Kijue kitendo cha kibaiolojia na kikemia kinachofanya maisha yaendelee duniani

hydroxo

JF-Expert Member
Oct 19, 2015
2,808
5,585
Usanisinuru(photosynthesis);ni kitendo cha kikemia na kibaiolojia ambapo mimea ya kijani(green plants) hubadili nishati ya mwanga wa jua kuwa nguvu ya kikemia inayohifadhiwa na mmea katika sukari aina ya stachi.

Kitendo hiki cha usanisinuru hufanywa na mimea ya kijani(green plants) kwa sababu mimea ya kijani inamiliki kiwiti(chloroplasts) zenye chembe ndogo ndogo za kijani(chlorophylls) zenye uwezo wa kuvuta na kubadili mwanga wa jua kuwa nishati ya kikemikali.

Ili kitendo hiki kifanyike kinahitaji; maji,na gesi ya kaboni daioksaidi kutoka angani hivyo basi kitendo hiki pia usawazisha kiwango cha gesi hii ambayo ikizidi huwa sumu kwa mwanadamu.

Baada ya kitendo hiki kukamilika huzalisha; maji, sukari,na gesi ya OKSIJENI inayotufanya mimi, wewe na viumbe hai wengine tuweze kuishi kwani kila siku tunaitumia katika upumuaji na uvunjaji wa chakula mwilini (respiration) kitendo kinachotupa nguvu zinazotusaidia katika shughuli za maisha yetu ya kila siku.

HAKUNA MIMEA HAKUNA MAISHA.
 
Mbona hakuna wachangiaji? Au kwa sababu uzi sio wa kisiasa, niko bize kiaina nitachangia nikirudi
 
Mbona hakuna wachangiaji? Au kwa sababu uzi sio wa kisiasa, niko bize kiaina nitachangia nikirudi
Wana JF walio wengi wapo wanajadili mimba ya wema kama vile huyo wema ni mwanaume kwa hiyo kama wanashangaa vile iweje abebe mimba au kama haijatokea kwa binadamu wa kike kubeba mimba.
 
naunga mkono hoja kwa maana nyingine Jua ndio mwanzo wa nishati yote duniani isipokua nyuklia........ ambayo Uraniam ilifanywa wakati jua linafanyika.

Siku jua litakapokufa na huu ndio mwisho wa uhai wa kila kiunbe katika galaxy yetu
 
naunga mkono hoja kwa maana nyingine Jua ndio mwanzo wa nishati yote duniani isipokua nyuklia........ ambayo Uraniam ilifanywa wakati jua linafanyika.

Siku jua litakapokufa na huu ndio mwisho wa uhai wa kila kiunbe katika galaxy yetu
Naam,sawa kabisa jua ndio chanzo kikuu cha nishati duniani na pindi litakapoacha kuzalisha nishati yake by nuclear fussion reaction hakuna maisha yatakayo exist duniani na sio maisha tu hata sayari na magimba mengine yataachiwa na jua, kumbuka jua ndio linashikiria vitu vyote katika solor system kwa sababu ya ukubwa wa acceleration due to gravity yake ambayo ni 275N/Kg.
 
Wana JF walio wengi wapo wanajadili mimba ya wema kama vile huyo wema ni mwanaume kwa hiyo kama wanashangaa vile iweje abebe mimba au kama haijatokea kwa binadamu wa kike kubeba mimba.
Teeh! teeh! we jamaa una utani na wana JF, ngoja waje.
 
