Kigwangalla usipotoshe kuhusu Katibu Mkuu Dkt. Mashinji

Tumaini Makene

JF-Expert Member
Jan 6, 2012
2,642
6,070
Tunamshukuru Dkt. Hamis Kingwangalla kwa kutoa maoni yake akikiri ukweli kuhusu Katibu Mkuu wa Chama, Dkt. Vincent Mashinji kuwa ni mwanasiasa mzuri, msomi mzuri na msemaji mzuri.

Hapo hapo kwa makusudi ya kutumwa au kujituma mwenyewe, katika maoni yake hayo ambayo ameandika na kuyasambaza mitandaoni, Kingwangalla amefanya upotoshaji kwa nia anayoijua yeye.

Kingwangalla ambaye ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, amedai kuwa Katibu Mkuu Mashinji hakuwahi kuwaokoa yeye na watu wengine walioshiriki mgomo wa madaktari mwaka 2005 wala hakuwahi kuongoza mgomo huo, lakini hapo hapo anajikanganya kwa kukiri kuwa Katibu Mkuu ALISHIRIKI mgomo huo huo.

Ili asilazimike kujikanganya kwa sababu tu ametumwa au amejituma kupotosha, Kingwangalla awaambie Watanzania ni akina nani waliowaokoa interns (akiwemo yeye Kingwangalla) waliogoma mwaka huo mwezi Februari?

Kumbukumbu zinaonesha kuwa baada ya interns hao kugoma ilikuwa imeamriwa wafukuzwe na wanyang’anywe leseni, hivyo seniors wao kama akina Erasto Ngonyani, Dkt. Mashinji na wengine, nao wakaamua kugoma ili kuwaokoa interns wasifukuzwe.

Kingwangalla kwa namna ile ile ya kujituma au kutumwa kupotosha, ameandika kuwa Katibu Mkuu Dkt. Mashinji alinyanyaswa na supervisor wake (ambaye hamtaji jina, Prof. Mwafongo).

Kama Naibu Waziri haujui ukweli kuhusu Dkt. Mashinji na supervisor wake, asikimbilie kuandika kitu asichokijua na kujishushia hadhi.

Tumsaidie. Wala asiende mbali. Amtafute Katibu Mkuu wa Wizara yake, atamsaidia kupata ukweli ili siku nyingine aandike kwa usahihi. Kama hataweza kumfuata Katibu Mkuu wa Wizara yake, basi tunamsaidia kumwambia kuwa taarifa zinaonesha wawili hao (mwanafunzi na msimamizi wake) ni watu wenye mahusiano mazuri wala hakukuwahi kuwa na tukio kama alivyopotosha Kigwangalla.

Kuhusu msimamo usiotetereka, Kingwangalla kajikanganya zaidi. Siku nyingine akiamua kujituma au akikubali kutumwa kupotosha mambo ni vyema afikirie mara mbili au awe na kumbukumbu sahihi.

Madaktari waliogoma mwaka 2005 pamoja na masuala mengine, walitaka upatikanaji wa vifaa hospitalini na maslahi ya madaktari. Mambo ambayo hadi leo miaka 11 baadae bado ni kilio kikubwa katika sekta hiyo nyeti kwa maendeleo ya jamii.

Anasema eti walimtenga na kumwepuka kumwalika katika vikao vya CC ya migomo. Vyema. Kwa ujasiri huo anaojivika wa kusema anayotaka kuwaaminisha watu kuwa ni kweli, Je Kigwangalla yuko tayari kuwaambia Watanzania, ni nani aliyekwenda kumbembeleza na kumpigia magoti Waziri Mkuu Fredrick Sumaye, aki-surrender?

Kama atashindwa, basi asiogope pale atakaposaidiwa kwa kupewa picha ili amuone huyo mtu akiwa amepiga magoti ya kujisalimisha.

Kigwangalla leo yuko anafanya kazi ndani ya Serikali ya CCM ambayo mwaka 2005 aliigomea kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake, Dkt. Mashinji bado yuko upande wa mabadiliko akiendeleza kudai haki hizo na nyingine kwa ajili ya wananchi.

