Kikwete anaishi tanzania gani?

lifeofmshaba

JF-Expert Member
Feb 19, 2011
867
219
05_11_p12qwv.jpg
Rais Jakaya Kikwete akipokea zawadi kutoka kwa Msaidizi Mtendaji Mkuu wa Uongozi Institute, Linda Manu baada ya kuzindua bodi ya chuo hicho jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa bodi hiyo, Ritva Koukku-Ronde, Waziri wa Nchi, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia na Balozi wa Finland, Juhani Toivonen



Katika pita pita yangu kwenye vyombo vya habari leo nimekutana na habari ya kusikitisha sana,
Raisi Kikwete ameanzisha taasisi ya kuwafua (shule/chuo) viongozi ili kupa viongozi WENNYE MAADILI


nilipigwa butwaa na hii habari, kwa sababau zifuatazo
  1. je maadili yanaweza kufundisha kwa kiongozi vyuoni au ni utashi wa mtu?
  2. Ni nani serikali mwenye maadili ya kutosha kufundisha wengine huko serikali?
  3. lakini pia hii ni ishara kwamba kikwete hajui nini chanzo cha viongozi wake pamoja na yeye kutokuwa na maadili?
  4. je TAKURUKU wanafanya kazi vya kutosha na wanameno? na jeshi la polisi na tume ya maadili ya viongozi wameshindwa kazi hii ya kuwanyoosha?
  5. kwa nini kikwete anataka kuendelea kufanya kazi na viongozi wasio na maadli kuhasi cha kuwapeleka shule
  6. Kikwete anaogopa nini kutumia sheria zilizopo kuleta maadili ya viongozi, ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha wanapokosea
  7. huu ni upotezaji wa pesa kwa kuwalipa watakaotoa somo kwa hao viziwi na kuwalipa posho watakaudhuria hiyo semina
kama kikwete hajui chanzo cha maadili kupolomoka ni hakika hata huko wanakwenda kufundihswa hawata fundishwa mambo yaliyosababisha kupolomoka maadili yao
hii ni pamoja na ukweli kwamba yeye ni chanzo kikuu cha viongozi hao kutokuwa na maadili kwa kuwa dhaifu katika kutoa maamuzi magumu, lakini pia rushwa na uongozi wa kupeana bila kujali sifa na anayepewa ili yeye ni mwanzilishi / mwasisi


Maadili ya viongozi uwezi kuwafundisha kwa semina au washa wengi wao ni wasomi katika taaluma zao wameshafundishwa maadili kinachotokosekana serikali kwa sasa ni uzalendo na mfumo mbovu wa uongozi wa uwajibikaji na uwajibishwaji mfano wiki iliyopita raisi Kikwete alimchagua Mrindoko kuwa Naibu waziri wa wizara ya maji, lakini huyo huyo Mrindoko ni zao la ufisadi na mmoja ya watanzania aliyeifikisha TANESCO hapo ilipo sasa na kuliingiza taifa pamoja na TANESCO hasara kubwa. Je ili nayo Kikwete anataka wakasome shuleni,
Maadili ya viongozi hayajengwi na semini wala washa yanajengwa na shirie kali zinazotekerezwa na kufuatwa, ni lini tumejaribu kutumia sheria kuwasukuma viongozi wetu kuwa na maadili ikashindikana?
Kwa nini tunawabembeleza sana viongozi wan chi hali taifa likiwa na wasomi rukuki waliotayari kulitumikia taifa lao
Kikwete kwa ili umeshemsha tena, naona bado ujajua tatizo ni nini?
Tatizo ni wewe kupindisha na kuchezea sheria za nchi kama ulivyofanya kwa wezi wa EPA, na kamwe utopata viongozi makina na wazalendo, maadili yanaalia ikulu na uzalendo ni ndio kiini pekee za maadili.
Futa hayo mafunzo yako hakuna kitu hapo ni matumizi mabaya ya pesa tu.
pencil.png
 
Kubwa la kushangaza ambalo najiuliza sipati majibu ni pale alipoongea na mwandishi wa TBC1 nakuse tanzania haina chuo cha uongozi! Hivi Public administration, Management programs mbalimbali zinazotolewa mlimani, mzumbe, UDOM na kwingineko mwisho wake ni nini? Au kwakuwa institute imeitwa UONGOZI INSTITUTE ndo upya? Kama huna lakuoshea Mkuu wa kaya kwa waandishi wa habari kaa kimyaaaaaaaaaaaaaa
 