Usanisinuru(photosynthesis);ni kitendo cha kikemia na kibaiolojia ambapo mimea ya kijani(green plants) hubadili nishati ya mwanga wa jua kuwa nguvu ya kikemia inayohifadhiwa na mmea katika sukari aina ya stachi.kitendo hiki cha usanisinuru hufanywa na mimea ya kijani(green plants) kwa sababu mimea ya kijani inamiliki kiwiti(chloroplasts) zenye chembe ndogo ndogo za kijani(chlorophylls) zenye uwezo wa kuvuta na kubadili mwanga wa jua kuwa nishati ya kikemikali.Ili kitendo hiki kifanyike kinahitaji; maji,na gesi ya kaboni daioksaidi kutoka angani hivyo basi kitendo hiki pia usawazisha kiwango cha gesi hii ambayo ikizidi huwa sumu kwa mwanadamu.baada ya kitendo hiki kukamilika huzalisha; maji, sukari,na gesi ya OKSIJENI inayotufanya mimi, wewe na viumbe hai wengine tuweze kuishi kwani kila siku tunaitumia katika upumuaji na uvunjaji wa chakula mwilini (respiration) kitendo kinachotupa nguvu zinazotusaidia katika shughuli za maisha yetu ya kila siku. HAKUNA MIMEA HAKUNA MAISHA.
lengo kuu la kuvuta oxygen ni kuondoa carbondioxide mwilini
 
Usanisinuru(photosynthesis);ni kitendo cha kikemia na kibaiolojia ambapo mimea ya kijani(green plants) hubadili nishati ya mwanga wa jua kuwa nguvu ya kikemia inayohifadhiwa na mmea katika sukari aina ya stachi.kitendo hiki cha usanisinuru hufanywa na mimea ya kijani(green plants) kwa sababu mimea ya kijani inamiliki kiwiti(chloroplasts) zenye chembe ndogo ndogo za kijani(chlorophylls) zenye uwezo wa kuvuta na kubadili mwanga wa jua kuwa nishati ya kikemikali.Ili kitendo hiki kifanyike kinahitaji; maji,na gesi ya kaboni daioksaidi kutoka angani hivyo basi kitendo hiki pia usawazisha kiwango cha gesi hii ambayo ikizidi huwa sumu kwa mwanadamu.baada ya kitendo hiki kukamilika huzalisha; maji, sukari,na gesi ya OKSIJENI inayotufanya mimi, wewe na viumbe hai wengine tuweze kuishi kwani kila siku tunaitumia katika upumuaji na uvunjaji wa chakula mwilini (respiration) kitendo kinachotupa nguvu zinazotusaidia katika shughuli za maisha yetu ya kila siku. HAKUNA MIMEA HAKUNA MAISHA.

Nina mawazo tofauti na sentensi hii ''ambapo mimea ya kijani(green plants) hubadili nishati ya mwanga wa jua kuwa nguvu ya kikemia inayohifadhiwa na mmea katika sukari aina ya stachi'' ....Mimea HUTUMIA nishati ya jua kutengengeza nishati ya wanga (carbohydrates). Kwa maana nyingine nishati ya jua hutumika ''kuivisha chakula'' na kupata wanga huku ikizalisha maji na oxyen kama ulivyosema. Swali kuna mimea ambayo haina rangi ya kijani je inauwezo wa kutengeneza wanga kama mingine?
 
lengo kuu la kuvuta oxygen ni kuondoa carbondioxide mwilini
Hapana, lengo la kuvuta oxygen si kuondoa carbondioxide,lengo la oxygen in respiration ni ku act as final acceptor katika stage ya mwisho ya aerobic respiration inayojulikana kama electron transport chain au oxidative phosphorylation.

Oxygen inapokea eletron na 2 hydrogen proton kutengeneza metabolic water,hiyo hasa ndio kazi ya oxygen.
 
Hapana, lengo la kuvuta oxygen si kuondoa carbondioxide,lengo la oxygen in respiration ni ku act as final acceptor katika stage ya mwisho ya aerobic respiration inayojulikana kama electron transport chain au oxidative phosphorylation.

Oxygen inapokea eletron na 2 hydrogen proton kutengeneza metabolic water,hiyo hasa ndio kazi ya oxygen.
carbondioxide ikibak mwilini kinatokea nini?..na je bila kuvuta oxygen carbondioxide inaweza kutoka
 
Back
Top Bottom