Kijana: Epuka UKIMWI ili usidharaulike

Nimepoteza kaka zangu wawili kwa ukimwi.. Hadi Leo huwa naogopa sana kuhusu huu ugonjwa.. Nakumbuka kaka yangu alivyofariki kwa huu ugonjwa mwaka 2010 nikiwa form four nililia sana. Acheni Jamani mambo ni hatari sana kuhusu huu ugonjwa.. Hapa ninapoandika Kuna kaka zangu tena wawili wanaishi na maambukizi ya ukimwi.. Tumebaki wawili tuu ambao tupo safe.. Kila nikiona habari za Ukimwi nasononeka nawakumbuka kaka zangu waliotangulia mbele za haki pia mawazo yananijia kuhusu Hawa kaka zangu wanaoishi na maambukizi ya ukimwi. Inauma sana yaani ndugu zangu acha kabisa omba yasikukute maana sisi tuliobaki ndo tumekuwa walezi wa watoto walioachwa.

Onyo.. Mungu akikujalia Hali nzuri ya maisha itumie vizuri kwa sifa na utukufu wake Usije ukamkufuru mungu. Mungu akikutelekeza utapata pigo la maisha.. Hawa ndugu zangu waliofariki walikuwa na maisha mazuri sana kipindi sisi tupo wadogo ila walikosa hekima ya kutumia Mali zao badala yake wakaendekeza anasa.. Yaani Mimi hapa nilipo naogopa kweli ukimwi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole Mkuu nyumban kwenu ni mkoa gan Mkuu,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
thread yako ni nzuri

sema tu umeiwasilisha kikanyaboya kanyaboya

halafu umekosa unyenyekevu,subira na ujasiri ktk namna bora ya kuiwasilisha

Sent using Jamii Forums mobile app
Kabisa yaani ina harufu ya stigmatism...anashindwa kujua wapo rafiki au jamaa humu humu ambao Ni waathirika wa hili,na wengine ukute wala haikua makosa yao kwa kujitakia

Lakini anasahau kuwa wengi wetu Ni waathirika japo sio kwa moja kwa moja...wapo tumepoteza wazazi,Dada na Kaka,wajomba na shangazi au namna yeyote wapendwa wetu wakiwemo marafiki kwa tatizo hili

No wonder atakwambia ana degree halafu analalamika hana kazi,Sasa huyu kwenye Jamii anakuwakilisha vipi,au ukute anahangaika kumeneji shughuli zake lakini kushindwa kukaa na Jamii inayomzunguka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah izi mada za Ukimwi mbona tunatishana kila kona ukimwi ukimwi..juz kat nmekaa zangu sina mpango wowote nmechill mara nikafungua redio flan ivi tena ilkua tune inn dah nisikutane na wimbo wa Starehe by ferooz....ukizngatia mwez ulio pita kuna njia nilipita dah iyo njia naijua mwenyewe...sjakaa sawa nyuz za ukimwi kama zote dah kuna nn jmn kinakuja?..
 
Halafu ARV zinasaidia lakini zimawafanya watu wasiogope na kuepuka.

Zamani kabla ya ARV waathirika walikuwa wanakonda sana na kupandisha makenchi mabegani,

Hali hii ikisaidia watu kumuogopa mtu na kumuepuka,

Hatari iliyopo siku hizi mwathirika wa HIV hawezi julikana kwa macho wala nywele.

Siku hizi ni wachache sana wanaokonda .

Siku hizi nywele haziwi kalikiti kama zamani.

Siku hizi wanatoka vitambi.

Wachache sana labda umuone usoni kwenye mashavu wanakuwaje sijui.

Sasa nyakati hizi ndiyo za kuwa makini sana hatari imeongezeka.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu wanawake wengi hawakatai mwanaume yeyote akijaribu kumtaka anakubaliwa hata kwa bure au pombe

Yani ni wachache wenye huruma ya kuepuka kuambukiza Wengine lakini wengi wanakuwaga na roho fulani ya kutaka wapate wengi.

Inasikitisha sana!

Mungu azidi kutuhurumia na yatuepuke na ndugu zetu na kuambizana kuepuka mara kwa mara


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo maana mimi nawauliza wanaume hivi huwa hujiulizi mara mbili tatu na kustuka unapoona mwanamke anajiletea mwenyewe kwako kirahisi?

Hushangai kwanini anavaa nguo za mitego?

Hushangai yeye anakupigia simu na kujutafuta kila wakati?

Hustuki tu?

Au ndiyo unachukulia kuwa unabahati ya kupendwa?

Yani kwamba wewe unangekewa au?

Tafakali


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwerevu akiona mwanamke anaji expose (anavaa mavazi ya mitego) anajua hapa hatari maana huenda atakuwa cha wote

Yani wewe unazani huyo mwanamke wewe ndiyo utaanza naye?!

Hujiulizi kwa wepesi huu wa kujigonga kwako ameshajigonga kwa wangapi?

Adui amepofusha macho yenu na fahamu zenu?!

Basi tumrejee Mungu kila mtu kwa Imani yako, tukatubu makosa yetu na kujitahidi kuishi kwa kushika maagizo yake hiyo itasaidia sana kuepuka uovu.

Maana imeandikwa :
“Kwa kumcha Mungu watu huepuka uovu”

Na kumcha Mungu siyo kwenda kwanisani/msikitini halafu ukirudi kwenye jamii matendo yako ni yale yale maovu!

Kumcha Mungu ni kumuogoma Mungu sana na kujitahidi kuyashika maagizo yake wakati wote na popote siku zote.

Nawatakia kheri ya Mwaka mpya 2020


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu binti wengine wamejaa tamaa kutaka simu kali , starehe, kupenda pesa, n.k

Hali hiyo imewafanya wajiingize kwenye uhusiano na mibaba yenye michanganyo ya wanawake wengiiii ikiwemo michepuko,

Kwa hiyo binti anakuwa na boyfriend wake wa chuo au mtaani wa umri wake wakati huo huo na jibaba analiita anko wake linamtafuna na kummwagia mahela

Hatari kubwa sasa hapo !

Ndiyo unakuta siku hizi hata takwimu za Tacaids wanakwambia kuanzia umri kati ya 18 sijui 24 hadi ngapi hapo ndiyo majanga wanaongoza

Mungu atuhurumie na hao wazungu waaanze kuuza dawa tu za kuponyesha jamani sijui lini?!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
UKIMWI ni upungufu wa kinga mwilini dawa yake ni kuziongeza kinga mwilini

hebu tuanze kutumia akili vijana na kufikirisha ubongo haiwezekani ukimwi uletwe na wazungu na wao hao hao wakuletee dawa

alafu watu wanaweza kupaa paka mwzini huko na kufanya mambo ya ajabu, teknolojia imekua Kwa kiasi kikubwa hivo alafu washindwe kweli kupata dawa ya ukimwi Kwa miaka zaidi ya 30 sasa

lazima kuna jambo linafichwa na haliko sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom