Kiini macho cha Kamati ya January Makamba na Dowans

Kiini macho cha Kamati ya January Makamba na Dowans

HAYO YALITABILIWA. UKIONA WANA UFALME WAAPIGANA WAO KWA WAO, UJUE HUO NDIO MWISHO WA UFALME HUO. J. MAKAMBA NI MMOJA WAO, KATIBU MKUU CCM NI BABA YAKE. WAKITOFAUTIANA NDIO MWISHO. I want to witness their sad demise.
 
Hoja zote nzuri lakini mwisho wake vichekesho tu. Hoja kama hizo hizo zilishaibuliwa bungeni lakini zinavyozimwa haingii hakilini.

Shida za kila aina na umaskini uliokithiri ndio utawafanya wawe 'solution oriented' for any issue that arises in all aspect of life otherwise I do not see any concrete actions on those probs.
 
kuna kampuni nyingine imekodisha mitambo serikali, mitambo ikaletwa, ikafanyiwa test run, halafu ikazimwa......haijatumika tena mpaka leo, na kila mwezi serikali inalipa renting fees.....zimefikia zaidi ya $20,000,000
 
Mtoto wa paka anacheza na mawindo yaliyoletwa na mama..!!
 
Hiii ni michezo yao ya Kuigiza.....na kama nimemwelewa hivi sasa hawa mafisadi wanateswa sana na suala la wananchi kupoteza imani na ki-corrupt Govt chao......thatswhy wengine wanajifanya wanakuja na rangi za kutaka kutetea wananchi ilhali kila kitu kipo wazi.....Watu pekee nisio watilia shaka kutoka katika kile chama cha kifisadi katika sakata hili kwamba wapo pamoja na wananchi ni....Sitta na Kidogo Mwakyembe...
 
Aache upuuzi wake.
Yeye si alikuwa ikulu, inamaana hakuwahi hata kusikia hiyo dili wakati inapita? Kwa nini hakushauri wakati huo? Anaona hali imebadilika sasa hivi ndo anatafuta sapoti ya umma kama walivyofanya uvccm. Wanatakiwa washauri kabla sio kusubiri watu waanzishe ishu ndo wao wadandie.
 
what makes it being crap?
Unataka mpaka cdm wakisema ndio manakubali?
Tunapingana kwa hoja sio chuki binafisi zisizoweza kujenga nchi yetu


anajigonga tu,,,,,hana jipya....kama kweli yeye ni safi angekataa ubunge aliyopewa na baba yake.
 
1.Ukifuata mambo ya wanasiasa wakati mwingine Nchi inaweza isifike Mbali.

2.Huyu dogo alikuwa karibu na Rais wakati madudu yote yanatokea ,Je alichukua hatua gani ya kukemea wakati yeye yupo pale State house...alimshauri nini Rais

3.Hili suala kama anaona lina umuhimu sana na yeye haogopi mtu alipeleke bungeni..

4.Haya mbiyo za 2015
 
me nashauri angeenda bungeni akaomba awasilishe hoja binafsi (ingawa na doubt kama angepata nafasi mana kesi ipo mahakamani), ila ni hoja nzuri na ya kizalendo kbs
 
katumwa huyu wameanza kugeukana wao kwa wao, Bado Chenge na AG nao watatoa yao, si unaona Mkuu JK ameshatoa yake EI haijui DOWANS imeanzisha na nani, hivi pale ikulu hakuna mtu anyejua kujibu hoja muhimu kwa kumweleza mkuu wetu kuwa atawashagaza sana wananchi akisema kuwa hawajui wamiliki wake, hivyo anadhalilisha UWT kwa kuwa hawako makini hata nchi yaweza uzwa bila kujua
 
haya yote maigizo tu baada ya kuona wamewekwa uchi,anafanya hivyo ili ionekane ccm wanachukia ufisadi na kuwajali wananchi but in reality sio,..na yeye atuambie dili ya malaria aliyompora sugu,..like father like son,...is this a fuc*in dynasty?
 

Mhh ndugu yangu hii nayo ikiwa crap basi hoja nzuri zitakuwa hazipo. Bila kujali lengo la mtoa hoja (january makamba) nikiri tu kwamba kijana ameiweka vizuri sana hoja yake na ninaamini kwamba majibu ya waziri yatatufungua macho na masikio kuhusu mwendelezo wa ahadi nyingi hewa za CCM lakini pia zitatupa kitu kizuri cha kukitumia come 2015 kwenye uchaguzi.

CCM inaweza kuwa inajikaanga yenyewe kwa mafuta yake,na amini nawaambieni January Makamba ni kijana mdogo na ana miaka mingi mbele yake mungu akimpa uzima ya kufanya politics hawezi kufurahia kuharibu career yake in favour ya wazee wa CCM ambao maisha yao ya siasa yako ukingoni na most of them hata mwaka 2015 hawatakuwepo kwenye political arena (kwenye active politics) ama kwasababu ya uzee au sababu nyingine zozote.
 
Anaendeleza mbio zake za kugombea u-prezidaa come 2015
 
Hivi huyu January si alikuwa karibu na Kikwete wakati haya yote yanatokea sasa kwanini hakumshauri, halafu hivi Ngeleja amegeuka ghafla bubu mbona simsikii au kazi aliyotumwa ameishaimaliza
 
Back
Top Bottom