K.Nyerere.

Kapesa katamu mkuu!
 
thank you very much, its a good analytical piece of work. Kwa kweli nchi yangu pendwa ya Tanzania iko na ombwe kubwa la uongozi this time more ever.

Kwa kifupi udhaifu wa JK.
Tukiendelea kumwita VAsco da Gama Dhaifu, tunamjengea kinga kwenye matukio kama haya.Hii ndiyo style yake ya utawala.kwa hili la kutesa wana harakati, ndiyo uhodari alionao, na sio dhaifu kwenye hili.
 
Tukiendelea kumwita VAsco da Gama Dhaifu, tunamjengea kinga kwenye matukio kama haya.Hii ndiyo style yake ya utawala.kwa hili la kutesa wana harakati, ndiyo uhodari alionao, na sio dhaifu kwenye hili.

Mkuu Maubero uko sahihi sana katika muono wako huo. Yes we need to do something aisee. Hii sasa hatujivunii tena ule uhuri wetu wa kutoa maoni na kuhoji lolote lile bila kuogopa kwamba utangólewa meno na kucha bila ganzi. It is very dangerous aisee

We need to do something, the question is what and how: That remains a million dollar question....
 
Last edited by a moderator:
Wanaopaswa kuchunguzwa sikiliza maneno yao, wakishirikiana na kina Pasco wa JF.

[h=5]Nape Nnauye
[/h][h=5]Hili la kutekwa na kupigwa na kuumizwa kiasi hichi kaka yangu Kibanda, kila nikilitafakari maneno ya waliosema hakutatawalika na makala za Kibanda mbili au tatu za mwisho kabla ya kuhama chombo cha habari kabla ya anachofanyia kazi sasa vinajirudia kichwani mwangu sana! Get well soon brother!
[/h]
 
Siku hizi kila tukio litahusiswa na Uislam, Ugaidi, Uamsho, al qaeda!!! Kwa mtindo huu Watanzania tumekwisha. Akili za Watanzania zimekuwa Under Control ya neno Uislam, hata bado mutayaona mengi. Tafakari.
 
Wanaopaswa kuchunguzwa sikiliza maneno yao, wakishirikiana na kina Pasco wa JF.

Nape Nnauye

Hili la kutekwa na kupigwa na kuumizwa kiasi hichi kaka yangu Kibanda, kila nikilitafakari maneno ya waliosema hakutatawalika na makala za Kibanda mbili au tatu za mwisho kabla ya kuhama chombo cha habari kabla ya anachofanyia kazi sasa vinajirudia kichwani mwangu sana! Get well soon brother!

Sote twamjua Nape kuwa hatumii akili hasa azungumziapo mambo nyeti yawezayo kuitia nchi hii machafukoni. Nilishasema kuwa wanaotafuta sababu nyingine zaidi ya zilezile zilizommwagia tindikali kubenea, zilezile zilizomuua Mwangosi, sababu zaidi ya zile zilizomteka Dk. Ulimboka, wanaotafuta sababu zaidi ya zile wanajaribu kujikinga mvua kwa mwamvuli wa wavu. Mwisho watalowana tu!
 
Huu nadhan ni mpango mahusus wa kuangamiza wanaharakat, kwenye gazeti la raiamwema lililopita kulikuwa na habari kuhusu kumwangamiza mmoja wa waandishi wake anayeishi inchin wingereza ila wapelelezi wa nchi hiyo waliufichua mpango huo na kumpa ulinzi, mpango huo inawezekana una orodha ya waandishi wengine makini akiwamo huyu bwana kibanda
 
Nadhani tathmini yako potofu matukio ya aina hiyo hayafanani. Yale yaliyojidhihirisha kupigwa au kuuawa na askari yanakuwa katika mazinzingira yanayojulikana. Ungekuwa mchambuzi mzuri unge-cite matukio yanayofanana. Kupigwa risasi na kuawa kwa padre zanzibar na hili la kibanda ambapo wahalifu hawajulikani. Hii ni mifano ya kufanya uchambuzi ni nani? Kabla sijaanza uchambuzi ningependa kueleza kuwa haya ni maoni yangu.

Kwanza kuna kundi la watu au wanasiasa ambao imma fa imma wanataka serikali iliyopo madarakani iondolewe kwa nguvu kwa sababu wameona njia ya kura wanashindwa. Ili kuiondoa SERIKali hii ni lazima wananchi waiuchikie. Juhudi zimefanyika sana kuipakazia kila aina ya sifa mbaya wakiwemo waandishi wa habari pamoja na Kibanda kuajiriwa na gazeti linaloongozwa na kundi hilo. Aidha shirika moja la dini nalo likawa limo kupigia upatu huo na viongozi wake wamekuwa wakitamka hadharani na kwenye nyumba zao za ibada kuwasihi waumini wake waichukie serikali hii.

Kuna kiongozi mmoja wa kidini amefanya safari karibu nchi nzima na kila kanisa amekuwa anaomba asalishe misa zote tatu ili kuhubiri chuki dhiidi ya seikali hii.zanzibar dini kubwa sio RC ni Anglican au Lutheran.RC iko bara. Kwanini washambulie dini ndogo? Nadhani lengo ni serikali ya muungano ndio isiyotakiwa.pili kibanda amehamia magazeti ya mkereketwa wa ccm ambayo ndio inayoongoza serikali ya sasa.

Hivi kweli serikali au CCM ifanye hivyo ili izidi kuchukiwa na wananchi wake? Hebu jiulize ni chama gani hapa nchini mwanachama wake akihama hutukanwa hushambuliwa na hata kuuawa? Chama gani kinachochochea vurugu na kusababisha mapambano na dola? Haya ni maswali ambayo mwenye busara ndio anayotakiwa kuyajibu.
 
Back
Top Bottom