Kigogo TCAA ang'ang'ania Ofisi

Kigogo TCAA ang'ang'ania Ofisi

Informer

Platinum Member
Joined
Jul 29, 2006
Posts
1,604
Reaction score
6,698
MKURUGENZI wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Fadhili Manongi amedaiwa kung’ang’ania ofisi, licha ya kukabidhiwa barua ya kustaafu kwa mujibu wa sheria

Taarifa za uhakika ambazo gazeti hili imezipata zinasema kwamba tayari Manongi ana barua ya kustaafu tangu Machi 31, mwaka huu lakini ameendelea kuwamo ofisini.

Akiwa ndani ya ofisi hiyo, Manongi kwa sasa anaratibu safari za kiofisi ambako kwa wiki hii alikuwa Mtwara kabla ya kwenda Gaborone, Botswana. Taarifa zinasema kwamba Gabarone anakwenda kushiriki mkutano wa Wakurugenzi wa Usafiri wa Anga kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo kwa nchi za Kusini mwa Afrika.

“Huyu mtu amestaafu, hata kwenye bodi aliulizwa na akajibu atafutwe Katibu Mkuu, Katibu Mkuu akajibu kuwa wamempa barua ya kustaafu na kwamba hana budi kukabidhi ofisi, lakini hajafanya hivyo,” alisema mtoa habari.

Gazeti hili lilimtafuta Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka bila mafanikio kwa siku za Jumatatu hadi Jumatano mpaka gazeti hili linakwenda mitamboni.

Lakini lilimpa nafasi Manongi kuzungumzia uwepo wake ofisini ilihali ana barua ya kustaafu mkononi ambako alisema, “Uwepo wangu ofisini unajulikana kwa wakubwa, muulize Waziri au Katibu Mkuu.”
 

Attachments

  • habari (1).jpg
    habari (1).jpg
    809.8 KB · Views: 867
Kaka kustaafu kunataka moyo,hasa unapoangalia yale marupurupu,wizi,rushwa kubwa na ndogo,halafu unaingia kijiweni haujui kesho yako,lazima utagoma.Ila mwenye kosa ni yule anayeendelea kumlipa mshahara.
 
Katibu mkuu ni mpare na Manongi ni mpare wanatoka sehemu moja Kazi kwako
 
Kuna habari nilipashwa, kuna kamishna mmoja TRA muda wake uliisha; yeye akajua kama kawa kama dawa wataongeza ungwe ya pili...alipopewa barua aachie ofisi kaomba wampe miezi kadhaa aweke data sawa...miezi imeisha jamaa anaendelea kwenda job

Walichofanya walibadili kitasa...alichokaje....si mnajua mishahara yao ya milioni 15 kuachia ngazi ni ngumu saaana...


Kaka kustaafu kunataka moyo,hasa unapoangalia yale marupurupu,wizi,rushwa kubwa na ndogo,halafu unaingia kijiweni haujui kesho yako,lazima utagoma.Ila mwenye kosa ni yule anayeendelea kumlipa mshahara.
 
Kaka kustaafu kunataka moyo,hasa unapoangalia yale marupurupu,wizi,rushwa kubwa na ndogo,halafu unaingia kijiweni haujui kesho yako,lazima utagoma.Ila mwenye kosa ni yule anayeendelea kumlipa mshahara.
Mkuu hapo atakuja kulia na kusaga meno siku ya siku ikifika!!

Hawa jamaa huwa wanakata hela zote alizolipwa wakati akiwa tayari na barua ya kustaafu! Kuna Afisa mmoja wa kilimo huku kwetu alijiongezea siku kimya kimya akendelea kuvuta posho za safari kama kawaida. TAMISEMI ikagundua kwamba siku zote alizojilipa alikuwa anapaswa kuwa amestaafu, jamaa alitakiwa kurejesha fedha zote alizokuwa amejilipa!! Labda kama hayo yanafanyika huku mashambani tu siyo huko mijini!!
 
MKURUGENZI wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Fadhili Manongi amedaiwa kung’ang’ania ofisi, licha ya kukabidhiwa barua ya kustaafu kwa mujibu wa sheria

Taarifa za uhakika ambazo gazeti hili imezipata zinasema kwamba tayari Manongi ana barua ya kustaafu tangu Machi 31, mwaka huu lakini ameendelea kuwamo ofisini.

Akiwa ndani ya ofisi hiyo, Manongi kwa sasa anaratibu safari za kiofisi ambako kwa wiki hii alikuwa Mtwara kabla ya kwenda Gaborone, Botswana. Taarifa zinasema kwamba Gabarone anakwenda kushiriki mkutano wa Wakurugenzi wa Usafiri wa Anga kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo kwa nchi za Kusini mwa Afrika.

“Huyu mtu amestaafu, hata kwenye bodi aliulizwa na akajibu atafutwe Katibu Mkuu, Katibu Mkuu akajibu kuwa wamempa barua ya kustaafu na kwamba hana budi kukabidhi ofisi, lakini hajafanya hivyo,” alisema mtoa habari.

Gazeti hili lilimtafuta Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka bila mafanikio kwa siku za Jumatatu hadi Jumatano mpaka gazeti hili linakwenda mitamboni.

