Kikao cha dharula: Kitimoto kwa wabunge wa CCM wanaopigia kelele Escrow

Kwa katiba ya mwaka 1977 tuitumiayo kwa sasa naibu haingii kwenye kikao cha baraza la mawaziri labda katiba pendekezwa ya Chenge imeruhusu hivyo.

"The ends justify the means" nashaka na thread yaweza ikawa ni safisha njia ya Mwiguru 2015 haa..haa..haa mtazamo 2 wadau.
 
Kwani wewe huoni aibu kukopi mada ambazo wameweka watu awali na wewe kuzirudisha tena.
 
Izo kampeni tu za mwigulu wala si ajabu akawa yeye make jamaa kiukweli huwa hana akili nzur ya kupambanua mambo anapendatu ustar lakini bado sana ajipange


kwaa urais ndo kabsa hata robo bado,hana kichwa cha kua rais,umeambiwa urais ni kuvaa skafu???

We endelea tu kujilia vijisent anavyo kupa upige kelele ila mwambie ukweli bado sana usimfiche
 
Kikao kinaongozwa na Wasira na Lukuvi,

Wabunge wa ccm wale wanaopiga kelele kuhusu Wizi huu wamewekwa mtu kati,

Kinafanyikia Ikulu ya Dodoma kwa siri kubwa, hata magari yao yote yameigizwa ndani kabisa, kwa hapa nje lipo Gari la Lembeli aina ya Range Rover Namba T382 lililokosa nafasi ndani. kikao hiki kimeitishwa kwa meseji tu hii ni baada ya jioni kutangazwa kuwa kimeahirishwa,

Sababu za usiri huu ni pale tulipowaanika jana katika kikao chao cha shinikizo kwa Werema ajiuzuru, Zigo limemdondokea Godfrey Zambi kuwa ndie aliyevujisha siri ile kwakuwa aligoma kuzima simu na alikuwa akichati fb wakati kikao kikiendelea, hivyo kikao cha sasa hivi katupwanje.

Kikao hiki kwa sasa kimembana Ndugai kwamadai anaihujumu serikali,

Ndugai amezila kuendelea na Bunge amesema yeye sasa hata ongoza vikao, bora awe pembeni kuepusha msongamano!

Ccm imegawanyika makundi matatu, lile linaloshinikiza waliohusika na wizi huu wote wapigwe chini lakini,ukifuatilia kundi hili linavizia vyeo vya uwazili, na tayari kampenzi za kuwania vyeo hivyo zimeanza.

Kundi la pili hili ni wanafiki wa kati wasio na msimamo, lenyewe linataka wafukuzwe wachache (maswi,tibaijuka,mhongo na werema) hili linasema linanusuru serikali isianguke.

Kundi la mwisho ni la wezi wenyewe, hili linafanya kila njia ripoti hii isisomwe bungeni, hili linaongozwa na Pinda na Werema.
Wewe na yericko mpoje au zote aid za mtu mmoja make hii mada aliweka yeriko nyerere mda wa tano na dakika ishirini na tatu usiku naona sasa na wewe unakopi kama ilivyo tupe ufafanuzi.
 
Duh.....naibu waziri ndani ya kikao rasmi cha baraza la Mawaziri!!!
Danganya vizuri basi!

Kile hakikuwa kikao cha baraza la mawaziri. Kingekuwa hivyo kingeongozwa na makamo wa rais na siyo waziri mkuu. Ndiyo maana manaibu waziri walihudhuria.
 
Mwigulu anadhani kuwa Watanzania hawajui majukumu ya Naibu Waziri. Naibu waziri kama yeye kimsingi ni "msaidizi wa karibu" wa Waziri ndio maana hata Bungeni wao kazi yao kujibu maswali ya wizara wakati mawaziri wenyewe wanachati na simu zao. Akishindwa kujibu vema ndio utasikia " Naona Waziri mwenyewe kasimama kutoa jibu, tumsikilize"
Hivyo Mwigulu na timu yake wasipende kupotosha watu kuhusu nafasi yake maana kila atamkacho lazima kipate kibali cha bosi wake yaani Saada Mkuya laa sivyo anaweza kupigwa MEMO kali ya utovu wa nidhamu.
Saada hawezi kumpiga kimemo mwigulu kwani anajua kuwa bosi wake anavikubali vitendo vya mwigulu.saada mkuya inabidi awe mpole ama aendane na speed ya naibu wake.
 
mwambie aje aongee hadhalani kama anaweza uone ccm watakavyo mfanya uko sirini kila mtu anaweza akaropoka tu usitake kumsifu kihivyo
Mbona huwa anaongea?,umesahau hadi TBC waliwahi kucover hotuba yake kwa taifa akihutubia toka mwanza?,Na huyo ni naibu waziri anahutubia taifa.
hapana chezea mtoto wa mfugaji ng'ombe.
 
Imeamriwa popote alipo Spika Makinda aje, Ndugai out hadi sakata lipite, afanye awezavyo Pinda apone,.. Wachangiaji wakali wasipate nafasi iitwe briefing ya wabunge wote watapike nyongo nje ya waandishi ili siku ya mjadala kuwe na hewa safi.Kama ni kuondoka waondoke mawaziri ila sio waziri mkuu.

Inatakiwa njia ya kumuangukia au kumdhibiti Mh. Mengi wa IPP,

Leo agenda kuhusu Mengi itajadiliwa kwa kina katika kikao cha baadae. Ifahamike kuwa Vyombo vya habari vya Bwana Mengi vimekuwa vinalielezea jambo hili kwa uwazi na uhuru mkubwa kiasi cha umma kulielewa.
 
Naibu waziri anaingia kwenye kikao cha baraza la mawaziri? au kilikuwa kikao cha kawaida cha viongozi wa serikali.
Mkuu umeniwahi kweli. Naibu waziri si mjumbe wa baraza la mawaziri kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri. Hivyo basi kama kikao hicho kilihudhuriwa na akina Zambi na Mwigulu kitakuwa si kikao cha Baraza la Mawaziri bali kikao cha utendaji tu serikalini.
 
Back
Top Bottom