Kijana Exaud, mbunifu anafurahisha!

Kijana Exaud, mbunifu anafurahisha!

Nakumbuka enzi nikiwa bado shule ya msingi miaka ya 1990 na 2000s mwanzoni nilitembelea Moshi Vijijini niliona sana baiskeli za mbao na kuna nyingine kama guta watu wa huko walikuwa wanaita "viparkala".

Hivi ilikuwa havina mechanism ya kuendesha bali ilitegemea zaizi penye mteremko ndio mnapanda kinaserereka. Sehemu ya mlima ni kusukuma tu hamna namna.

Matairi ya mbao kama hivyo na yamepigwa mpira ili yasipasuke na kati kati kuna plug/nondo inayofitishwa kwenye ball bearing ili tyres ziwe na mzunguko laini na waharaka.


Nakumbuka watu wa huko walivitumia kipindi hicho kwenda navyo kwenye misitu ya mlima Kilimanjaro kwaajili ya kubebea kuni au majani ya mifugo.

Huu ubunifu upo mda tu. Watu wa huko Kilimanjaro nadhani mtakuwa mashahidi.
 
Ila nikiwakumbuka Muddy Physics na Kihombo walivyokufa desperately yani hii nchi haijali wasomi. Yani Muddy physics alikuwa ndio Mohsen Fakhrizadeh wetu yule Iranian nuclear scientist Mossad walimuua.
 
Amenikumbusha utotoni nimezitengeneza sana. Ila wazazi walikuwa wanapenda ya matairi matatu kwa sababu inapakia mzigo mkubwa zaidi, hiyo ni ya starehe zaidi.
 
View attachment 1764804View attachment 1764805View attachment 1764810

Nimekutana na mtoto Exaud (ana miaka 12, darasa la 5) pale Mbalamwezi,mbele kidogo ya (Mafinga) Nyololo, njia ya Iringa -Mbeya.
Nimefurahia ubunifu wake na jinsi ambavyo Neno la Mungu limemkaa.

KILA MWENYE PUMZI AMUSIFU BWANA

Kizuri zaidi ni namba plate liyoiokota barabarani na "kusajili" pikipiki yake.
Hapo nikasimama na kumuuliza ametoka wapi, kasema ametoka mashine ya kusaga, katumwa na mama!

Hii imenikumbusha na mimi utotoni!
Hongera sana Exaud!
Naona kama ni Mbalamaziwa, njia panda ya Malangali High School, vipo vingi sana wenyewe wanaita Vibagadu
 
Iringa vinaitwa VIGELETI..kikikuangusha tegemea kulala bed mwezi 1 hayo mambao yakifumuka kwenye mseleleko .utaimba haleluya...tumeendesha mno enzi hizo
Umenikumbusha mbali Mkuu, kuna mtu kule home hiyo kitu iliwahi kung'oa nanilii za huku chini alililia balaa.
 
Back
Top Bottom