Kikwete: In Black And White


Asante sana mkuu kwa data hizi. Najua kuna baadhi walikuwa hawajui. Na kama ulivyosema ni hekima kutumia lugha ya kistaarabu. Nia ni kumfaahamu mgombea vema. Unajua hotuba za mwalimu zinatuongoza kwa mengi.

Ina maana Ridhiwani si mtoto wa Salma? Salma na JK wana watoto wangapi? Na hao wengine mama yao ni nani? Je mke wake wa kwanza bado yupo au walitalikiana na kama kuna data zozote?
 

Jamani Mutu asante sana mwaya. Ila jamani si ungesema sasa huyo Nguza alimuingilia kwa kimada chake kipi? Au ndiyo maneno ya mitaani hayo? Asante mwaya.
 
Nadhani kuwa jambo kubwa lililoanza kumletea umaarufu Kikwete miaka ya tisini lilikuwa ni insubordination fulani ambapo alitakiwa kuidhinisha nyaraka fulani akiwa naibu waziri wa maji, nishati na madini. Aliona kabisa kuwa nyaraka zile hazikuwa na maslahi kwa nchi akaamua kwenda kumwuliza Nyerere moja kwa moja huko Butiama namna ya kushughulikia nyaraka zile bila hata kumhusisha waziri wake na rais wake Mwinyi wakati huo.

Haijulikani Nyerere alimshauri vipi ila alikataa kabisa kuidhinisha nyaraka zile na kuziwekea kizingiti kikubwa sana kwa Raisi Mwinyi, jambo ambalo lilimkera sana bosi wake (Waziri wa maji na nishati) na Waziri wa fedha (Malima.) Hata hivyo kitendo kile kilifurahiwa sana na Mzee mwinyi pia akampandisha cheo kuwa Waziri Kamili wa Maji na baadaye kuwa Waziri wa Fedha.

Akiwa waziri wa fedha alibana sana mianya ya misamaha ya kodi na wafadhili (nachukia sana neno hili) wakafurahishwa sana utendaji ule na kurudisha tena imani kwa serikali ya Mwinyi. Kipindi hicho ndipo nyota ya Kikwete ilipopanda sana na kuna wakati Mwinyi alikuwa akiwajibu watu wanaoomba misamaha ya kodi kuwa " Ombi lenu ninalielewa ila sintawasaidia lolote kwa sababu Jakaya mkali"
 
Jamani Mutu asante sana mwaya. Ila jamani si ungesema sasa huyo Nguza alimuingilia kwa kimada chake kipi? Au ndiyo maneno ya mitaani hayo? Asante mwaya.

kweli ni maneno ya mtaani ,ila maneno ya mtaani si maneno?.
Mtaani ndio ushahidi watu tunao .................... ila nadhani unaposema maneno ya mtaani unamaanisha kuwa habari zisizi na uhakika.

Ila bigi lady shuhuda wa mashuda wako mtaani na ndio wanasema haya yote.
Kuna watu wanapicha za mkulu akipiga mtungo ilala kabla yakuwa mkulu tena za video ila hiyo tunaweka pembeni ngoja tuongelee ya msingi (maana hapo hajavunja sheria ni raha zake).

Big Lady tusitoke sana nje ya mstari najua utapata hamu ya kujua mengi ila mambo mengine bora usijue mwenyewe najuta kujua hili.
 

Hii ni habari njema sana kujua jinsi alivyo mzalendo na kutanguliza mbele maslahi ya Taifa.

Je, kwa maoni yako Kikwete uliyemzungumzia hapa ni yule yule wa leo? Kama kuna tofauti ni ipi na imesababishwa na nini?
 

Mmmh, hii ni habari kubwa. Any way tuyaache hayo. Unafahamu chochote juu ya details za watoto wake 8 na mama zao?
 

Ni kweli hata mimi Nilikuwa shabiki but kwa sasa namjua kiundani Sorry sipo huko tena!!
 
Mkapa hakuwa amefanya cha kukumbukwa alkini baada ya kuingia madarakani alifanya mengi saaana japo kulikuwa na dosari dnogo ndogo.
Naunga mkono hoja kwa 90% mkuu!!
 
Henge:
Ni kweli hata mimi Nilikuwa shabiki but kwa sasa namjua kiundani Sorry sipo huko tena!

Henge, unaweza kutuhabarisha unavyomjua kwa undani?
 

mkuu,hapa ipo sawa kweli??
 
Tena Muache kuwadanganya watu digrii ya uchumi hawezi kupata huyo hata siku moja na hana aliyonayo ni degree inaitwa Political Economy yaani siasa ya Uchumi but it is still under political science. Sasa mnahaibisha degree za watu wenye vichwa vyao makini waulize wachumi kina Lipumba ndo wanaijua Economics ni nini?
 

Hebu tuweke vizuri, ni degree ipi aliyonayo JK
Bachelor of Economics au
Bachelor of Political Economy?
 
