VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Kigogo mmoja wa CCM ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM amesema kuwa mtangaza nia Edward Lowassa anapiga kampeni badala ya kutafuta wadhamini. Mjumbe huyo wa CC amenidokeza kuwa jambo hilo litamkwamisha vya kutosha Lowassa katika kujaribu kupenya katika mchujo wa kuelekea kupigiwa kura na Mkutano Mkuu.
"Unajua ndugu yangu, Lowassa anajiharibia mwenyewe. Kitendo cha kuandaa watu kwa maelfu na kuzungumza nao ni kampeni na si kutafuta wadhamini. Watu wanadai kuwa Lowassa anakusanya umati ili 'kuitisha' CC kuwa yeye anakubalika zaidi na hivyo hazuiliki kupitishwa kuwa mgombea wa CCM. Anaitisha CC? Really?" alisema Mumbe huyo wa CC huku akicheka.
"Wakati mwingine mbwembwe huponza. Wanatakiwa wadhamini 450 kila mkoa katika mikoa 15,kati ya hiyo 3 iwe ya Zanzibar. Hiyo niyo kanuni. Sasa watu 20,000 mkoa mmoja nwa kazi gani? Huku ni kupoteza muda na rasilimali. Sitta na Dr. Bilal ni mifano mizuri, wametafuta wadhamini na kukamilisha bila maonesho yasiyo na msingi. Mambo kama ya Lowassa asubiri wakati wa kampeni akipitishwa kugombea,si sasa" aliongeza kigogo huyo ambaye hakutangaza nia.
Mzee Tupatupa wa Lumumba Dar es Salaam
"Unajua ndugu yangu, Lowassa anajiharibia mwenyewe. Kitendo cha kuandaa watu kwa maelfu na kuzungumza nao ni kampeni na si kutafuta wadhamini. Watu wanadai kuwa Lowassa anakusanya umati ili 'kuitisha' CC kuwa yeye anakubalika zaidi na hivyo hazuiliki kupitishwa kuwa mgombea wa CCM. Anaitisha CC? Really?" alisema Mumbe huyo wa CC huku akicheka.
"Wakati mwingine mbwembwe huponza. Wanatakiwa wadhamini 450 kila mkoa katika mikoa 15,kati ya hiyo 3 iwe ya Zanzibar. Hiyo niyo kanuni. Sasa watu 20,000 mkoa mmoja nwa kazi gani? Huku ni kupoteza muda na rasilimali. Sitta na Dr. Bilal ni mifano mizuri, wametafuta wadhamini na kukamilisha bila maonesho yasiyo na msingi. Mambo kama ya Lowassa asubiri wakati wa kampeni akipitishwa kugombea,si sasa" aliongeza kigogo huyo ambaye hakutangaza nia.
Mzee Tupatupa wa Lumumba Dar es Salaam