Kikwete: Chagueni kijana kunirithi

Kikwete: Chagueni kijana kunirithi

Ujana ccm miaka mingapi? Tuna katibu wa vijana huku kwetu ana wajukuu
 
Aliyekuwa na uwezo wa kuwashawishi watz kuhusu kiongozi wa kumrithi ni Nyerere tu, tena kwa kuwa tulikuwa tumelala. Sio sasa na hasa kama anayetushawishi ni JK. Akae pembeni tunajua tunayemuhitaji, yeye asubiri kuhesabu mazuri yake na mabaya yake watz watayaainisha.
 
Watanzania hatutaki kabisa rais dhaifu kutuongoza namna ya kupata rais bora. Tangu alipoingia ikulu hakuna kitu alichofanya kikaleta matokeo mazuri kwa hiyo tukiingia mkenge na kumsikiliza tuchague anayempenda yeye tumeumia!
ulitaka akuzalishe ndo ujue kwamba kafanya la maana? barabara, maji, mashule, mavyuo, umeme, mahosipitali na mengine mengi hayakutoshi?
 
Hofu tu inamsumbua,anajua akiingia yeyote kati ya Lowassa,Wassira,Sitta,Sumaye ama Mwandosya si ajabu hata simu zake zitakuwa hazipokelewi ikulu,ni Rais dhaifu aliyeiongoza nchi kwa majungu tu.Na anaelewa fika kuwa japo mama na mtoto wanampigia debe Joka la Mdimu,yeye binafsi hana imani na joka la mdimu(litamgonga kisigino mchana kweupe)
 
Sio kijana tu, bali awe na sura nzuri pia, yaani mtanashati. Hii ndio blanda mojawapo tuliyoifanya kama watz.
 
ben ulitaka akuzalishe ndo ujue kwamba kafanya la maana? barabara, maji, mashule, mavyuo, umeme, mahosipitali na mengine mengi huvioni? hebu wakati mwengine muandike vitu vyenye uhalisia na sio porojo.

Badala ya kujadili mageuzi ya kimfumo anajadili sura za watu

Yeye alikua na muonekano wa ujana akafanya nini ?Tena kwa kauli zake atawatia nuksi hata wagombea wenye haiba ya ujana

Reasoning capacity za aina hii tukianza kuzihoji tutaishia kuonekana tumemu-insult bure !
 
Ujana nao ni sifa ya kuwa rais wa nchi.. CCM hebu tupisheni mmeshashindwa kuongoza nchi, mmebakia mipasho tu sasa.
 
Hivi membe ni kijana???membe atakuwa mkubwa sna,alidumaa tu kwaajili ya shida alivyokuwa mdogo,ukitaka kujua ni mkubwa msogolee umuone na hilo domo lake
Amesema anayefafana na kijana kama yeye alivyokuwa wakati anagombea(miaka 55). Hapa haongelei umri bali mtu anavyo act.
Huyu anampigia kampeni Membe.
 
ben ulitaka akuzalishe ndo ujue kwamba kafanya la maana? barabara, maji, mashule, mavyuo, umeme, mahosipitali na mengine mengi huvioni? hebu wakati mwengine muandike vitu vyenye uhalisia na sio porojo.

Yote hayo kwa hela za kukopa na kutuongezea deni la Taifa.

Mifuko ya jamii wameifilisi kwa kukopa kujenga chuo cha UDOM n.k matokeo yake sasa wanataka kumbebesha huo mzigo mfanyakazi anapostafu kwa kumdhulumu mafao yake ili mifuko isife jumla.

Wameshindwa kubuni vyanzo vya mapato na kukusanya kodi sasa wanatekeleza ahadi zao kwa hela za kukopa na mwisho wa siku mwananchi ndio anaeumia.

Bora hata Mkapa aliacha hela ya kutosha ila huyu wa sasa atatuachia madeni tu.
 
Lowass 61 na Membe 61; nani mzee kati ya hao? Mvi sio uzee!!!!

Huu umri ni wakusomea au wakuombea kazi? Hawa watu waliozaliwa kabla ya uhuru kujua tarehe zao halisi za kuzaliwa ni kazi kwelikweli.

Mfano mtu anatoka familia za wafugaji, sanasana mzazi wake atakuambia, "ero wakati wasiri na saliwa ile maksai yangu kubwa kabisa ndio na anza kupanda" Niambie hapo utajua ni tarehe ngapi? Utaishia kubunia tarehe na kufoji cheti.
 
unachekesha.
sishangai wewe ni graduate wa UDOM.
huelewi hata hiyo miradi inatekelezwaje.

Yote hayo kwa hela za kukopa na kutuongezea deni la Taifa.

Mifuko ya jamii wameifilisi kwa kukopa kujenga chuo cha UDOM n.k matokeo yake sasa wanataka kumbebesha huo mzigo mfanyakazi anapostafu kwa kumdhulumu mafao yake ili mifuko isife jumla.

Wameshindwa kubuni vyanzo vya mapato na kukusanya kodi sasa wanatekeleza ahadi zao kwa hela za kukopa na mwisho wa siku mwananchi ndio anaeumia.

Bora hata Mkapa aliacha hela ya kutosha ila huyu wa sasa atatuachia madeni tu.
 
Kwanza alianza na dhana ya "zamu ya mwanamke." Aliposhindwa kumuuza Asha Rose ndipo sasa anakuja na dhana ya ujana. Awaache Watanzania wajichagulie wenyewe. Marekani na ukongwe wake wote katika demokrasia hivi sasa wanamshupalia Hillary Clinton mwenye umri wa miaka 68. Uongozi si ujana. Ni weledi na uzoefu. Kama akionekana kijana mwenye weledi basi tumkubali, si kulazimisha.

Jamani tumsamehe huyu ndiye Mhe Dkt JK akionesha rangi zake halisi. Master Msanii. Pamoja na kukaa ikulu miaka kumi kichwa kimeendelea kuwa cha nazi. Bado mtu wa miaka 55 naye ni kijana kwake (amejitolea mfano). Kwa bahati mbaya hakuwa na vision wakati anaingia ikulu na wala hana busara yo yote anayoweza kuachia jamii. Utazungumzaje kuhusu ujana badala ya uwezo. Lakini kutokana na usanii, anafikiri hapo atawapumbaza vijana (kwa wingi wao) wamshangilie- hilo ndilo alilotaka: kushangiliwa!!! pathetic!
 
Lakini ana hoja,MTU kama wasira na miaka sabini amuongoze nani? labda chuki Uchaguzi Pawaga na Mtu was tanga,na mpaka kikwete kasema hivyo kamuona wasira jinsi anavyotumia muda mwingi kusinzia ofisini na kukoroma,na inawezekana alishaweka godoro na shuka ofisini,si unajua wako ofisi ya raisi
 
Last edited by a moderator:
Yaani vijana wa CDM maneno yamewatoka mengi sana kupinga kauli ya ujana kwasababu nyie tayari focus yenu ipo kwa Babu Dr Slaa ambaye Ana umri wa miaka 76.

Yaani kelele nyingi sana kisa Babu siyo kijana, any way Rais kasema mrithi wa CCM atakayepeperusha Bendera ya CCM siyo Bendera ya CDM wala CUF wala NCCR Mageuzi!

CDM tunajua tayari kuna Babu 76, CUF Kama kawa Mzee wa Uyuwi Tabora Le professor!
 
Back
Top Bottom