Kijana wa Kiume wa kuuza Duka -Hardware

Kijana wa Kiume wa kuuza Duka -Hardware

Kama mshahara unaanzia milioni mbili na inalipa overtime na unatoa mapumziko siku ya week end sema nikuletee mchapakazi
 
Tatizo la jf ndio hili wakija vjana kutafuta kazi hta vbarua si vbarua wala kazi vinavyoonekana na vikija vbarua vjana ndio hawaonekani
Vijana wamesusa km kazi ajirini watoto wa Shangazi zenu kazi unatangaza ila mshahara hutangazi unataka mkalipane nini makubariano 40 kwa mwezi?
 
Ndugu Mkuu/Meneja wa Duka la Hardware,
Naandika barua hii kuomba nafasi ya kazi kama muuzaji duka la hardware, kama ilivyotangazwa. Nina umri wa miaka 24 na nimehitimu Kidato cha Nne.
Nina uelewa mzuri wa hesabu, jambo ambalo ninaamini litanisaidia sana katika majukumu ya kuuza na kutoa huduma sahihi kwa wateja. Ingawa tangazo linasema "ANAISHI MADALE, WACO, KULANGWA au maeneo jirani," niko tayari kuhamia au kusafiri kwenda eneo la kazi ili kuhakikisha ninatimiza majukumu yangu kikamilifu.
Nina shauku kubwa ya kujifunza na nina uwezo wa kufanya kazi chini ya uangalizi mdogo. Ninaamini nina sifa na ujuzi unaohitajika kwa nafasi hii.
Ninaomba fursa ya kuweza kueleza zaidi kuhusu sifa na uzoefu wangu katika mahojiano.
Asante kwa muda wako na kuzingatia ombi langu.
Kwa heshima,
Jina Daudi Daudi
[Namba yangu ya Simu -PM]
 
Muda wa kutafuta kazi ndo huwa mpo hivi ngoja muipate sasa.....
Mi nna kijana ananiboa sana kero yake kubwa ni kuchelewa chelewa kazini na akiwa na dharura hasemi, na simu hapokei ananikera mnoooo....

Ila uaminifu 99% hata nikisahau hela nitaikuta yani sio mwizi kabisa, hiki tu ndo kinafanya nivumilie ufala wake.

Nawaza naweza kumtimua nikaleta kibaka.
Muelekeze tuu my former boss alikuwa anapiga simu mpka kero ,

Ila tulivumiliana hivyo hivyo, maake yeye anapenda WhatsApp call, kidg WhatsApp call

Mm namuambia nipigie normal calls hataki,, anasema hataki normal calls, like ??
 
Biashara ya hardware, Kama mume hakai kwenye hesabu basi mke anafaa akae kwenye hesabu(pesa)

Ukikosea hapo ukamuweka mjomba,mpwa,binamu,mtu baki/jamaa...

Baada ya miezi 6 tu utaziona dalili za kurudi masihi/Yesu kwa Mara ya pili!.
 
Back
Top Bottom