Katika hotuba yake kwa mawakili wa Tanganyika Law Society kwenye hafla ya kuchangia fedha za kuanzisha Kituo cha Msaada wa Kisheria (Legal Aid), hafla iliyofanyika Ijumaa usiku tarehe 31 Oktoba, 2008 kwenye viwanja vya Karimjee, Rais Kikwete alitahadharisha uwezekano wa mhimili moja kuvuka mipaka yake na kuingilia shughuli za mihimili mingine ili "kujipendekeza kwa wananchi ama kwa sababu ya ubinafsi, ama kwa kisingizio kuwa mihimili mingine haifanyi kazi yao vizuri". Akataka Watanzania wakatae hali hiyo!
Mawakili wote waliokuwepo kwenye hafla hiyo walielewa maana ya kauli hiyo ya Kikwete: ilimlenga Sitta na Bunge lake la "viwango na kasi", ambalo hivi karibuni limekuwa mbele kuisukuma Serikali kuchukua hatua kuhusiana na EPA, Richmond, Twin Towers na uozo mwingine. Inaonesha kuwa Kikwete alikerwa sana na hatua ya Sitta "kumshauri" kuwa mkali kidogo katika kushughulikia mafisadi baada ya Kikwete kutoa hotuba ambayo wengi waliita ya "mdebwedo" Bungeni.
Maoni yangu:
(1) Bunge chini ya Sitta linatimiza wajibu wake vizuri. Hivyo Rais na yeye atimize wajibu wake sawasawa! Asipofanya hivyo, ni halali kwa Sitta na wabunge wengine kumsukuma atimize wajibu wake!
(2) Kama ni suala la kuingilia madaraka ya mihimili mingine, Rais Kikwete na wasaidizi wake wamevunja rekodi. Uamuzi wa kuwabagua watuhumiwa wa wizi wa fedha za EPA kati ya kundi la kushitakiwa na kundi la kuendelea kutesa na fedha za wizi, ni kuingilia wajibu wa kikatiba wa mhimili wa mahakama!
Mawakili wote waliokuwepo kwenye hafla hiyo walielewa maana ya kauli hiyo ya Kikwete: ilimlenga Sitta na Bunge lake la "viwango na kasi", ambalo hivi karibuni limekuwa mbele kuisukuma Serikali kuchukua hatua kuhusiana na EPA, Richmond, Twin Towers na uozo mwingine. Inaonesha kuwa Kikwete alikerwa sana na hatua ya Sitta "kumshauri" kuwa mkali kidogo katika kushughulikia mafisadi baada ya Kikwete kutoa hotuba ambayo wengi waliita ya "mdebwedo" Bungeni.
Maoni yangu:
(1) Bunge chini ya Sitta linatimiza wajibu wake vizuri. Hivyo Rais na yeye atimize wajibu wake sawasawa! Asipofanya hivyo, ni halali kwa Sitta na wabunge wengine kumsukuma atimize wajibu wake!
(2) Kama ni suala la kuingilia madaraka ya mihimili mingine, Rais Kikwete na wasaidizi wake wamevunja rekodi. Uamuzi wa kuwabagua watuhumiwa wa wizi wa fedha za EPA kati ya kundi la kushitakiwa na kundi la kuendelea kutesa na fedha za wizi, ni kuingilia wajibu wa kikatiba wa mhimili wa mahakama!