Lakini lilimpa nafasi Manongi kuzungumzia uwepo wake ofisini ilihali ana barua ya kustaafu mkononi ambako alisema, “Uwepo wangu ofisini unajulikana kwa wakubwa, muulize Waziri au Katibu Mkuu.”

inashangaza wenye nafasi nafasi nzuri NA KUBWA NDIYO Wenye kung'ang'ania ofisi, mamlaka husika ziko wapi? Kuchukua hatua? Hao wanaojiita OFMA? Wako wapi kufichua ufisadi huu ambao unaota mzizi?
 
mkuu hiyo ya kubadilisha kitasa imeniacha hoi sana. da!

Kuna habari nilipashwa, kuna kamishna mmoja TRA muda wake uliisha; yeye akajua kama kawa kama dawa wataongeza ungwe ya pili...alipopewa barua aachie ofisi kaomba wampe miezi kadhaa aweke data sawa...miezi imeisha jamaa anaendelea kwenda job

Walichofanya walibadili kitasa...alichokaje....si mnajua mishahara yao ya milioni 15 kuachia ngazi ni ngumu saaana...
 
Sidhani Katibu Mkuu anaweza kumsaidia kiongozi kama Manongi...kaiharibu sekta sana
 
inashangaza wenye nafasi nafasi nzuri na kubwa ndiyo wenye kung'ang'ania ofisi, mamlaka husika ziko wapi? Kuchukua hatua? Hao wanaojiita ofma? Wako wapi kufichua ufisadi huu ambao unaota mzizi?


ziko wapi enzi za kenya hassan? AliruDIshwa uwanja wa ndege akitaka kusafiri safari ya kikazi, ili hali ameisha staafu, katika utumishi wa umma, akina manongi wapo wengi sana, wananchi inabidi tuanze kuwafichua mmoja mmoja
 
Kuna habari nilipashwa, kuna kamishna mmoja TRA muda wake uliisha; yeye akajua kama kawa kama dawa wataongeza ungwe ya pili...alipopewa barua aachie ofisi kaomba wampe miezi kadhaa aweke data sawa...miezi imeisha jamaa anaendelea kwenda job

Walichofanya walibadili kitasa...alichokaje....si mnajua mishahara yao ya milioni 15 kuachia ngazi ni ngumu saaana...

Inabidi wafanyakazi wa serikalini wapewe mishahara mizuri ili kuwafanya wakistaafu wawe na njia mbadala ya kuishi.Tatizo kubwa linakuwa watu wanakosa zile pesa za rushwa ambazo ndiyo nyingi na sababu siyo zao kihalali zinatumika vibaya.
 
Mkuu hapo atakuja kulia na kusaga meno siku ya siku ikifika!!

Hawa jamaa huwa wanakata hela zote alizolipwa wakati akiwa tayari na barua ya kustaafu! Kuna Afisa mmoja wa kilimo huku kwetu alijiongezea siku kimya kimya akendelea kuvuta posho za safari kama kawaida. TAMISEMI ikagundua kwamba siku zote alizojilipa alikuwa anapaswa kuwa amestaafu, jamaa alitakiwa kurejesha fedha zote alizokuwa amejilipa!! Labda kama hayo yanafanyika huku mashambani tu siyo huko mijini!!

Kaka maisha ya mtaani tunayaweza walala hoi.Ukiwa na kaelfu kako utakula hata bamia.
 
Inabidi wafanyakazi wa serikalini wapewe mishahara mizuri ili kuwafanya wakistaafu wawe na njia mbadala ya kuishi.Tatizo kubwa linakuwa watu wanakosa zile pesa za rushwa ambazo ndiyo nyingi na sababu siyo zao kihalali zinatumika vibaya.

Kuna habari nilipashwa, kuna kamishna mmoja TRA muda wake uliisha; yeye akajua kama kawa kama dawa wataongeza ungwe ya pili...alipopewa barua aachie ofisi kaomba wampe miezi kadhaa aweke data sawa...miezi imeisha jamaa anaendelea kwenda job

Walichofanya walibadili kitasa...alichokaje....si mnajua mishahara yao ya milioni 15 kuachia ngazi ni ngumu saaana...

Ndugu Mishahara Mizuri au wapewe midogo ili wasiistamani wakati wa kuacha? maana naona hapo ni 15Mil au hiyo bado ni midogo?
 
Kweli mambo huenda yakabadilika, huyu jamaa alikataa kuwaongezea mikataba watumishi wengi kama alikua Clark of works, msemaji wa mamlaka, madereva wawili ila mmoja mahakama ilimrudishaa, IT Manager. Sasa yeye kama aliona mazuri why hataki kuzika a. Na ana kibaraka wake Rube Luhongole alikua akimpotosha mambo mengi nayeye amebskiza miezi michache ya kumaliza Mkataba ingawa anaonekana mzee zaidi.Walipandikiza mbegu za ubaguzi sasa unawatafuna wenyewe
 
Mr. Manongi anatakiwa ajue kila chenye mwanzo hakikosi mwisho, mwisho wako umefika unang'ang'ania kitu gani? unatembea mikoani na gali la serikali uoni aibu ? Mwenzako alostaff bwana DSR umetuma watu wakachue vitambulisho na baadhi ya vitu vya ofisi, nafasi yako ni Mkataba na sio mwajiliwa wa permanent hivyo hamna miaka 60, mkataba wako umeisha 30 March nani anakulipa mshahala?
 
Inatakiwa uwe na moyo wa chuma kustaafu kazi TCAA ni mojawapo ya taasisi ya serikali inayolipa vizuri kuliko hata BOT jumlisha na safari za nje kila wiki. Dereva tu wa std 7 anapata net laki 9- CEO siyo chini ya Ml 10. We utastaafu kweli kwa hiari?
 
Back
Top Bottom