Kifaa cha kupoza joto

Kifaa cha kupoza joto

Ulongupanjala

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2013
Posts
8,506
Reaction score
13,976
Wakuu heshima kwenu,

Naomba kujua maana naamini hapa JF kuna great thinkers.

Nina mtoto mchanga na ninaishi Tanga mjini,kwa ujumla ni joto sana iwe usiku hata mchana na inapelekea mtoto kulia na kuota vipele vingi vya jasho.

Je kuna kifaa ambacho ni kizuri kwa kupoza joto na bila kumuathiri mtoto? ninaona feni sio njia sahihi maana ni hatari kwa mtoto,pia sina uwezo wa kutumia AC kutokana na kushea mita ya umeme na itapelekea kero kwa wengine.

Naomba ushauri wenu na kama mtu anajua kifaa cha kupoza joto anitajie jina na bei pia.

Asanteni wote.
 
Tafuta kuna feni fulani unajaza maji kwenye inapoza vyema kabisa au ikibidi uweke feni za stand au mezani sio mapangaboi hizo feni ziwe hata tatu ila zote ziwe zinapuliza kwenye ukuta kisha hewa ina circulate chumba kizima itakuwa nafuu sana kwa mtoto manake unakuwa kama upepo tu katika mazingira ya kawaida.
 
Wakuu heshima kwenu,

Naomba kujua maana naamini hapa JF kuna great thinkers.

Nina mtoto mchanga na ninaishi Tanga mjini,kwa ujumla ni joto sana iwe usiku hata mchana na inapelekea mtoto kulia na kuota vipele vingi vya jasho.

Je kuna kifaa ambacho ni kizuri kwa kupoza joto na bila kumuathiri mtoto? ninaona feni sio njia sahihi maana ni hatari kwa mtoto,pia sina uwezo wa kutumia AC kutokana na kushea mita ya umeme na itapelekea kero kwa wengine.

Naomba ushauri wenu na kama mtu anajua kifaa cha kupoza joto anitajie jina na bei pia.

Asanteni wote.
Mkuu Tumia Air cooler zipo za bei powa..
 
Hizi aircooler nimewahi kununua lkn ni fake tupu,nilirudisha dukani niliponunua mlimani city.
 
Chukua barafu weka ktika ndoo toboa matundu pembeni ya ndoo. Chukua fan toboa mfuniko wa ndoo iyo fani uweke pale ulipotoboa ipulize ndane ya ndoo. Utapata ac safi sana
 
Nunua zile fan zasaloon ile unaifunga dirishani alafu iwashe nombr ndogo baada ya mba mfupi itakuwa imechukuaewa ya nje na kuingiza ndani ndani kutapoa gharama ni kama 40000/ivi
 
Nunua zile fan zasaloon ile unaifunga dirishani alafu iwashe nombr ndogo baada ya mba mfupi itakuwa imechukuaewa ya nje na kuingiza ndani ndani kutapoa gharama ni kama 40000/ivi
Tutajie jina Mkuu inaitwaje. Thanks!
 
Mh, upo Tanga eeh, ok fanya hivi, kwanini usihamie Lushoto kwa muda then mwezi april unarudi Tanga mjini?
Kama ni kazi u can still work as well, maana gari za lushoto coaster zinaingia Tanga mjini mapema sana.
 
Asante kwa ushauri mzuri nitaufikiria!!!!!!!!!!!

Mh, upo Tanga eeh, ok fanya hivi, kwanini usihamie Lushoto kwa muda then mwezi april unarudi Tanga mjini?
Kama ni kazi u can still work as well, maana gari za lushoto coaster zinaingia Tanga mjini mapema sana.
 
Back
Top Bottom