Alloyce PR
JF-Expert Member
- Nov 15, 2020
- 590
- 706
"Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali kuhusu mienendo ya vyama vya siasa, chama cha siasa hufikia mwisho wa uhai wake, 'kifo cha mende' si kwa kupigwa marufuku rasmi au kushindwa kwenye sanduku la kura, bali kinapopotoka kimaadili na kisera kwa kujikita katika ulaghai na siasa za porojo.
Dalili kuu ya kufa kwa chama ni pale kinapoacha kujenga hoja zenye mwelekeo wa kitaifa na badala yake kuibuka na ajenda za kusaka umaarufu wa muda mfupi zisizo na msingi wa kisera wala kiuchumi, mfano wa hoja potofu nikutoa ahadi za kuanzisha pensheni kwa waendesha boda-boda bila mpango madhubuti wa utekelezaji. Uhalisia wa siasa unahitaji uaminifu, tafiti sahihi, na sera endelevu, si miujiza ya kisiasa isiyo na mizizi kwenye uhalisia wa rasilimali na mifumo ya kijamii." Alloyce, P.R.
Dalili kuu ya kufa kwa chama ni pale kinapoacha kujenga hoja zenye mwelekeo wa kitaifa na badala yake kuibuka na ajenda za kusaka umaarufu wa muda mfupi zisizo na msingi wa kisera wala kiuchumi, mfano wa hoja potofu nikutoa ahadi za kuanzisha pensheni kwa waendesha boda-boda bila mpango madhubuti wa utekelezaji. Uhalisia wa siasa unahitaji uaminifu, tafiti sahihi, na sera endelevu, si miujiza ya kisiasa isiyo na mizizi kwenye uhalisia wa rasilimali na mifumo ya kijamii." Alloyce, P.R.