Mmmh, hii ni habari kubwa. Any way tuyaache hayo. Unafahamu chochote juu ya details za watoto wake 8 na mama zao?

Najua Ridhiwani na mwengine wa kike si wa Salma, Na kuna binti mmoja alikuwa akisoma magogoni white mrembo ni binti wa mkulu alizaa na secretary wake ...binti huyo alikuwa so cool.

Ila hope ni vyema kujua private life ya kiongozi ila isiwe kigezo na tusitumie vibaya.Itatumika vibaya kama tu wao watashift kwenye smear za namna hiyo.Huyu salma alikumwoa alipoenda mtwara na familia ya salma ipo pale changombe.

Na kitu ambacho wanaome tunatakiwa kuwa makini ni ukiwa unapiga sana nje unamsahau mke wako hata muda tu wakuwa pamoja ,basi very likely akapata faraja sehemu nyingine. CHECK KWA WANAO JIFANYA VIWEMBE NA KUSAHAU WAKE ZAO.

CCM acheni siasa za personal life maana habari zilizo hifaziwa ni kwa heshima.
 
Na kitu ambacho wanaome tunatakiwa kuwa makini ni ukiwa unapiga sana nje unamsahau mke wako hata muda tu wakuwa pamoja ,basi very likely akapata faraja sehemu nyingine.

Ok Mkuu tunakupata:

So Ridhiwani na mwingine wa Kike - Si wa Salma Kikwete

Binti - aliyesoma magogoni - Alizaa na secretary wake. Swali ni Secretary wake yupi kama hutajali kufafanua? Je, alikuja kumwoa naye?

Familia ya Salma Kikwete iko Chang'ombe - Any details?

Maandishi ya Blue in Bold - yana uhusiano gani na JK?
 
Namwonea huruma JK pindi atakapotoka madarakani, kama hafahamu basi namkumbusha kuwa ni wakati wake wa kuandaa mazingira mazuri pindi akistaafu apewe heshima yake kama kiongozi aliyetumikia taifa, anaendeleza mchezo wake wa hila kwa kuwachafua wenzake kupitia vyombo vya habari.

Hii dhambi itakuja kumrudi na tena mara mbili pindi atokapo madarakani, na hii itakuwa kwa yeye na familia yake, akumbuke mla huliwa, amefika mbali hata kutumia magazeti yanayoendeshwa na kodi za walala hoi kuwakashifu wagombea wenzake tena kwa kuingilia maisha binafsi ya mtu.

Uungwana ni vitendo, watu wanayajua mengi kuhusu maisha binafsi ya JK na rafiki zake na wapo kimya, kwani wanajua hatuchagui mtu kwa misingi ya maisha binafsi bali uwezo binafsi wa kuliongoza taifa, ole kwa JK na Mkuchika mnaobariki ushabiki wa kipuuzi unaofanywa na vyombo vya habari kwa maslahi yenu, historia itawahukumu
 

Mkuu angalia thread ya KIKWETE: In Black and White.

Mods tunaomba mziunganishe.
 
Jakaya Mrisho Kikwete ni moja kati ya Watanzania wanaogombea kiti cha Urais wa Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM. Katika kipindi cha miaka 5 iliyopita yeye ndiyo amekuwa Rais wa JMT (Jamuhuri ya Muunganao wa Tanzania).
Lakini je, Kikwete ni nani hasa?
Katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikuwa mwanaharakati wa siasa za wanafunzi na alichaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Serikali ya Wanafunzi ya Chuo Kikuu hicho, mwaka 1973-1974.
Makamu wa RAIS MWANAUME PEKEE TOKEA CHUO HICHO KIANZE HADI LEO
 

Source: https://www.jamiiforums.com/uchaguz...a-ya-ndoa-ngono-ya-wanasiasa-wa-tanzania.html
 
KIkwete ndiye aliyejenga chuo kikuu cha dodoma kitakachochukua wanafunzi 40,000
Kikwete ndiye amenunua Panton za Kigamboni.
Kikwete ndiye anataka kuleta mradi wa mabasi yaendayo kasi ( nenda ferry) kaone umeenza
kikwete anataka kujenga daraja la Kigamboni
KIkwete amefanikiwa kumaliza mpasuko wa kisiasa Zanzibar
Kikwete ameleta mfumo wa kura za maoni za wanachama wote wa CCM na kuwa chama pekee nchini kuwa na mfumo huu (demokrasia ya kweli)
Kikwete ameweza kuboresha sheria ya madini.
Kkwete kaongeza idadi ya wanawake ambao ni mama zetu katika uongozi.
Kikwete kaimarisha takukuru hadi ikakamata wanaCCM wenzie.
Kikwete kaleta uhuru wa vyombo vya habari, mfano, hapa JF tunazungumza kwa uhuru bila bughuza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…