Kifo cha mende kwa chama cha siasa

Kifo cha mende kwa chama cha siasa

Ngoja nikae nifuatilie hili vizuri mkuu, yamkini nikapata uelewa kuhusu hilo tofauti na ambavyo nilifikiria kabla.
Kwanini haukufuatilia au kufanya utafti wa hiyo agenda ( boda boda kupewa pension) kabla.
Badala yake umekimbia jf kuandika thread ukiwa ume-conclude kwamva ni kitu ambacho hakiwezekani ni political propaganda?
 
Kwanini haukufuatilia au kufanya utafti wa hiyo agenda ( boda boda kupewa pension) kabla.
Badala yake umekimbia jf kuandika thread ukiwa ume-conclude kwamva ni kitu ambacho hakiwezekani ni political propaganda?
Naomba msaada mmoja unaweza kunipa source ya uhakika inayoelezea Rwanda inavyotoa pensheni kwa boda-boda au hata nchi nyingine kama unayo. Naomba msaada mkuu kwenye hilo nipate kujifunza.
 
Ngoja nikae nifuatilie hili vizuri mkuu,
Kabla hujaomba nikupe source , ulisema ngoja ukae ufuatilie vizuri . Je umefuatilia au unataka nifanye kazi ambayo uliahidi kuifanya kwa faida yako?
Naomba msaada mmoja unaweza kunipa source ya uhakika inayoelezea Rwanda inavyotoa pensheni kwa boda-boda au hata nchi nyingine kama unayo. Naomba msaada mkuu kwenye hilo nipate kujifunza.
 
"Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali kuhusu mienendo ya vyama vya siasa, chama cha siasa hufikia mwisho wa uhai wake, 'kifo cha mende' si kwa kupigwa marufuku rasmi au kushindwa kwenye sanduku la kura, bali kinapopotoka kimaadili na kisera kwa kujikita katika ulaghai na siasa za porojo.

Dalili kuu ya kufa kwa chama ni pale kinapoacha kujenga hoja zenye mwelekeo wa kitaifa na badala yake kuibuka na ajenda za kusaka umaarufu wa muda mfupi zisizo na msingi wa kisera wala kiuchumi, mfano wa hoja potofu nikutoa ahadi za kuanzisha pensheni kwa waendesha boda-boda bila mpango madhubuti wa utekelezaji. Uhalisia wa siasa unahitaji uaminifu, tafiti sahihi, na sera endelevu, si miujiza ya kisiasa isiyo na mizizi kwenye uhalisia wa rasilimali na mifumo ya kijamii." Alloyce, P.R.
Wakati tunaanzisha PSSN 1 kwenye TASAF mwaka 2012, watu wengi walipinga andiko tulilopeleka WB kuwa haitawezekana.

Leo hii zaidi ya Watanzania milioni 1 wananufaika na TASAF (japokuwa kuna kaya hewa nyingi zinawekwa na VEOs/WEOs) kila mwaka.

Shida kubwa ya sisi tunajiita/tunaoitwa wasomi ni kutofanya tafiti hata za maeneo tunapoishi, na hili ni tatizo kubwa sana kwenye ngazi ya taifa, maana serikali na tafiti ni ardhi na mbingu, ndio maana hatufiki kwenye maendeleo.

Hata CHF walisema haiwezekani.
MKURABITA pia walisema haiwezekani.
 
Wakati tunaanzisha PSSN 1 kwenye TASAF mwaka 2012, watu wengi walipinga andiko tulilopeleka WB kuwa haitawezekana.

Leo hii zaidi ya Watanzania milioni 1 wananufaika na TASAF (japokuwa kuna kaya hewa nyingi zinawekwa na VEOs/WEOs) kila mwaka.

Shida kubwa ya sisi tunajiita/tunaoitwa wasomi ni kutofanya tafiti hata za maeneo tunapoishi, na hili ni tatizo kubwa sana kwenye ngazi ya taifa, maana serikali na tafiti ni ardhi na mbingu, ndio maana hatufiki kwenye maendeleo.

Hata CHF walisema haiwezekani.
MKURABITA pia walisema haiwezekani.
Asante sana mkuu, umeeleza vyema na mimi ngoja nijifunze kuhusu hili.
 
Asante sana mkuu, umeeleza vyema na mimi ngoja nijifunze kuhusu hili.
Usiwe unakimbilia kusema jambo fulani haliwezekani.
Kuna chama kiliweka elimu bure kwenye sera/ilani yake, na CCM walipinga kuwa haiwezekani, lakini tulikuja kuona CCM wakiichukua na kuifanyia kazi na ikawezekana (japokuwa bado kuna ubishani kuwa si bure sababu ya michango).
 
