King Octavian
JF-Expert Member
- Oct 1, 2011
- 403
- 353
Wakuu mambo vipi! Naomba kuuliza kwa waliowahi kutumia au wanaotumia hivi vifurushi vya internet vya voda, wanidaidie kwa hili hiki kifurushi cha internet cha mwezi cha kudownload bila kikomo(unlimited download) wanachokiuza shillingi 40,000/= je, speed yake ya kudownload nayo ina pungua kasi unapokua umedownload GB kadhaa? au ni uniform speed kwa muda wote ndani ya huo mwezi husika? Nimeuliza hivi kwa sababu nimewahi jiunga na kifurushi cha wiki nzima chenye gharama ya shilingi 12,500/= mwanzoni speed ikawa powa inayokwenda mpaka 1Mbps, lakini baada ya kudownload kama 2Gb speed ikashuka saana mpaka kwenye 30kbps. Kwa wenye ufahamu wanisaidie kwa hili nataka kuunga kifurushi hiki lakini nahofia isije ikawa kina utaratibu kama wa cha wiki, elf40 nyingi bwana.
Hiki cha mwezi kinapungua speed au hakipungui? na kama kinapungua ni baada ya kudownload Data kiasi gani?
Asanteni.
Hiki cha mwezi kinapungua speed au hakipungui? na kama kinapungua ni baada ya kudownload Data kiasi gani?
Asanteni.