Kigogo wa Barrick aikaanga kampuni ya ACACIA

Kigogo wa Barrick aikaanga kampuni ya ACACIA

mawazomgala

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2014
Posts
342
Reaction score
212
profesa-696x406.jpg

Ni Profesa John Thornton aliyekuja nchini kuonana na Rais JPM wakati wa sakata la makinikia.

Athibitisha msimamo wa tume ya makinikia kuwa ACACIA imekuwa na tabia ya kukwepa kodi Tanzania.

Asikitika kampuni hiyo kusababisha kuharibika kwa mahusiano ya kibiashara na serikali.

NA Mwandishi maalum
MWENYEKITI Mtendaji wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation, Profesa John Thornton, amesema kampuni yao ya Acacia Mining inayofanya kazi Tanzania, haijawahi kulipa kodi ya mapato (Coporate Income Tax) kwa serikali ya Tanzania kutokana na shughuli za uchimbaji wa dhahabu nchini suala ambalo limeathiri uhusiano baina ya kampuni hiyo na serikali.
Kauli hiyo ya Prof. Thornton inaleta matumaini kwa serikali ya Tanzania katika majadiliano yanayoendelea baina yake na Barrick juu ya tozo na kodi ambazo wanatakiwa kuilipa serikali kutokana na usafirishaji wa makinikia kwa miaka 19 tangu Acacia kuanza shughuli zake za uchimbaji nchini.
Tayari kampuni ya Barrick imeshakubali kulipa Tanzania dola milioni 300 kama utayari wa kushirikiana wakati majadiliano yakiendelea baina ya pande hizo.
Kwa mwaka mmoja na nusu sasa serikali imezuia usafirishaji wa makinikia (gold concentrate) nje ya nchi suala ambalo limeathiri utendaji kazi wa kampuni ya Acacia nchini kwa kiasi kikubwa pamoja na kusababisha kuporomoka kwa hisa zake katika soko la hisa la London.
Akizungumza katika mahojiano na The Globe and Mail mwanzoni mwa mwezi Septemba mwaka huu alisema Migodi ya Barrick inayomilikiwa na Acacia kwa asilimia 64 nchini Tanzania “hajalipa kodi ya mapato kwa Tanzania” zaidi ya kulipa mirabaha na kodi za mishahara tu.

