Kijana using'ang'anie kuishi maisha ya ghali bila mipango

Kichwa Kichafu

JF-Expert Member
Apr 13, 2017
44,565
188,769
Habari!

Kuna wimbi kubwa la vijana kujaribu kuishi maisha yenye standard za juu huku maisha yao bado kabisa hayana msingi imara kuishi hivyo.

Kijana usikurupuke katika haya maisha kutokana na maisha ya wengine au msukumo wa hisia bila kufanya tafiti yako binafsi, kweli ni jambo zuri sana na jema kuishi katika standard ambazo kila siku unatamani kuishi kulingana na upambanaji wako.

Wengi wanafanikiwa kupambana na utafutaji, tatizo linakuja kwenye mipango baada ya yote(Upambanaji). Hapo ndipo imekuwa changamoto kubwa sana kwa vijana wa sasa kurukia maisha ambayo hatoweza kuishi kwa muda mrefu.

Na kama atafanikiwa kuishi hayo maisha ambayo yapo juu ya hali uliyonayo basi cashflow za IN pamoja na OUT zitabalance na hatoweza kukua zaidi ya hapo alipo kwa sasa ndani ya miaka kadhaa. Au moja kwa moja kijana akaishi kwa madeni ya muda mrefu.

Wengi wao utawakuta wakilaumu kwa sababu mbalimbali ikiwepo shughuli wanazofanya halizipi.

La hasha! Kumbe mchawi ni yeye mwenyewe kwa kuchagua maisha yenye standard za juu/ lifestyle huku hakuna miamba ya kushikilia hayo maisha aliyochagua kuishi.

Hivyo basi kijana kuwa makini sana hapo kwenye maisha unayochagua ishi fanya kulingana na ulichonacho huku ukiweza kujipanga kujenga nguzo imara za kusaidia kuishi maisha ya ndoto zako kwa kipindi kirefu bila kuyumbayumba.

Nawasilisha Mzee Mkoloni

Cc: Kichwa Kichafu
 
Mafanikio siyo kitu unachokipata kwa bahati.

Unahitaji kufanya kazi kwa bidii na kujitoa muhanga.Kila mtu anataka kufanikiwa lakini wangapi wapo Tayari kutia bidii ,Muda kujinyima na kujiandaa ili kushinda.?

Tunahitaji kujitoa sadaka na nidhamu binafsi.Hakuna mbadala wa kufanya kazi kwa bidii.

Things may come to those who wait,but only the things left by those who hustle
Abraham Lincoln
 
Hakuna cha kuzikwa nacho mkuu.

Ukiishi hivyo hutodhubutu kufanya vitu vya kudumu kisa kuna kufa.

Si kila unachokifanya ni kwa ajili ya kwako mwenyewe mengi tunafanya kwa faida ya wengine.

Maisha unayoishi sasa wewe kuna watu walijitoa kufanya hivyo mkuu.

Kuna na mawazo positive kila siku utanishukuru.
Kwani dunia ni yetu? Kuna chochote utazikwa nacho?
 
Kuwa na long term plans za kula hizo bata boss.

Tengeneza maisha ya familia yako na watu wanaokuzunguka wale bata pamoja na wewe kwa kipindi kirefu.

Kuwa mtu wa kukua kila siku usikubali kubaki pale pale ndani ya muda fulani.

Jitahidi speed ya mafanikio inakuwa kubwa kulingana na neno lako la "life is too short".
Life is too short acha tule bata tu
 
Shukrani mkuu.
Mafanikio siyo kitu unachokipata kwa bahati.

Unahitaji kufanya kazi kwa bidii na kujitoa muhanga.Kila mtu anataka kufanikiwa lakini wangapi wapo Tayari kutia bidii ,Muda kujinyima na kujiandaa ili kushinda.?

Tunahitaji kujitoa sadaka na nidhamu binafsi.Hakuna mbadala wa kufanya kazi kwa bidii.

Things may come to those who wait,but only the things left by those who hustle
Abraham Lincoln
 
Back
Top Bottom