manuu
JF-Expert Member
- Apr 23, 2009
- 4,064
- 10,745
Ni kijana aliyetokea kwenye familia yenye uwezo kiasi, wazazi wake walijitahidi kuhakikisha mwanao anapata elimu iliyobora wakaamua kumpeleka South Africa Johannesburg mtoto alisoma huko kuanzia primary mpaka Sec School.
Akiwa form 2 kuna maandamano na vurugu yalitokea shuleni kwao yakihusisha wanafunzi wote wakipinga maswala ya chakula kuwa si kizuri.Maandamano yale yalipelekea polisi kufika shuleni pale na kuwakamata baadhi ya wanafunzi akiwa ni pamoja na huyo kijana waki Tz.
Walipofikishwa pale polisi wanafunzi wengine wazazi wao walifika pale na kuwatoa watoto wao kwa dhamana maana wengi wao walikuwa ni wazawa wa huko akabaki yule wa kitanzania.
Ilipofika usiku mtoto yule akiwa amechanganywa na wahalifu wengine.Mhalifu mmoja akamwita ili alale nae na akawa kama anamsaidia maana wahalifu wengi walikuwa wakimsakama sakama kijana yule.
Kijana yule akaamini muhalifu yule aliemwita ndiyo atakae msaidia akienda akawa amelala karibu yake.Ilipofika usiku wa manane muhalifu yule akaanza kumvua yule kijana suruali kijana akapambana nae huku akipiga kelele bila msaada wowote akavuliwa suruali na yule mhalifu akamwingilia kinyume na maumbile.Kesho yake akaenda kushtaki kwa askari lakini hata hakusikilizwa.
Ikawa mchana ikawa usiku tena yule mhalifu akamwingilia tena.Mhalifu yule ndiye alikuwa kama kiongozi kwenye chumba kile waliopo kwahiyo akawa anajifanya kumsaidia yule kijana kupata chakula kizuri na kwa wakati.
Basi kijana alikaa wiki pale na kila usiku akawa anaingiliwa hivyo hivyo bila msaada wowote.Baada ya week mama yake akawa ameshafika akitokea Tz akaruhusiwa kumdhamini mtoto wake.
Ila akaona afya ya mtoto imedhoofu sana mama yule alilia kwa uchungu mno akamchukua mwanae na kurudi nae Tz kijana yule alizidi kudhoofu afya sana.Mama akakaa na mtoto wake akamuuliza kwanini mbona huna raha una mawazo mno.Mtoto ndiyo akamwadithia mama ake kisa kilichomkuta akiwa mahabusu kule South Africa.
Mama alilia mno akamwambia baba mzazi wa mtoto baba aliumia mno.Wakampeleka hospital wakakuta ni kweli mtoto aliingiliwa na akakutwa yuko na ugonjwa wa fungus akatibiwa na akapima UKIMWI akakutwa hana.
Ila ilipofika miezi kama 4 hivi akaenda kupima tena akakutwa aliambukizwa HIV na mpaka sasa anaendelea kutumia dawa hizo, ila kijana ni mtu wa kulia tu hana raha kabisa.
Akiwa form 2 kuna maandamano na vurugu yalitokea shuleni kwao yakihusisha wanafunzi wote wakipinga maswala ya chakula kuwa si kizuri.Maandamano yale yalipelekea polisi kufika shuleni pale na kuwakamata baadhi ya wanafunzi akiwa ni pamoja na huyo kijana waki Tz.
Walipofikishwa pale polisi wanafunzi wengine wazazi wao walifika pale na kuwatoa watoto wao kwa dhamana maana wengi wao walikuwa ni wazawa wa huko akabaki yule wa kitanzania.
Ilipofika usiku mtoto yule akiwa amechanganywa na wahalifu wengine.Mhalifu mmoja akamwita ili alale nae na akawa kama anamsaidia maana wahalifu wengi walikuwa wakimsakama sakama kijana yule.
Kijana yule akaamini muhalifu yule aliemwita ndiyo atakae msaidia akienda akawa amelala karibu yake.Ilipofika usiku wa manane muhalifu yule akaanza kumvua yule kijana suruali kijana akapambana nae huku akipiga kelele bila msaada wowote akavuliwa suruali na yule mhalifu akamwingilia kinyume na maumbile.Kesho yake akaenda kushtaki kwa askari lakini hata hakusikilizwa.
Ikawa mchana ikawa usiku tena yule mhalifu akamwingilia tena.Mhalifu yule ndiye alikuwa kama kiongozi kwenye chumba kile waliopo kwahiyo akawa anajifanya kumsaidia yule kijana kupata chakula kizuri na kwa wakati.
Basi kijana alikaa wiki pale na kila usiku akawa anaingiliwa hivyo hivyo bila msaada wowote.Baada ya week mama yake akawa ameshafika akitokea Tz akaruhusiwa kumdhamini mtoto wake.
Ila akaona afya ya mtoto imedhoofu sana mama yule alilia kwa uchungu mno akamchukua mwanae na kurudi nae Tz kijana yule alizidi kudhoofu afya sana.Mama akakaa na mtoto wake akamuuliza kwanini mbona huna raha una mawazo mno.Mtoto ndiyo akamwadithia mama ake kisa kilichomkuta akiwa mahabusu kule South Africa.
Mama alilia mno akamwambia baba mzazi wa mtoto baba aliumia mno.Wakampeleka hospital wakakuta ni kweli mtoto aliingiliwa na akakutwa yuko na ugonjwa wa fungus akatibiwa na akapima UKIMWI akakutwa hana.
Ila ilipofika miezi kama 4 hivi akaenda kupima tena akakutwa aliambukizwa HIV na mpaka sasa anaendelea kutumia dawa hizo, ila kijana ni mtu wa kulia tu hana raha kabisa.