Hata hivyo si Barrick wala Thornton ambao wamekanusha kuhusu ukweli wa kauli hiyo zaidi ya Barrick kujaribu kufafanua kuwa wanafikiri kuwa Mwenyekiti huyo alitia chumvi wakati akimaanisha kuwa kiasi kilicholipwa kwa serikali ya Tanzania ni kidogo sana ikilinganishwa na mapato ya Acacia katika shughuli za uchimbaji dhahabu nchini.
Kauli hiyo imeleta mgongano baina ya Barrick na Acacia baada ya Acacia kuipinga na kusema wanashangazwa na taarifa hiyo isiyo sahihi ya Thornton.
Kwa mujibu wa Globe, Acacia ikiwa imetolewa kwenye mazungumzo kati ya serikali ya Tanzania na Barrick, mafaili kwaajili ya kuunda mkataba mpya yamekabidhiwa kwa Kevin Thomson ambaye Mtendaji Mwandamizi wa Mikakati wa Barrick.
Kampuni ya Acacia iliingia katika kashfa ya usafirishaji wa makinikia na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni ya fedha kwa mujibu wa tume ya uchunguzi iliyoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza ukweli wa kiasi na thamani ya madini yaliyopo katika makontena ya makinikia yaliyozuiliwa.
Kamati hiyo ilibaini kuwepo kwa viwango vingi vya juu vya dhahabu ndani ya makinikia yaliyofanyiwa uchunguzi. Viwango hivyo ni kati ya 671 g/t hadi 2375 g/t, sawa na wastani wa 1400 g/t.
“Wastani huo ni sawa na 28 kg za dhababu kwenye kontena moja lenye tani 20 za makinikia. Hivyo, kwenye makontena 277 ya makinikia yaliyozuiliwa Bandari ya Dar es Salaam na Bandari Kavu yatakuwa na wastani wa tani 7.8 za dhahabu yenye thamani ya TZS bilioni 676 (USD 307,292,720),” ilisema taarifa hiyo iliyotolewa Mei mwaka jana na kuongeza;
“Aidha, kwa kutumia kiwango cha juu kilichopimwa kwenye kontena moja lenye shehena ya tani 20 za makinikia (47.5 kg), kiasi cha dhahabu katika makontena 277 kitakuwa 13,157.5 kg ambazo thamani yake ni Sh trilioni 1.146 (USD 521,300,150).
“Hivyo, thamani ya dhahabu katika makontena 277 yaliyozuiliwa bandarini ni kati ya TZS bilioni 676 na bilioni 1,147.”
Kutokana na taarifa hiyo ya Kamati ya Mkinikia, Prof. Thornton alikutana na Rais Magufuli Juni 14 2017 na kufanya mazungumzo ambapo aliahidi kuwa Barrick ipo tayari kufanya majadiliano na serikali ili kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na kuendesha shughuli zake hapa nchini.
Julai 31 2017 majadiliano baina ya pande hizo mbili yalianza huku upande wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi na baadae Barrick ikakubali kuilipa Tanzania Dola za Marekani Milioni 300 sawa na Sh bilioni 600.
Hatua hiyo ilifikiwa Oktoba mwaka jana wakati kamati mbili za majadiliano ile ya Tanzania na ya Barrick zilipokuwa zikiwasilisha ripoti ya mazungumzo yao kwa Rais Magufuli ambapo ikiwa ni mara yake ya pili kukutana na Rais Prof. Thornton alitoa salamu za shukrani na kusema kampuni yao italipa kiasi cha dola za Marekani milioni 300 kama njia ya kuonesha utayari wake na uaminifu kwa Serikali ya Tanzania.
Thornton alisema licha ya kuwa kwa sehemu kubwa wameafikiana masuala mengi, lakini suala ya tozo ya malimbikizo ya kodi bado hawajakubaliana kikamilifu na kwamba wameliweka kiporo wakati akiwasiliana na wanahisa wengine ili kufikia makubaliano zaidi.
Kauli yake ya sasa inaleta matumaini makubwa kwa serikali ya Tanzania kuwa huenda kiasi cha zaidi ya Trilioni 400 kilichokadiriwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kikalipwa na kampuni hiyo.
Baada ya Globe kuchapisha kauli hiyo ya Thornton, Mkurugenzi Mtendaji wa Acacia, Peter Geleta aliibuka na kukanusha taarifa hiyo akisema kuwa si taarifa sahihi.
“Tulishangazwa sana na taarifa zisizo sahihi za Thornton na tumetaka Barrick watoe ufafanuzi,” aliiambia Globe.
Geleta alitoa ufafanuzi kwa wafanyakazi wake kupitia tangazo la ndani la Septemba 18 mwaka huu kuwa Acacia na kampuni zake tanzu umelipa dola bilioni 1 kama kodi na mrabaha kwa serikali kwa miaka zaidi ya 15.
Alisema kwa nusu ya mwaka huu wamelipa kodi ya mapato ya dola milioni 23.3 na mwaka jana dola milioni 34.6 na kwamba kwa miaka 15 wamelipa jumla ya dola milioni 140 kama kodi.
 
Huko Tarime mara kuna viongozi na baadhi ya walimiki wa mgodi Barack wapo mahabusu mda huu baada ya kufikishwa mahakamani leo kwa ufisadi wa pesa kwa malipo ya milahaba kwenye maeneo ya migodi, wana JF fuatilieni huko mtapata taarifa zote.
 
Kusema ukweli huyu MWENYEKITI Mtendaji wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation, Profesa John Thornton, ni mtu very intelligent!. Anaishambulia kampuni tanzu yao ya Acacia Mining, ili tuu kuipa Tanzania confidence kuwa Barrick wako na sisi, hivyo kufanya mazungumzo na serikali yetu bila kuwahusisha Acacia, na chochote kitakachofikiwa kwenye mazungumzo ya Barrick na serikali yetu, ni nothing at all Kwa sababu the determinants sio serikali yetu wala sio Barrick, bali ni Acacia.