Hadi hapo nani mwenye msimamo, kuyumba au kutetereka, Dkt. Mashinji au Kigwangalla? Ni Dkt. Mashinji au yule aliyekwenda kupiga magoti?

Tumshauri tena Kigwangalla, kama daktari wa binadamu kwa taaluma aheshimu taaluma yake. Pia ajikite katika majukumu aliyopewa. Bado kuna ‘vilio vingi’ katika wizara yake, ambavyo haviwezi kumalizwa kwa staili ya kutumbua majipu bali uongozi wenye dira na maono (MABADILIKO). Lakini pia aheshimu kaka na dada zake waliomtangulia katika taaluma hiyo, ambalo ni jambo zuri tu.

Makene
 
Ingawa Kwangu mimi suala la kuwa ni nani aliongoza migomo sioni kama priority lakini,

Mhe.Hamis Kigwangallah (Nassoro Bagale-Jina lake la awali) anatafuta Ligi isiyo na maana tu.

Nimesoma kejeli za naibu huyu waziri wa Afya dhidi ya Katibu Mkuu Mpya wa CHADEMA Dr.Mashinji

Ni jambo la ajabu kuwa Kigwangallah anajinasibu kuongoza migomo ya wanafunzi na pia kupigania maslahi ya madaktari kwa uaminifu zaidi akiwa mwanafunzi badala ya kutuambia kuwa baada ya siku zaidi ya 100 madarakani kama naibu waziri mwenye dhamana amefanya nini kutatua kero katika tasnia ya Afya ikiwa ni pamoja na kutetea maslahi ya madaktari

Inashangaza mtu mwenye tuhuma za kunyakua jina la mtu mwingine baada ya kufeli la saba anakejeli taaluma ya mtu ngazi ya shahada ya Uzamili(Masters)

Hajawahi kujibu kwa ufasaha tuhuma hizi alizoporomoshewa na Mwananzega Mwenzake Hussein Bashe ambaye pia ni Kada wa CCM

Gonga hapo .

www.jamiiforums.com/threads/bashe-kigwangalla-vita-kali-nzega-bashe-amsasambua-mh-kigwangalla.144127/

Ben Saanane
 
Anakazi kubwa ya kuhakikisha hospital/zahanati zinajengwa kila kijiji tanzania (ahadi ya rais).

Hizi zinaitwa SECURITY WORK, kazi ambazo haziongezi chochote kwenye majukumu yako makubwa uliyopangiwa.

kwa cheo chake, hizo kazi kuna jamaa wengi tu rumumba wanalipwa na zipo kwenye job discription zao sio NW. Wewe unapoteza Attention yako Kwa majukumu yako Bure.
 
Siasa za Tanzania bana!

Watu wazima na akili zao za mashaka eti wanabishana nani aliongoza mgomo!

Hivi ni vichekesho!

Silly politicians and silly politics.

Haishangazi Tanzania iko katika hali hii ya kisiasa na kiuchumi.

Waziri na Katibu Mkuu wa chama kikuu cha upinzani hizi ndizo priorities zao!

Mbaya zaidi, wapambe wao wanashangilia!

Nani aliyeturoga?
 
Ndio shida ya kurusha mawe ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo ,hivi hawa wanasiasa vichwa vyao ni kama panzi ?? Haviwezi kutunza kumbukumbu ?Kigwangalla si yupo humu ?? Njoo huku sio unakimbilia Facebook au Instagram kutoa tuhuma zako
 
Tunamshukuru Dkt. Hamis Kingwangalla kwa kutoa maoni yake akikiri ukweli kuhusu Katibu Mkuu wa Chama, Dkt. Vincent Mashinji kuwa ni mwanasiasa mzuri, msomi mzuri na msemaji mzuri.

Hapo hapo kwa makusudi ya kutumwa au kujituma mwenyewe, katika maoni yake hayo ambayo ameandika na kuyasambaza mitandaoni, Kingwangalla amefanya upotoshaji kwa nia anayoijua yeye.

