Kijana wa kiume akamatwa akimfanyia mtihani mpenzi wake wa kike

Hiyo mbona ilitokea nikiwa nasoma kwenye ka chuo Fulani hapa Tanzania. Dada alikua ana supplementary (mtihani wa kutimiliza) wa QMS hivyo boyfriend wake siku ya kufanya mtihani huo wakaingia wote kila mtu akapewa booklet, yule dada akawa haandiki chochote, halafu yule kaka akawa ndio anaandika na mbaya zaidi kwenye booklet akawa amendika namba ya yule dada ambayo iko kwenye kitambulisho cha dada, hivyo msimamizi alivyoangalia kitambulisho cha dume hakina ile namba, kuangalia kitambulisho cha sister ndio chenye ile namba, na walikuwa wamekaa pamoja!!!!

Chuo kile hakina mchezo, ukishikwa unacheat kinachofuatia nikupandishwa kwenye gari ya wagonjwa ambulance hadi stendi kuu Msamvu na ndio mwisho wa Chuo!!!!
Wote wakakosa chuo kwa ajili ya "mapenzi"
 
Walisemaje sijui huko kwao kila mmoja alipofika!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…