Kikwete anamfahamu Al Adawi!

HII HAPA YA UKWELI KABISA..........

in_news1.jpg


Kwa hiyo Zengwe mpaka kwenye Identity halisi ya mtu...yaani wanatuletea mtu ambae sie....kweli nimeamini serikali tunayo
 
Nchi hii tumefika kubaya, kila mtu bei yake inajulikana. Wahariri wote bei yake inajulika. Haiwezekani mtu yuko hapa nchini halafu uniambie eti aemekataa kupigwa picha ndo maana hazipo magazetini!! Huu ni uzushi. Kwani wale polisi waliokamatishwa na Jerry Muro wakati wanapokea kitu kidogo waliruhusu wapigwe picha!

Yaani kinakuja chanzo cha habari muhimu kama mtu anayejiita mmiliki wa Dowans Tanzania halafu vyombo vya habari viseme eti amekataa kupigwa picha!! Mambo mengine ni ya c.h.o.o.n.i. kabisa hata kuyasikia inatia kichefu chefu. Kifupi ni kuwa media house zote hapa bongo zinanunulika kama mtumba wa mmachinga mtaani. Hawataki kutoa hiyo picha sababu wameshalishwa.

Ni afadhali mkaeni kimya, lakini msiseme eti mmekosa picha kwa sababu huyu mtu kagoma kupigwa picha!! wapi na wapi! Wote tunaonana mazuzu tu.
 
Au ndo kama yale yale ya Gongo la Mboto! Mabomu yamelipuka, vyombo vya habari vinakimbilia ofisini kwa kova kutafuta habari!! Halafu mnalalamika eti hampewi habari! Hakuna habari yenye thamani inayojitoa tu. Ndo maana kina Asange wamekuwa Ma supa staa wa Dunia. Ikiwa kazi ya vyombo vya habari ni kwenda kusikiliza official opinion tu basi wakati wa Nyerere tulikuwa na vyombo vya habari bora kuliko sasa.

Mtu yuko nchini, tena mnabwata kuwa mmeongea naye, tukiwauliza tupeni picha yake mnasema eti kakataa kupigwa picha!! Nivyi wenyewe mlioandika hiyo habari kuwa yupo ndo waongo. Hayo yote mnayosema eti kasema, mmepewa ili muandike! Vinginevyo vyombo vya habari hamwezi kufanya press conference na mtu hewa halafu habari yake ndo inatawala vichwa vya habari!!

huuu ni wizi mtupu!!
 
INAKERA!, INATIA KINYAAAAAA! Tz ya sasa na ya kesho inamalizwa ndani ya sekunde chache, watanzania kilichobakia, tuache porojo za kulalamika, kulalamika hakuzai kauli ya kutenda na kuthubutu, wana JF naombeni tuituimie JF kwa ajili ya kupanga mikakati jinsi ya kuinusuru hii nchi, tutumie mifano ya wenzetu waliofanikiwa kuwaondoa hao kupe! walifanikiwa kwa kupeana michapo na jinsi gani ya kuwaondoa kwa njia ya Facebook na mitandao kama hii yetu ndo mana unaona kitu cha kwanza hao kupe wanaanza kufunga hizi asasi, lakini wanakuwa wameshachelewa, unga unakuwa ushatiwa mchanga! Yani apa nuilipo sina hali natamani ata nijitoe mhanga, inakera kwa kitendo anachokifanya Mkwere na vibaraka wake akina Ngereja! Kumbe ndo mana walikuwa wamechachamaa DOWANS iwashwe, iwashwe! mara JK analidanganya taifa kuwa wanaangalia jinsi gani wanaweza kuyanusuru hayo mabilioni ya pesa, sasa tushike lipi tuache lipi, kwa sababu sa ivi tunasikia sa ivi waqnawaomba wawashe, watawaombaje uku wanadaiwa na bado wamewapeleka mahakamani? Arooooo Kikwete, aise acha kutuchafua akili, Mubarak, amekuacha bt Swaiba ako Gadafi hakuachi! nakwambia anaondoka na wewe, coz tumechoka! Halafu hao waandishi habari wasio na taaluma walikuwa wanachukua habari gani, ahalafu wampelekee nani? si sio vipofu tusiohitaji picha, tunahitaji kumfahamu huyo mwizi wetu ili tumalizane nae, na wala hatutaki cha mahakama mana ndo wale wale!! ITV na Radio One mmesema mtakuwa na mjadara juu ya hili, hakikisheni mnatuletea na picha yake huyo jamaa, la sivyo na nyie bora mukaacha coz itakuwa ni umbea tu.
 
nadhani MMMJ atakuwa anamjua vilivyo,kwani ye si alishawahi kufanya mahojjiano naye huko middle east??Mwanakijiji tengua kitendawili hiki
 
Nchi hii tumefika kubaya, kila mtu bei yake inajulikana. Wahariri wote bei yake inajulika. Haiwezekani mtu yuko hapa nchini halafu uniambie eti aemekataa kupigwa picha ndo maana hazipo magazetini!! Huu ni uzushi. Kwani wale polisi waliokamatishwa na Jerry Muro wakati wanapokea kitu kidogo waliruhusu wapigwe picha!

Yaani kinakuja chanzo cha habari muhimu kama mtu anayejiita mmiliki wa Dowans Tanzania halafu vyombo vya habari viseme eti amekataa kupigwa picha!! Mambo mengine ni ya c.h.o.o.n.i. kabisa hata kuyasikia inatia kichefu chefu. Kifupi ni kuwa media house zote hapa bongo zinanunulika kama mtumba wa mmachinga mtaani. Hawataki kutoa hiyo picha sababu wameshalishwa.