Kingwangalla ambaye ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, amedai kuwa Katibu Mkuu Mashinji hakuwahi kuwaokoa yeye na watu wengine walioshiriki mgomo wa madaktari mwaka 2005 wala hakuwahi kuongoza mgomo huo, lakini hapo hapo anajikanganya kwa kukiri kuwa Katibu Mkuu ALISHIRIKI mgomo huo huo.

Ili asilazimike kujikanganya kwa sababu tu ametumwa au amejituma kupotosha, Kingwangalla awaambie Watanzania ni akina nani waliowaokoa interns (akiwemo yeye Kingwangalla) waliogoma mwaka huo mwezi Februari?

Kumbukumbu zinaonesha kuwa baada ya interns hao kugoma ilikuwa imeamriwa wafukuzwe na wanyang’anywe leseni, hivyo seniors wao kama akina Erasto Ngonyani, Dkt. Mashinji na wengine, nao wakaamua kugoma ili kuwaokoa interns wasifukuzwe.

Kingwangalla kwa namna ile ile ya kujituma au kutumwa kupotosha, ameandika kuwa Katibu Mkuu Dkt. Mashinji alinyanyaswa na supervisor wake (ambaye hamtaji jina, Prof. Mwafongo).

Kama Naibu Waziri haujui ukweli kuhusu Dkt. Mashinji na supervisor wake, asikimbilie kuandika kitu asichokijua na kujishushia hadhi.

Tumsaidie. Wala asiende mbali. Amtafute Katibu Mkuu wa Wizara yake, atamsaidia kupata ukweli ili siku nyingine aandike kwa usahihi. Kama hataweza kumfuata Katibu Mkuu wa Wizara yake, basi tunamsaidia kumwambia kuwa taarifa zinaonesha wawili hao (mwanafunzi na msimamizi wake) ni watu wenye mahusiano mazuri wala hakukuwahi kuwa na tukio kama alivyopotosha Kigwangalla.

Kuhusu msimamo usiotetereka, Kingwangalla kajikanganya zaidi. Siku nyingine akiamua kujituma au akikubali kutumwa kupotosha mambo ni vyema afikirie mara mbili au awe na kumbukumbu sahihi.

Madaktari waliogoma mwaka 2005 pamoja na masuala mengine, walitaka upatikanaji wa vifaa hospitalini na maslahi ya madaktari. Mambo ambayo hadi leo miaka 11 baadae bado ni kilio kikubwa katika sekta hiyo nyeti kwa maendeleo ya jamii.

Anasema eti walimtenga na kumwepuka kumwalika katika vikao vya CC ya migomo. Vyema. Kwa ujasiri huo anaojivika wa kusema anayotaka kuwaaminisha watu kuwa ni kweli, Je Kigwangalla yuko tayari kuwaambia Watanzania, ni nani aliyekwenda kumbembeleza na kumpigia magoti Waziri Mkuu Fredrick Sumaye, aki-surrender?

Kama atashindwa, basi asiogope pale atakaposaidiwa kwa kupewa picha ili amuone huyo mtu akiwa amepiga magoti ya kujisalimisha.

Kigwangalla leo yuko anafanya kazi ndani ya Serikali ya CCM ambayo mwaka 2005 aliigomea kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake, Dkt. Mashinji bado yuko upande wa mabadiliko akiendeleza kudai haki hizo na nyingine kwa ajili ya wananchi.

Hadi hapo nani mwenye msimamo, kuyumba au kutetereka, Dkt. Mashinji au Kigwangalla? Ni Dkt. Mashinji au yule aliyekwenda kupiga magoti?

Tumshauri tena Kigwangalla, kama daktari wa binadamu kwa taaluma aheshimu taaluma yake. Pia ajikite katika majukumu aliyopewa. Bado kuna ‘vilio vingi’ katika wizara yake, ambavyo haviwezi kumalizwa kwa staili ya kutumbua majipu bali uongozi wenye dira na maono (MABADILIKO). Lakini pia aheshimu kaka na dada zake waliomtangulia katika taaluma hiyo, ambalo ni jambo zuri tu.