Mtoto wako akifanya kosa kubwa la kustahili adhabu Kali hata ya kifo, wewe baba ili kumnasua mwanao, utakuwa tayari kuthibitisha kuwa mwanao ni insane, hivyo insanity ni defence kwenye criminal cases.

Anachofanya Boss wa Barrick ni kuendelea kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa, huku Barrick wakiuza shares zao, Kwa sasa tayari wameisha uza 51% majority kwa Rangold na wao kubaki na 49%, next month mkutano mkuu wa share holders unaitishwa kubariki mabadiliko hayo, hivyo sisi kujikuta hatuna chetu!.

Je, wajua kuwa mazungumzo yetu na Barrick ni mazungumzo tu? Mwenye uamuzi wa mwisho ni Acacia!, Kwanini hakushirikishwa?!. Je, Tutalipwa?. - JamiiForums

Je, wajua kuna uwezekano Barrick wanatuingiza mkenge?!. Hili la kugawana 50/50 ya faida ni kweli au ni changa la macho tu?. - JamiiForums

Mambo ya Barrick; Barrick Executive Chairman Thornton Ajiuzia Shares na kumiliki Shares Milioni 5!. - JamiiForums

Wakati Tukisubiri $ Milioni 300 zetu Kutoka Barrick, Yauza Hisa za $ Milioni 300 Kwa Mchina Huku Ikinunua Mgodi wa Randgold Kwa $ Bilioni 18.3!. - JamiiForums

Dola milioni 300, siku 90, sentano kipande haijalipwa! acacia inakula hasara, has no capacity to pay! Tumedanganywa? - JamiiForums

P
 
Jamani tumechoka kusubiri noah zetu tangu mlipoanza hamumalizi tu?.
 
Anachofanya Boss wa Barrick ni kuendelea kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa, huku Barrick wakiuza shares zao, Kwa sasa tayari wameisha uza 51% majority kwa Rangold na wao kubaki na 49%, next month mkutano mkuu wa share holders unaitishwa kubariki mabadiliko hayo, hivyo sisi kujikuta hatuna chetu!.
Mkuu kama mwana JF na mwanasheria na mtafuta habari mzuri, unaweza kutusaida vifungu vya sheria ama za kwetu ama za kimataifa ama za nchi ilikosajiliwa BArrick ili tusimamishe mchakato huu mpaka makubaliano yafikiwe baina yetu na wao(barrick)?
 
Kusema ukweli huyu MWENYEKITI Mtendaji wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation, Profesa John Thornton, ni mtu very intelligent!. Anaishambulia kampuni tanzu yao ya Acacia Mining, ili tuu kuipa Tanzania confidence kuwa Barrick wako na sisi, hivyo kufanya mazungumzo na serikali yetu bila kuwahusisha Acacia, na chochote kitakachofikiwa kwenye mazungumzo ya Barrick na serikali yetu, ni nothing at all Kwa sababu the determinants sio serikali yetu wala sio Barrick, bali ni Acacia.

Mtoto wako akifanya kosa kubwa la kustahili adhabu Kali hata ya kifo, wewe baba ili kumnasua mwanao, utakuwa tayari kuthibitisha kuwa mwanao ni insane, hivyo insanity ni defence kwenye criminal cases.

Anachofanya Boss wa Barrick ni kuendelea kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa, huku Barrick wakiuza shares zao, Kwa sasa tayari wameisha uza 51% majority kwa Rangold na wao kubaki na 49%, next month mkutano mkuu wa share holders unaitishwa kubariki mabadiliko hayo, hivyo sisi kujikuta hatuna chetu!.