Usiwe unakimbilia kusema jambo fulani haliwezekani.
Kuna chama kiliweka elimu bure kwenye sera/ilani yake, na CCM walipinga kuwa haiwezekani, lakini tulikuja kuona CCM wakiichukua na kuifanyia kazi na ikawezekana (japokuwa bado kuna ubishani kuwa si bure sababu ya michango).
Hilo tutajadili siku nyingine. Sijasema haiwezekani, suala ni kuwa wanapotoa ahadi wanakua wamefanya utafiti kwa kiwango gani kujiridhisha na utekelezaji wake.
 
Lazima tuanze na kuwawezesha wananchi kuzalisha halafu pension baadaye.
Fikra zetu zijengwe kwenye kuwawezesha wananchi kiuchumi wakati wakiwa vijana badala ya kuwafanya tegemezi Annapolis serikali itaweza kujenga mifumo imara ya hifadhi ya jamii na hivyo pension kwao.
 
Hilo tutajadili siku nyingine. Sijasema haiwezekani, suala ni kuwa wanapotoa ahadi wanakua wamefanya utafiti kwa kiwango gani kujiridhisha na utekelezaji wake.
Hii inchi ina wasomi wengi tu wazuri.
Tafiti za changamoto zinazoikabili jamii yetu na tatuzi zake zipo nyingi tu zimefanyika na zipo makabatini zinapigwa na vumbi.

Kwa wanasiasa, huwa wanaweza kuchukua tafiti fulani na kueleza kuwa wana tatuzi ya changamoto fulani lakini hawawezi kuweka hadharani njia za kutatua hizo changamoto.

Wanasiasa ni wabinafsi, lakini hilo haliwafanyi kuwa hawana njia za utatuzi wa changamoto.

Kama ulisikia leo wakati Kitila anataka kuwataja walioshiriki kuandaa ilani, aliambiwa asitaje majina ya wasomi walioshiriki.
Fikiria na utapata sababu kwa nini.
 
"Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali kuhusu mienendo ya vyama vya siasa, chama cha siasa hufikia mwisho wa uhai wake, 'kifo cha mende' si kwa kupigwa marufuku rasmi au kushindwa kwenye sanduku la kura, bali kinapopotoka kimaadili na kisera kwa kujikita katika ulaghai na siasa za porojo.

Dalili kuu ya kufa kwa chama ni pale kinapoacha kujenga hoja zenye mwelekeo wa kitaifa na badala yake kuibuka na ajenda za kusaka umaarufu wa muda mfupi zisizo na msingi wa kisera wala kiuchumi, mfano wa hoja potofu nikutoa ahadi za kuanzisha pensheni kwa waendesha boda-boda bila mpango madhubuti wa utekelezaji. Uhalisia wa siasa unahitaji uaminifu, tafiti sahihi, na sera endelevu, si miujiza ya kisiasa isiyo na mizizi kwenye uhalisia wa rasilimali na mifumo ya kijamii." Alloyce, P.R.
Labda kama huna akili, ANC ilipigwa marufuku na kiongozi wake aliwekwa jela kwa miaka 27, je ilikufa?
 
Labda kama huna akili, ANC ilipigwa marufuku na kiongozi wake aliwekwa jela kwa miaka 27, je ilikufa?
Labda wewe ndio kama hauna akili, hilo andiko limezungumzia mtu au chama kuwekwa ndani?

Uwe unasoma andiko au wakati mwingine soma walau comment utajua andiko linahusu nini. Wacha kukurupuka mkuu.
 
Hii ya kuwapa bodaboda pensheni nilipoisikia, nilisikitika sana. Kupewa wanaweza kupewa, lakini sio kwa utaratibu aliousema Heche.

Ninavyojua, ni ngumu kupewa pensheni kama huchangii. Watumishi wengine wanachangia sehemu ya kipato chao ndio maana wanalipwa pensheni. Kama Heche na Chadema wanaweza kuwalipa bodaboda bila kuchangia, hiyo ni political propaganda na kitu kisichowezekana.
Nakumbuka aliwahi kuhojiwa Mzee SITTA (marehemu )Kuhusu SERA ya elimu bure iliyokuwa inahubiriwa na CHADEMA,Aliulizwa kuhusu suala la kutoa ELIMU bure kuanzia chekechea hadi kidato cha nne, MZEE SITTA alipinga sana na kusema hilo jambo haliwezekani.Lakini sasa hivi elimu ni bure mpaka kidato cha 4, kwahiyo usipinge tu kaka hakuna kisichowezekana.
 
Back
Top Bottom