Makene
Kamanda Makene kwetu sisi wenye akili tumemdharau sana na siyo kwa hilo tu bali ni kwa kila analotenda kwa kujikomba kwa watawala,kigwangala hana tofauti na ndumilakuwili
 
Tunamshukuru Dkt. Hamis Kingwangalla kwa kutoa maoni yake akikiri ukweli kuhusu Katibu Mkuu wa Chama, Dkt. Vincent Mashinji kuwa ni mwanasiasa mzuri, msomi mzuri na msemaji mzuri.

Hapo hapo kwa makusudi ya kutumwa au kujituma mwenyewe, katika maoni yake hayo ambayo ameandika na kuyasambaza mitandaoni, Kingwangalla amefanya upotoshaji kwa nia anayoijua yeye.

Kingwangalla ambaye ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, amedai kuwa Katibu Mkuu Mashinji hakuwahi kuwaokoa yeye na watu wengine walioshiriki mgomo wa madaktari mwaka 2005 wala hakuwahi kuongoza mgomo huo, lakini hapo hapo anajikanganya kwa kukiri kuwa Katibu Mkuu ALISHIRIKI mgomo huo huo.

Ili asilazimike kujikanganya kwa sababu tu ametumwa au amejituma kupotosha, Kingwangalla awaambie Watanzania ni akina nani waliowaokoa interns (akiwemo yeye Kingwangalla) waliogoma mwaka huo mwezi Februari?

Kumbukumbu zinaonesha kuwa baada ya interns hao kugoma ilikuwa imeamriwa wafukuzwe na wanyang’anywe leseni, hivyo seniors wao kama akina Erasto Ngonyani, Dkt. Mashinji na wengine, nao wakaamua kugoma ili kuwaokoa interns wasifukuzwe.

Kingwangalla kwa namna ile ile ya kujituma au kutumwa kupotosha, ameandika kuwa Katibu Mkuu Dkt. Mashinji alinyanyaswa na supervisor wake (ambaye hamtaji jina, Prof. Mwafongo).

Kama Naibu Waziri haujui ukweli kuhusu Dkt. Mashinji na supervisor wake, asikimbilie kuandika kitu asichokijua na kujishushia hadhi.

Tumsaidie. Wala asiende mbali. Amtafute Katibu Mkuu wa Wizara yake, atamsaidia kupata ukweli ili siku nyingine aandike kwa usahihi. Kama hataweza kumfuata Katibu Mkuu wa Wizara yake, basi tunamsaidia kumwambia kuwa taarifa zinaonesha wawili hao (mwanafunzi na msimamizi wake) ni watu wenye mahusiano mazuri wala hakukuwahi kuwa na tukio kama alivyopotosha Kigwangalla.

Kuhusu msimamo usiotetereka, Kingwangalla kajikanganya zaidi. Siku nyingine akiamua kujituma au akikubali kutumwa kupotosha mambo ni vyema afikirie mara mbili au awe na kumbukumbu sahihi.

Madaktari waliogoma mwaka 2005 pamoja na masuala mengine, walitaka upatikanaji wa vifaa hospitalini na maslahi ya madaktari. Mambo ambayo hadi leo miaka 11 baadae bado ni kilio kikubwa katika sekta hiyo nyeti kwa maendeleo ya jamii.

Anasema eti walimtenga na kumwepuka kumwalika katika vikao vya CC ya migomo. Vyema. Kwa ujasiri huo anaojivika wa kusema anayotaka kuwaaminisha watu kuwa ni kweli, Je Kigwangalla yuko tayari kuwaambia Watanzania, ni nani aliyekwenda kumbembeleza na kumpigia magoti Waziri Mkuu Fredrick Sumaye, aki-surrender?

Kama atashindwa, basi asiogope pale atakaposaidiwa kwa kupewa picha ili amuone huyo mtu akiwa amepiga magoti ya kujisalimisha.

Kigwangalla leo yuko anafanya kazi ndani ya Serikali ya CCM ambayo mwaka 2005 aliigomea kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake, Dkt. Mashinji bado yuko upande wa mabadiliko akiendeleza kudai haki hizo na nyingine kwa ajili ya wananchi.

