idoyo
JF-Expert Member
- Jan 13, 2013
- 3,051
- 1,423
HKigwangalla ameteuliwa kuwa naibu waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kipinidi cha 2015-2020. Rais JPM ametumia muda mrefu akichakata kile kilichoitwa na wafia chama kuwa ni 'mawaziri bora'. Tayari watanzania wamesahau kauli na majibu aliyotoa Mh. HKigwangalla juu ya wagonjwa kusongamana kwenye hospitali za umma, wakati wa mdahalo juu ya sera za vyama kwenye elimu na afya (MKIKIMKIKI). Alisema hizo ni kauli za kisiasa, na hakuna shida kama hiyo kwenye hospitali. Jibu hili lilikasirisha sana hadhira. Leo ni waziri katika sekta ambayo haamini kama kuna matatizo yanayosemwa na jamii.
Au la, HKigwangalla ukuje hapa na useme majibu yako yalikuwa ya kisiasa kutetea chama chako wakati ule hali ilipokuwa mbaya!
Dk Kigwangala apata wakati mgumu kuitetea CCM - Kitaifa | Mwananchi
Au la, HKigwangalla ukuje hapa na useme majibu yako yalikuwa ya kisiasa kutetea chama chako wakati ule hali ilipokuwa mbaya!
Dk Kigwangala apata wakati mgumu kuitetea CCM - Kitaifa | Mwananchi
Last edited by a moderator: