anania
Member
- Jul 2, 2010
- 83
- 8
Jamani ndugu zangu imefika kipindi inatubidi kutumia hata elimu ya ngumbalo au darasa la saba kutambua kuwa hakuna kuoteshwa na Mungu wala nani.
Huyo mama wa Tabora naye kaoteshwa na Mungu? na kuhusu kijana wa miaka 17 Mbeya ipo vipi?
Kinacho fanyika ni kwamba hawa watu walikuwa wanatoa huduma ya dawa hii tokea zamani sema sasa wamesoma majira na nyakati ya kuwa wanatakiwa kutumia dawa zao kuwashika wengi zaidi kwa kudanganya kuwa wameoteshwa,ili jambo hilo liwe kiimani zaidi. na kupata baraka za viongozi wa dini na selikari.
Inasemekana dawa anayotoa huyo mama wa Tabora ina nguvu sawa na kikombe cha babu ndio maana hata bei ni ile ile na foleni ni ndefu inakaribia na ya babu,utofauti ni kwamba kikombe cha mama hakina foleni ya magari.
Na kuna watu wamejitokeza kutoa ushuhuda kuwa wamepona kwa kikombe hicho cha bibi.Kazi kwetu kutenganisha mchanga na dhahabu
Huyo mama wa Tabora naye kaoteshwa na Mungu? na kuhusu kijana wa miaka 17 Mbeya ipo vipi?
Kinacho fanyika ni kwamba hawa watu walikuwa wanatoa huduma ya dawa hii tokea zamani sema sasa wamesoma majira na nyakati ya kuwa wanatakiwa kutumia dawa zao kuwashika wengi zaidi kwa kudanganya kuwa wameoteshwa,ili jambo hilo liwe kiimani zaidi. na kupata baraka za viongozi wa dini na selikari.
Inasemekana dawa anayotoa huyo mama wa Tabora ina nguvu sawa na kikombe cha babu ndio maana hata bei ni ile ile na foleni ni ndefu inakaribia na ya babu,utofauti ni kwamba kikombe cha mama hakina foleni ya magari.
Na kuna watu wamejitokeza kutoa ushuhuda kuwa wamepona kwa kikombe hicho cha bibi.Kazi kwetu kutenganisha mchanga na dhahabu