Kubwa la kushangaza ambalo najiuliza sipati majibu ni pale alipoongea na mwandishi wa TBC1 nakuse tanzania haina chuo cha uongozi! Hivi Public administration, Management programs mbalimbali zinazotolewa mlimani, mzumbe, UDOM na kwingineko mwisho wake ni nini? Au kwakuwa institute imeitwa UONGOZI INSTITUTE ndo upya? Kama huna lakuoshea Mkuu wa kaya kwa waandishi wa habari kaa kimyaaaaaaaaaaaaaa


huyu anatupoteza kabisa sijui ana matatizo gani? kila taaluma inafundisha maadili, lakini pia maadili ni utashi wa mtu
wasio na maadili wafukuzwe
 
wadau na watz wote kwa ujumla wetu, tujipange tupambane tupate katiba itayoondoa mianya yote ya utawala mbovu. hapo tutakuwa tumepata tiba na chuo kizuri cha uongozi bora, kuliko hizi ngojera inazopigwa na hawa watu wetu
 
wadau na watz wote kwa ujumla wetu, tujipange tupambane tupate katiba itayoondoa mianya yote ya utawala mbovu. hapo tutakuwa tumepata tiba na chuo kizuri cha uongozi bora, kuliko hizi ngojera inazopigwa na hawa watu wetu

kikwete anajifanya hajui nini kimepolomosha maadili kwenye serikali yake
yeye ni chanzo kwa kudawa madalaka kwa watu wachafu kama mrindoko
anashindwa nini kumfukuza hali anajua ni mchafu bado anampandisha vyeo kila kukisha, sasa kaanzisha chuo ina maana hakuna watanzania wenye uwezo wa kuongozi machoni pake ni hao tu ndio anawaona?
 
narudia kusema tulichaagua sura badala ya kiongozi
na sisi tunakula shubiri
 
Anaishi chini ya bahari, tunaloliona ni bosheni tu na anaongoza kwa masharti ya sheikh yahya sio kwa utashi wake
 
its only madness and ufisadiat work!

msijeshangaa kuna mtu kakamata hapo dola kibao za WB/IMF au development partners. kisha watz tukajikuta tunalipa mbele ya safari!! hahah, hii ndo tz mazee
 
hii ni njia ya kula pesa ya walipakodi.je kwani
asichague mawaziri wengine ndio maana katiba inabidi ibadilike mawaziri
wasiwe wabunge lakini naye hajui kuchagua,mfano mtaalam wa energy unampeleka kwy
wizara ya maji wapi na wapi
 
ndio maana serikali inamshinda
sasa anataka kutumaliza hazina kwa kulipia haya mambo yasiyo na msingi

hii ni njia ya kula pesa ya walipakodi.je kwani
asichague mawaziri wengine ndio maana katiba inabidi ibadilike mawaziri
wasiwe wabunge lakini naye hajui kuchagua,mfano mtaalam wa energy unampeleka kwy
wizara ya maji wapi na wapi
 
Huyu ndiye yule raisi na waziri mkuu wake waosema hawajui kwa nini watanzania ni masikini-huu ni msiba wa kitaifa.
 
Kubwa la kushangaza ambalo najiuliza sipati majibu ni pale alipoongea na mwandishi wa TBC1 nakuse tanzania haina chuo cha uongozi! Hivi Public administration, Management programs mbalimbali zinazotolewa mlimani, mzumbe, UDOM na kwingineko mwisho wake ni nini? Au kwakuwa institute imeitwa UONGOZI INSTITUTE ndo upya? Kama huna lakuoshea Mkuu wa kaya kwa waandishi wa habari kaa kimyaaaaaaaaaaaaaa

Labda "definition" yake ya neno "Uongozi" ni tofauti na ile tunayoifahamu wengine!
 
uwezi kumfundisha kiongozi kuhacha ufisadi kwa kuwaomba, sheria itumike TAKURUKU wanafanya kazi gani?
 
Back
Top Bottom