Je, wajua kuwa mazungumzo yetu na Barrick ni mazungumzo tu? Mwenye uamuzi wa mwisho ni Acacia!, Kwanini hakushirikishwa?!. Je, Tutalipwa?. - JamiiForums

Je, wajua kuna uwezekano Barrick wanatuingiza mkenge?!. Hili la kugawana 50/50 ya faida ni kweli au ni changa la macho tu?. - JamiiForums

Mambo ya Barrick; Barrick Executive Chairman Thornton Ajiuzia Shares na kumiliki Shares Milioni 5!. - JamiiForums

Wakati Tukisubiri $ Milioni 300 zetu Kutoka Barrick, Yauza Hisa za $ Milioni 300 Kwa Mchina Huku Ikinunua Mgodi wa Randgold Kwa $ Bilioni 18.3!. - JamiiForums

Dola milioni 300, siku 90, sentano kipande haijalipwa! acacia inakula hasara, has no capacity to pay! Tumedanganywa? - JamiiForums

P
Kweli nimeaamini wewe siyo mwanasheria!! Hivi unajua kuwa ukinunua kampuni pia unanunua vyote including wadai na wadaiwa? Hivyo kama tayari kuna mkataba ambao unahusu Barrick kuilipa TZ then huyo mnunuaji basi ananunua na hayo madeni??. Unless kuwe hakuna makubaliano!
 
Mkuu kama mwana JF na mwanasheria na mtafuta habari mzuri, unaweza kutusaida vifungu vya sheria ama za kwetu ama za kimataifa ama za nchi ilikosajiliwa BArrick ili tusimamishe mchakato huu mpaka makubaliano yafikiwe baina yetu na wao(barrick)?
Hatuwezi kusimamisha chochote, kwa sababu we have nothing to do with Barrick. We have everything to do with Acacia, and not Barrick, kuna vitu nikivisema humu, nitaonekana mtovu wa nidhamu kwa sababu baadhi ya wahusika wa majadiliano na Accia, sio tuu ni walimu wangu pale UDSM, bali wengine ni ma supervisor wangu wa LL.B dissertation, I don't know ni kwa nini walikubali kufanya negotiations na mtu ambaye is not part to contract, Barrick, na kumuacha Acacia ambaye ndiye mhusika mkuu!.

Barrick anaweza ku offload shares zake ndani ya Acacia, kwenye hostile takeover, bila Acacia wenyewe kujua kwa kuiuza kwa Mchina Ile 64% ya Barrick ndani ya Acacia, hivyo kujikuta hatuna wa kuzungumza naye!.

Tanzania kwenye multinational corporates negotiations, ni waupe na watupu kama vilaza wa chekechea.

Nikupe mfano mdogo wa kusikitisha.
Kwenye mkataba wa Richmond, kulikuwa na kipengele kuwa uamuzi wa MIGA ni final na conclusive, tukasaini.

Kisha tukavunja mkataba baada ya kuhakikishiwa hatutashitakiwa.
Tulishitakiwa, tunashindwa, tukadaiwa fidia, tukajidai hatulipi, kiukweli, tulilipa every cent Kwa siri!. Baadhi ya wanasheria wetu, tena wenye majina makubwa, na wengine Wana titles kubwa, hadi ma professors lakini ni bure kabisa!.
P
 
Kweli nimeaamini wewe siyo mwanasheria!! Hivi unajua kuwa ukinunua kampuni pia unanunua vyote including wadai na wadaiwa? Hivyo kama tayari kuna mkataba ambao unahusu Barrick kuilipa TZ then huyo mnunuaji basi ananunua na hayo madeni??. Unless kuwe hakuna makubaliano!
Naomba nisikuite kilaza,

Kwanza hakuna mkataba wowote kati ya Barrick na Tanzania, kilichopo ni MOU tuu!.

Pili, ukiuza kampuni unaweza kuuza assets tuu na sio liabilities.

Tatu lile deni letu kwa Acacia ni deni hewa, haliko registered popote, hata Acacia ikiuzwa leo, hakuna popote deni hilo litakapo onekana.

P
 
Hapa mtetea mafisadi Lisu presha inapanda na kushuka.

Pamoja na visebengo wao chadema waliahidi tutashitakiwa MIGA !!!!!
Hii Sinema imekaa vingine tulia kwanza acha kumshutumu Lisu, huko Tarime leo wamekwenda jela wazungu wa Barick pamoja na viongozi wa CCM na inasemekana hata DC na wengineo ni watuhumiwa uchunguzi unaendelea subiria Movie bado usiwe na haraka.
 
