Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,174
Wednesday, 12 January 2011
Na Hussein Issa
SIKU moja baada ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kuwasilisha pingamizi Mahakama Kuu kutaka serikali isiilipe Kampuni ya Dowans, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, ameibuka na kusema ni ruksa. Jaji Werema aliliambia gazeti hili jana kuwa, haoni tatizo lolote kwa wanasheria hao kupinga malipo hayo mahakamani, kwani suala hilo halina madhara kwa serikali.
"Waende tu (kupinga mahakamani), kwani ni sehemu ya kazi yao na huwezi kuwazuia. Hii haina madhara yoyote kwa serikali.
Mimi nimeshaongea vya kutosha kuhusu suala la Dowans na kulifafanua sana," alisema. Jaji Werema alisema tayari amesoma hukumu hiyo na kutoa mapendekezo yake kwa wizara husika, hivyo kinachotakiwa sasa ni serikali kutekeleza mapendekezo yake sio kuendeleza mjadala. "Sikiliza. Mimi nimeshatoa maoni yangu kupitia wizara husika. Hayo maswali mnayoniuliza nikiyajibu nitakuwa sijawatendei haki wananchi," alisema Jaji Werema.
Juzi LHRC, kwa kushirikiana na wanaharakati wa haki za jinsia nchini, waliwasilisha pingamizi Mahakama Kuu kupinga malipo ya fidia ya Sh97 bilioni kwa Kampuni ya Dowans. Hata hivyo, ili malipo hayo yafanyike, kesi hiyo ilipaswa kusajiliwa Mahakama Kuu jambo ambalo sasa limeonekana kuingia doa baada ya wanaharakati hao kuweka pingamizi kuzuia mchakato huo.
LHRC walitoa tamko hilo walisisitiza kuwa, wanaungwa mkono na vyama mbalimbali visivyo vya kiserikali yakiwamo mashirika yanayotetea haki za binadamu, usawa wa jinsia na ukombozi wa wanawake (FemAct).
Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Francis Kiwanga, alisema wameamua kuweka pingamizi kutokana na mikataba ya awali ya Kampuni ya Dowans kupatikana kwa rushwa na kukiuka maslahi ya umma.
"Kituo kinafungua shauri Mahakama Kuu kupinga uhalali wa tuzo iliyotolewa kwa Dowans isisajiliwe na kuwa, tuzo ya kimataifa kwa sababu mikataba ya awali ilipatikana kwa rushwa na kukiuka maslahi ya umma," alisema Kiwanga. Kiwanga alimtataja Wakili wa Kujitegemea na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Dk Sengondo Mvungi, kuwa ndiye wakili aliyeteuliwa kulisimamia shauri hilo.
"Ikiwa Bunge la Jamhuri ya Muungano kupitia Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa Novemba 13, 2007 ilithibitisha kuwa Richmond ni kampuni hewa, inawezekanaje kuwa na mkataba wa kurithisha Dowans?" alihoji Kiwanga. Kiwanga alisema Wizara ya Nishati na Madini inatia shaka kuhusu mwenendo wa suala zima la Dowans na kutaka Tanesco kukataa kulipa deni hilo.
"Uhalali wa kisheria wa miliki ya Dowans kwa mali za Richmond haupo. Ni kwanini serikali haikutaifisha mali za Richmond tangu awali? Pili ikiwa Dowans haikurithi kwa halali mali ya Richmond, inawezekanaje Dowans kuwa na madai halali dhidi ya serikali ya Tanzania?" alihoji Kiwanga.
Kiwanga alielezea shaka kwa serikali kuwa na uharaka wa kulipa deni hilo bila hata kuchukua hatua zozote za kisheria. Alihoji, "Nini hasa maslahi ya Wizara ya Nishati na Madini hasa ikizingatiwa ndio iliyoshinikiza Tanesco kukubali kuhusishwa na kuhamishwa kwa mkataba wa Richmond kwenda Dowans?"
