Kikwete: Muda wa kampeni ya katiba bado

Kikwete: Muda wa kampeni ya katiba bado

Huyu Prof. bure kabisa kichwa maji anashindwa kusoma alama za nyakati
 
Yaani watanzania milioni 45 tusijadiliane na kuichambua katiba yetu hadi Dhaifu mmoja aitwaye Jakaya Mrisho Kikwete ATOE RUKSA. Kama katiba ya zamani imempa mamlaka makubwa kiasi hicho inabidi ichomwe moto haraka
 
Ha,ha,ha,ha CCM ni majanga matupu bank zinavamiwa na kupolwa mabilioni ya shilingi,majambazi wanakamatwa na kufungwa huduma za kibenki zinaendelea kama kawaida na haziwezi kusitishwa kwa kuogopa kupolwa kwa mara nyingine.Kwenye katiba wafanyavurugu hawawezi kudhibitiwa kwa kuwa wamekuwa ni bora zaidi kwa CCM zaidi ya mamilioni na malioni ya watanzania wanaohitaji kupata elimu ya katiba.
 
Siyo kazi ya Rais kuwapangia wananchi nini cha kufanya na nini si cha kufanya hasa katika haki ya kukusanyika, haya si moja ya majukumu ya Rais.
 
Habari hii iwafikie UKAWA hasa CHADEMA,wananaharakati,na iliyokuwa tume ya Warioba ambao ni vinara wa kutozingatia sheria kabisa NA KUHESHIMU UTAWALA WA SHERIA.
Wewe ni mtu wa hovyo na usie na busara hata kidogo! kwa hiyo huyo aliyetoa hilo tamko yuko juu ya sheria? au yeye ndie mwenye haki ya kuipigia kampeni katiba yake hiyo ya hovyoo! Tanzania ni yetu wote na tutabanana humuhum!
 
KAMPENI BADO MUDA !!!sawa na huu waraka ni nini???sio kampeni ile!!Fumbo mfumbie mjinga mwerevu ataling'amua(UKAWA)mnataka kupiga kampeni wakati wengine wamezuiwa,NO way imekula kwenu
 
Haraka yote ya nini nibkukurupuka na kiherehere muda bado tulizeni au ni posho na upigaji wa hela kwenye vyama vyenu ndo unawatia wazimu matokeo yake hamueleweki bora mpigwe tu
 
Nashindwa kuielewa ccm na viongozi wake. Kwani hivi sasakinachofanyika ni kampeni au ni elimu kuhusu katiba?? Mbona maccm huwa hamna hoja?
 
Ninaogopa kutaja sifa halisi ya huyu mtu aitwaye kikwete nisije nikatukana.

Ila wanaojua alichosomea na passes zake naomba waziweke hapa ili pengine niweze kuelewa huyu ni kiumbe wa aina gani kichwani.

Sifahamu kama aliposema watanzania waisome katiba na wailewe ili wafahamu nini watakuwa wakikipigia kura, maneno haya yalikuwa ya kwake au ya mbayuwayu.

Anaposema muda wa kampeni bado wakati yeye tayari anafanya kampeni ya lazima na hata ameamrisha rushwa itumike kulazimisha katiba inapita anataka kuliaminisha taifa lifahamu lina raisi wa aina gani. Sijui kama alikuwa anasoma hotuba ambayo hakuipitia mapema au ndio upeo wake wa kufahamu na kumanage mambo uko chini kwango hicho.

Ninachelea napata mashaka na hata uwezo alio nao wa kuongoza familia yake.

Naogopa kusema zaidi nisije kunena yasiyonipasa.

Habari hii iwafikie UKAWA hasa CHADEMA,wananaharakati,na iliyokuwa tume ya Warioba ambao ni vinara wa kutozingatia sheria kabisa NA KUHESHIMU UTAWALA WA SHERIA.
 
Mbona yeye and Co wanasema katiba nzuri, hiyo siyo kampeni!? Anadhani wa Tz wajinga?

Sijawahi ona rais mnafiki kama huyu!! kwa wao sawa lakini wengine hapana! Ni aibu mkuu wa kaya kuruhusu aibu hii kisa kutetea serikali mbili na akiba nje ya nchi huku madawa hospital hakuna!!!