Yote semeni lakini kusema kuwa Barrick haijalipa kodi ya mapato? TRA sio TFF jamani
 
Ungetupia kwa kidhungu kidogo kwa sisi wa fisiem ambao kuelewa kuna shida kidogo
 
Hatuwezi kusimamisha chochote, kwa sababu we have nothing to do with Barrick. We have everything to do with Acacia, and not Barrick, kuna vitu nikivisema humu, nitaonekana mtovu wa nidhamu kwa sababu baadhi ya wahusika wa majadiliano na Accia, sio tuu ni walimu wangu pale UDSM, bali wengine ni ma supervisor wangu wa LL.B dissertation, I don't know ni kwa nini walikubali kufanya negotiations na mtu ambaye is not part to contact, Barrick, na kumuacha Acacia ambaye ndiye mhusika mkuu!.

Barrick anaweza ku offload shares zake ndani ya Acacia, kwenye hostile takeover, bila Acacia wenyewe kujua kwa kuiuza kwa Mchina Ile 64% ya Barrick ndani ya Acacia, hivyo kujikuta hatuna wa kuzungumza naye!.

Tanzania kwenye multinational corporates negotiations, ni waupe na watupu kama vilaza wa chekechea.

Nikupe mfano mdogo wa kusikitisha.
Kwenye mkataba wa Richmond, kulikuwa na kipengele kuwa uamuzi wa MIGA ni final na conclusive, tukasaini.

Kisha tukavunja mkataba baada ya kuhakikishiwa hatutashitakiwa.
Tulishitakiwa, tunashindwa, tukadaiwa fidia, tukajidai hatulipi, kiukweli, tulilipa every cent Kwa siri!. Baadhi ya wanasheria wetu, tena wenye majina makubwa, na wengine Wana titles kubwa, hadi ma professors lakini ni bure kabisa!.
P
Mayala hilo sakata la Barrick na Acacia bado bichi kuna vitendawili vingi ndani yake na vingi vikitenguliwa Tanzania itapigwa 3-0 na ndege ingine itakamatwa pengine na kuzuia pesa za TZ zilizopo nje, leo hii kuna MZUNGU wa Barrick na viongozi wa CCM huko mgodini Barrick ya Tarime wamefikishwa mahakamani na wapo magerezani kwa kukosa dhamana, fuatilia upate kujua mwendelezo wa Sinema za Barrick nchini Tanzania
 
Naomba nisikuite kilaza,

Kwanza hakuna mkataba wowote kati ya Barrick na Tanzania, kilichopo ni MOU tuu!.

Pili, ukiuza kampuni unaweza kuuza assets tuu na sio liabilities.

Tatu lile deni letu kwa Acacia ni deni hewa, haliko registered popote, hata Acacia ikiuzwa leo, hakuna popote deni hilo litakapo onekana.

P
Mkuu MOU kwa kiswahili cha kawaida ina maana gani? Wewe ni bingwa wa sheria kuliko tume ya Prof. Kabudi. Wewe ni mtangazaji tu kwenye sheria ni kilaza tu!
 
Huko Tarime mara kuna viongozi na baadhi ya walimiki wa mgodi Barack wapo mahabusu mda huu baada ya kufikishwa mahakamani leo kwa ufisadi wa pesa kwa malipo ya milahaba kwenye maeneo ya migodi, wana JF fuatilieni huko mtapata taarifa zote.
Wamiliki wa Barrick wapo Canada na USA, hawaishi hata Afrika, hafu huo mrabaha unaousema hata haujui, kama wakikwepa kulipa mrabaha hiyo dhahabu itaondokaje kwenda nje ya nchi?
 