Ni afadhali mkaeni kimya, lakini msiseme eti mmekosa picha kwa sababu huyu mtu kagoma kupigwa picha!! wapi na wapi! Wote tunaonana mazuzu tu.

Kwa mnaoishi nchi za magharibi nadhani mnaelewa maana ya neno PRIVACY.
 
Kwa mdadisi yeyote ziara ya anayejihita mmiliki wa Dowans Brig.Gen.Al Adawi inazua maswali mengi kuliko majibu; kwanza kwanini hakutaka kupigwa picha?

Pili katika hali ya kawaida R.A kama mwakilishi wake ndiye mwenyeji wake, hivyo alitakiwa awepo katika mkutano wake na wahandishi wa habari kwaajili ya kumtambulisha, inaonekana hilo halikufanyika.

Tatu ameingia tu na mtambo mmoja wa Dowans ukawashwa. Haiwezekanikuwashwa huko kwa mtambo huo ukatokana na mashauriano ya siku moja.

Inavyoelekea mipango yote tayari ilikwisha andaliwa, haya yanayotendeka sasa ni kiini macho, ndiyo maana kuna tetesi ya kwamba hata huyo anayejihita Brig. Gen. Al-Adawi uenda hasiwe mwenyewe bali kivuli chake.

Kwani hao waandishi ina maana wameshindwa kabisa kupata picha ya huyo msanii?
Kama waandishi wote wa Tanzania ambao hujinadi humu nchini tena wengine ni Seniors wameshindwa kupata picha tu ya huyo jamaa tena yeye ni mgeni na yupo humu nchini. Vipi kama waandishi hawa watatakiwa kutafuta habari za uchunguzi nje ya nchi hii?

Waandishi wetu akina Kibonde na wapiga picha wetu akina Michuzi mpo wapi?
 
Kwa mnaoishi nchi za magharibi nadhani mnaelewa maana ya neno PRIVACY.

Mmh jamani kuna issue za 'privacy', yaani leo hii mcheza sinema apeleke sinema yake sokoni halafu akatae kupigwa picha kwa kisingizio cha privacy! Atauza kweli? Watu tunatapatapa kutafuta uhalali wa kampuni na umiliki wake atuambie mambo ya 'privacy', if he was keen with his privacy he should have stayed wherever he is na hela zake benki!

In my opinion, the whole issue is cooked.
 
Kwa mnaoishi nchi za magharibi nadhani mnaelewa maana ya neno PRIVACY.

Acha uongo, hakuna privacy kwenye habari ya kawaida kama hii! Vyombo vya habari hawawezi kutumia kisingizio cha privacy kwenye suala hili. Yaani mtu yuko kwenye press conference halafu unaita kipengele cha privacy? Na hayo aliyoyasema kwa nini basi mliyaandika?? Acheni kuwalisha watu Pumba kwa kuwa tu mna vyombo vya habari!
 
Nijuavyo mimi kwenye kila hoteli (hasa hizi 4* na 5*) lazima kunakuwa na CCTV, sasa tuanzie hapo! Jamaa zetu wa hapo Movenpick, hebu kuwenu wazalendo na muwe tayari kufanya yale marubani wa Ghadafi waliomuasi!! Please eeh! Tuko nyuma yenu.....kwa mbali lakini!
 
MAFISADI MKOME HII SINEMA YA HIVI SASA JUU YA DOWANS LAASIVYO
TUKAPOROMOSHE 'MI-WIKILEAKS' ZAKE HAPA MPAKA MJISIKIE KUFAKUFA HIVI!!!

Hawa wamiliki wa Dowans wa KUKODI wala hatudanganyiki!! Lowassa na Rostam Azizi, kaundeni mpango mwingine; huu hapa tayari umeanguka kwa pua.

Na mkijaribu kubisha basi TUTAPOROMOSHA USHAHIDI KAMA MVUA HAPA kuliko hata ya Wikileaks mpaka mshangae wenyewe. Naona bora mkasimamishe hii sinema ya huyo Msaudia aliyeletwa nchini na Ridhiwani Kikwete tayari na makabrasha yote bandia, kabla hamjapata kuabika zaidi!!!!​

Hebu waonyeshe hawa mafisadi cha.....(Jina Lako! Lol.)
 
Mambo yanavyoenda nchi hii yanatia hasira sana!!! Uongo mwingine hata mtoto mdogo huwezi kumdanganya. Ninawaza jinsi mbegu hii ilivyoshamiri, na namna tunavyotakiwa kuiuproot!! Lakini yote yanawezekana! Hawa watu wanatugeuza kila siku tunavyotaka, na kuna watu wanasema wanaangalia security ya nchi na taarifa za kiintelejensia!! Tumegeuzwa wote vilaza, kiasi hata mtu kutoka sehemu nyingine anaweza kuamuru kutopigwa hata picha, na waandishi wetu wakatii, ataondoka bila ushahidi wowote kuwa alikuwepo!! Siamini kama hili limetokea...
 
Ile pichaniloiona hapa jf nimehisi ni tofauti na nikoiona kupitia google images!

Teh teh! Siku si nyingi atajitokeza another 'mburushi' atakaejiita Al Adawy halisi-hii sinema ya Dowans nadhani itavunja record za mauzo duniani! Hata hivyo, kwa sinema hii ya kihindi kumbe RA na washkaji wake si wajanja ki hivyo wala nn.
 
Back
Top Bottom