Mungu tuokoe watanzania!!!
 
mke wa Kikwete juzijuzi katika mikutano yake alikuwa anawaambia wanawake wenzake waipigie katiba inayopendekezwa kura ya ndio,mbona ameshindwa kumkemea mtu anaye kuwa nae nyumba moja? kwa kweli hila za ccm zimepitwa na miaka wale sio wakati
Hata TBC wanaendelea kupiga debe ati wanaelimisha!!! Kikwete hapo hana maana! Waache watu wajadili na kudadafua ili ustaafu kwa heshima lakini mpaka dk.hii nakuona kigeugeu na mzabizabina!!!
 
"Onyesha kwamba una akili timamu kwa kuikataa katiba ya 6 na vijisenti" kauli mbiu yetu.
 
Kauli kama hizi ndizo zinazomfanya Kikwete adharaulike na kila mwenye akili. Siku anakabidhiwa alisema anawaomba watanzania waikubali. Akiwa Mwanza akarudia tena, na jana Dodoma tena amerudia hivyo hivyo.

Huyu Rais wetu huwa haelewi anachosema mwenyewe. Akitamka yeye na wahuni wengine wa CCM kama akina Makonda siyo kampeni ila akitamka Warioba, Maalim Seif, Lipumba inakuwa kampeni! Disgusting.

...Profesa wetu anakremishwa cha kusema mkuu na bahati mbaya akili za kuambiwa hachanganyi na zake.. Hawa akina Sitta na Chenge sio wazuri hata kidogo wanamdhalilisha sana rais wetu.
 
Ila yeye alipowatangazia wananchi kupiga kura ya....si slifanya kampeni?....hapa ni jino kwa jino.
 
Prof wa kichina akumbuke mwinyi alizabuliwa kofi lkn yeye naona itakuwa zaidi ya hapo akistaafu.
 
WARYOBA sasa atulie MIKOCHENI na SIGARA zake.

ila Kikwete na Nape wao wanaruhusiwa kuanza kampeni mapemaaaa kwa kuwa sheria za tanzania haziwahusu maana wako juu ya sheria siyo? Rais mwenyewe alishaanza mapema kuwaambia wananchi wajiandae kupiga kura ya ndiyo. leo hii ndio anasema muda wa kampeni bado. I am not disappointed because i never expected anything better from him.
 
mke wa Kikwete juzijuzi katika mikutano yake alikuwa anawaambia wanawake wenzake waipigie katiba inayopendekezwa kura ya ndio,mbona ameshindwa kumkemea mtu anaye kuwa nae nyumba moja? kwa kweli hila za ccm zimepitwa na miaka wale sio wakati

Hapo kwenye red, Kitanda kimoja, supposedly!
 
Ninaogopa kutaja sifa halisi ya huyu mtu aitwaye kikwete nisije nikatukana.

Ila wanaojua alichosomea na passes zake naomba waziweke hapa ili pengine niweze kuelewa huyu ni kiumbe wa aina gani kichwani.

Sifahamu kama aliposema watanzania waisome katiba na wailewe ili wafahamu nini watakuwa wakikipigia kura, maneno haya yalikuwa ya kwake au ya mbayuwayu.

Anaposema muda wa kampeni bado wakati yeye tayari anafanya kampeni ya lazima na hata ameamrisha rushwa itumike kulazimisha katiba inapita anataka kuliaminisha taifa lifahamu lina raisi wa aina gani. Sijui kama alikuwa anasoma hotuba ambayo hakuipitia mapema au ndio upeo wake wa kufahamu na kumanage mambo uko chini kwango hicho.

Ninachelea napata mashaka na hata uwezo alio nao wa kuongoza familia yake.

Naogopa kusema zaidi nisije kunena yasiyonipasa.

Ngoja tuone hiyo media campaign aliyoandaa yenyewe itaitwaje maana si hataki kampeni zipigwe? na si hataki wananchi wajadiliane kuhusu katiba yao? Sasa nchi hii itakuwa ya namna gani kama watu hawawezi kukusanyika na kujadili mustakabali wa nchi yao? ni jukumu la vyombo vya usalama kuhakikisha ulinzi unakuwepo. Tatizo ni kwamba vyombo hivi siku hizi vimekuwa ndio vinavyotumika kuanzisha vurugu kwenye mikutano ya CDM. Jeshi la polisi halifahamu tena wajibu wake. Shame on PT, shame on JK!
 
Halafu lipo lile kundi linalodai wao katiba walishaisoma na kuielewa! Dunia hii haiishi vituko.
 
Back
Top Bottom