Kweli kabisa, na ndo maana jamaa wanaendesha majadiliano huku wakiuza hisa kwa Wachina tukija kushituka mchina atalipa capital gain 10% hafu ndo anakuwa mmiliki jamaa wajanja sana.
Kusema ukweli huyu MWENYEKITI Mtendaji wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation, Profesa John Thornton, ni mtu very intelligent!. Anaishambulia kampuni tanzu yao ya Acacia Mining, ili tuu kuipa Tanzania confidence kuwa Barrick wako na sisi, hivyo kufanya mazungumzo na serikali yetu bila kuwahusisha Acacia, na chochote kitakachofikiwa kwenye mazungumzo ya Barrick na serikali yetu, ni nothing at all Kwa sababu the determinants sio serikali yetu wala sio Barrick, bali ni Acacia.

Mtoto wako akifanya kosa kubwa la kustahili adhabu Kali hata ya kifo, wewe baba ili kumnasua mwanao, utakuwa tayari kuthibitisha kuwa mwanao ni insane, hivyo insanity ni defence kwenye criminal cases.

Anachofanya Boss wa Barrick ni kuendelea kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa, huku Barrick wakiuza shares zao, Kwa sasa tayari wameisha uza 51% majority kwa Rangold na wao kubaki na 49%, next month mkutano mkuu wa share holders unaitishwa kubariki mabadiliko hayo, hivyo sisi kujikuta hatuna chetu!.

Je, wajua kuwa mazungumzo yetu na Barrick ni mazungumzo tu? Mwenye uamuzi wa mwisho ni Acacia!, Kwanini hakushirikishwa?!. Je, Tutalipwa?. - JamiiForums

Je, wajua kuna uwezekano Barrick wanatuingiza mkenge?!. Hili la kugawana 50/50 ya faida ni kweli au ni changa la macho tu?. - JamiiForums

Mambo ya Barrick; Barrick Executive Chairman Thornton Ajiuzia Shares na kumiliki Shares Milioni 5!. - JamiiForums

Wakati Tukisubiri $ Milioni 300 zetu Kutoka Barrick, Yauza Hisa za $ Milioni 300 Kwa Mchina Huku Ikinunua Mgodi wa Randgold Kwa $ Bilioni 18.3!. - JamiiForums

Dola milioni 300, siku 90, sentano kipande haijalipwa! acacia inakula hasara, has no capacity to pay! Tumedanganywa? - JamiiForums

P
 
Utanunua madeni ambayo hayajathibitishwa kisheria? Au unazani wao hawana akili
Kweli nimeaamini wewe siyo mwanasheria!! Hivi unajua kuwa ukinunua kampuni pia unanunua vyote including wadai na wadaiwa? Hivyo kama tayari kuna mkataba ambao unahusu Barrick kuilipa TZ then huyo mnunuaji basi ananunua na hayo madeni??. Unless kuwe hakuna makubaliano!
 
Huko Tarime mara kuna viongozi na baadhi ya walimiki wa mgodi Barack wapo mahabusu mda huu baada ya kufikishwa mahakamani leo kwa ufisadi wa pesa kwa malipo ya milahaba kwenye maeneo ya migodi, wana JF fuatilieni huko mtapata taarifa zote.
Mkuu mbona vyanzo vyangu vya huko wananiambia kuwa hakuna kinachoendelea kuhusu taharifahii
 
Naomba nisikuite kilaza,

Kwanza hakuna mkataba wowote kati ya Barrick na Tanzania, kilichopo ni MOU tuu!.

Pili, ukiuza kampuni unaweza kuuza assets tuu na sio liabilities.

Tatu lile deni letu kwa Acacia ni deni hewa, haliko registered popote, hata Acacia ikiuzwa leo, hakuna popote deni hilo litakapo onekana.

P
Ni kweli na ndiyo mbinu hutumiwa na hizo kampuni kote barani Africa na sasa Tanzania lakini kwa Tanzania yapo mengi yamejificha ambayo yakifichuliwa itakuwa aibu kwa Duniani kotee.
 
Mkuu mbona vyanzo vyangu vya huko wananiambia kuwa hakuna kinachoendelea kuhusu taharifahii
Ngoja tuwatafute wananchi wa huko kisha tuanike namba za simu ili upate kuthibitisha hilo.
 
Back
Top Bottom