Hadi hapo nani mwenye msimamo, kuyumba au kutetereka, Dkt. Mashinji au Kigwangalla? Ni Dkt. Mashinji au yule aliyekwenda kupiga magoti?

Tumshauri tena Kigwangalla, kama daktari wa binadamu kwa taaluma aheshimu taaluma yake. Pia ajikite katika majukumu aliyopewa. Bado kuna ‘vilio vingi’ katika wizara yake, ambavyo haviwezi kumalizwa kwa staili ya kutumbua majipu bali uongozi wenye dira na maono (MABADILIKO). Lakini pia aheshimu kaka na dada zake waliomtangulia katika taaluma hiyo, ambalo ni jambo zuri tu.

Makene
Kijana tupe usahihi ili angalau tukuamini la sivyo ni porojo tu; Je Vicent alimaliza masters Muhimbili?...Je Vicent ana PhD kutoka OUT mwaka 2016 kama ulivyotoa wasifu wake?...nimekuuliza maswali "objective"..mengine yote ni "subjective issues" ambayo ni ngumu kuthibitisha tukaridhika likiwamo la migomo sababu tujuavyo UDSM baada ya mgomo wanafunzi hulazimishwa kuandika jinsi walivyoshiriki na kuomba msamaha na hakuwahi kutokea aliyekiri kwa barua "objectively"....,ukiweza kujibu maswali hayo pasipo shaka tutadadavuwa uthibitisho kutoka vyuo husika ili kuwa na "credible" SG!
 
Siasa za Tanzania bana!

Watu wazima na akili zao za mashaka eti wanabishana nani aliongoza mgomo!

Hivi ni vichekesho!

Silly politicians and silly politics.

Haishangazi Tanzania iko katika hali hii ya kisiasa na kiuchumi.

Waziri na Katibu Mkuu wa chama kikuu cha upinzani hizi ndizo priorities zao.

Mbaya zaidi, wapambe wao wanashangilia!

Nani aliyeturoga?
Huwezi kumchanganya Katibu mkuu wa chama kwani hujaona popote alipo andika kuhusu hilo, muulize huyo naibu waziri jee hizo ndio priorities za kazi yake?
 
Siasa za Tanzania bana!

Watu wazima na akili zao za mashaka eti wanabishana nani aliongoza mgomo!

Hivi ni vichekesho!

Silly politicians and silly politics.

Haishangazi Tanzania iko katika hali hii ya kisiasa na kiuchumi.

Waziri na Katibu Mkuu wa chama kikuu cha upinzani hizi ndizo priorities zao.

Mbaya zaidi, wapambe wao wanashangilia!

Nani aliyeturoga?


Achana na fikra za kurogana.Fikra za kishirikina hizi hazina nafasi karne hii.

Unaweza kuonesha mahali alipoandika Katibu Mkuu wa Chama cha Upinzani?
 
Mh. Naibu Waziri wa Afya Dr Kingwangalla hayo ndo majukumu uliyopangiwa na mh.Rais? Hii nchi ni ya ajabu haijapata kutokea duniani.
 
Akili ya Kigwa haitofautiani na akili ya Jah People mbunge wa Ccm Makambako.
Kigwangala bila hata chembe ya aibu, wakati wa mdahalo ulio andaliwa na TWAWEZA kuelekea uchaguzi mkuu 2015 liliulizwa swali la kwanini bado kuna wagonjwa wanalala sakafuni MUHIMBILI. Mbele ya Tv Kigwangala alikana kwamba hakuna wagonjwa wanao lala sakafuni MUHIMBILI. Huyu mtu siyo wa kumuamini hata kidog.
 
Katika="Mmawiaambaothawajahi69, member: 165175"]Wewe u ajuMakene ajibu maswalia uchumia tumbo?[/QUOTE]
Katika vijana ambao hawajahi kuwa na hoja ni wewe mwambie Makene ajibu maswali yangu;
1.Je Vincent alimaliza masters Muhimbili?
2.Je ana PhD OUT 2016 tarehe ngapi?;...akijibu haya maswali ntakutumia bandle!
 
Back
Top Bottom