Na Hussein Issa
SIKU moja baada ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kuwasilisha pingamizi Mahakama Kuu kutaka serikali isiilipe Kampuni ya Dowans, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, ameibuka na kusema ni ruksa. Jaji Werema aliliambia gazeti hili jana kuwa, haoni tatizo lolote kwa wanasheria hao kupinga malipo hayo mahakamani, kwani suala hilo halina madhara kwa serikali.
"Waende tu (kupinga mahakamani), kwani ni sehemu ya kazi yao na huwezi kuwazuia. Hii haina madhara yoyote kwa serikali.
Mimi nimeshaongea vya kutosha kuhusu suala la Dowans na kulifafanua sana," alisema. Jaji Werema alisema tayari amesoma hukumu hiyo na kutoa mapendekezo yake kwa wizara husika, hivyo kinachotakiwa sasa ni serikali kutekeleza mapendekezo yake sio kuendeleza mjadala. "Sikiliza. Mimi nimeshatoa maoni yangu kupitia wizara husika. Hayo maswali mnayoniuliza nikiyajibu nitakuwa sijawatendei haki wananchi," alisema Jaji Werema.
Juzi LHRC, kwa kushirikiana na wanaharakati wa haki za jinsia nchini, waliwasilisha pingamizi Mahakama Kuu kupinga malipo ya fidia ya Sh97 bilioni kwa Kampuni ya Dowans. Hata hivyo, ili malipo hayo yafanyike, kesi hiyo ilipaswa kusajiliwa Mahakama Kuu jambo ambalo sasa limeonekana kuingia doa baada ya wanaharakati hao kuweka pingamizi kuzuia mchakato huo.
LHRC walitoa tamko hilo walisisitiza kuwa, wanaungwa mkono na vyama mbalimbali visivyo vya kiserikali yakiwamo mashirika yanayotetea haki za binadamu, usawa wa jinsia na ukombozi wa wanawake (FemAct).
Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Francis Kiwanga, alisema wameamua kuweka pingamizi kutokana na mikataba ya awali ya Kampuni ya Dowans kupatikana kwa rushwa na kukiuka maslahi ya umma.
"Kituo kinafungua shauri Mahakama Kuu kupinga uhalali wa tuzo iliyotolewa kwa Dowans isisajiliwe na kuwa, tuzo ya kimataifa kwa sababu mikataba ya awali ilipatikana kwa rushwa na kukiuka maslahi ya umma," alisema Kiwanga. Kiwanga alimtataja Wakili wa Kujitegemea na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Dk Sengondo Mvungi, kuwa ndiye wakili aliyeteuliwa kulisimamia shauri hilo.
"Ikiwa Bunge la Jamhuri ya Muungano kupitia Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa Novemba 13, 2007 ilithibitisha kuwa Richmond ni kampuni hewa, inawezekanaje kuwa na mkataba wa kurithisha Dowans?" alihoji Kiwanga. Kiwanga alisema Wizara ya Nishati na Madini inatia shaka kuhusu mwenendo wa suala zima la Dowans na kutaka Tanesco kukataa kulipa deni hilo.
"Uhalali wa kisheria wa miliki ya Dowans kwa mali za Richmond haupo. Ni kwanini serikali haikutaifisha mali za Richmond tangu awali? Pili ikiwa Dowans haikurithi kwa halali mali ya Richmond, inawezekanaje Dowans kuwa na madai halali dhidi ya serikali ya Tanzania?" alihoji Kiwanga.
Kiwanga alielezea shaka kwa serikali kuwa na uharaka wa kulipa deni hilo bila hata kuchukua hatua zozote za kisheria. Alihoji, "Nini hasa maslahi ya Wizara ya Nishati na Madini hasa ikizingatiwa ndio iliyoshinikiza Tanesco kukubali kuhusishwa na kuhamishwa kwa mkataba wa Richmond kwenda Dowans?"