GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 63,029
- 126,474
Leo Katika Kipindi Chao Cha Morning Magic Kinachorushwa Na Radio Ya Magic FM Akiwa Na Mtangazaji Muongozaji Wao Orest Kawau, Maria Edward Na Salum Mkambala Huyu Mtangazji Mzee Kibwana Dachi Tena Katika Hali Ya Kujiamini Kana Kwamba Yeye Anayajua Mambo Ya Dhehebu La WAKATOLIKI Huku Akiwa Anatoa UFAFANUZI Kwa Kuhusiana Na Moshi Mweupe Na Mweusi Ambao Huwa Unatoka Wakati Makadinali Duniani Wakiwa Katika Mchakato Wa Kumtafuta PAPA.
Yeye KIBWANA DACHI Tena Kwa Mbwembwe Zote Na Akitamka Kabisa Kwa Wenzake Namnukuu ;
" Jamani Hili Halina Ubishi Wala Usiri Na Nasema Ukweli Kuhusiana Na Hili Jambo Ambapo Ni Kwamba Duniani Kote Hakuna Kanisa Ambalo LINAAMINI USHIRIKINA Kushinda Yote Kama La WAKATOLIKI " Mwisho Wa Kumnukuu.
Na Bahati Nzuri Hiyo Kauli Yake Naamini Hata Watu Wa TCRA Watakuwa Wameirekodi.
Nikiwa Kama Mmoja Wa WAKATOLIKI Tena NILIYETUKUKA Kabisa Nawaomba Upesi Na Haraka Sana Mabosi Zake Hawa Watutake Radhi WAKATOLIKI Wote Tanzania
Kisha Na Yeye Mwenyewe KIBWANA DACHI Kupitia Radio Yake Hiyo Hiyo Anayoifanyia Kazi Ya Magic FM Na Kwa Ukubwa Na Umuhimu Ule Ule ATUOMBE RADHI Sisi WAKATOLIKI Wote Nchini Tanzania Kabla Na Sisi Hatujachafua Hali Ya Hewa Kuanzia Kwa Dini Yake ( Ambayo Tunaijua ), Alichokifanya Mzee Wake Wakati Akiwa Afisa Mwandamizi Wa Jeshi La Polisi, Maisha Yake Binafsi Na Bila Kusahau Na AFYA YAKE Kiujumla.
AMETUDHALILISHA KULIKOTUKUKA SISI WAKATOLIKI WOTE NCHINI TANZANIA Na DUNIANI KWA UJUMLA. Na Najua Humu JF Yupo Na Hata Hao Mabosi Zake Niliowataja Hapo Na Wafayakazi Wenzake Wapo Humu Naomba Wamtaarifu Na ATUTAKE RADHI UPESI Na HARAKA Kabla Watu HATUJAFUNGUKA Na KUFUNGUKA Juu Yake Kwa Tunayoyajua.
====
JAMIIFORUMS: Tumepokea ujumbe kutoka kwa Kibwana Dachi kuhusiana na hili suala. Ujumbe wenyewe ni huu hapa;
Yeye KIBWANA DACHI Tena Kwa Mbwembwe Zote Na Akitamka Kabisa Kwa Wenzake Namnukuu ;
" Jamani Hili Halina Ubishi Wala Usiri Na Nasema Ukweli Kuhusiana Na Hili Jambo Ambapo Ni Kwamba Duniani Kote Hakuna Kanisa Ambalo LINAAMINI USHIRIKINA Kushinda Yote Kama La WAKATOLIKI " Mwisho Wa Kumnukuu.
Na Bahati Nzuri Hiyo Kauli Yake Naamini Hata Watu Wa TCRA Watakuwa Wameirekodi.
Nikiwa Kama Mmoja Wa WAKATOLIKI Tena NILIYETUKUKA Kabisa Nawaomba Upesi Na Haraka Sana Mabosi Zake Hawa Watutake Radhi WAKATOLIKI Wote Tanzania
- Dina Chahali
- Dativas Mango
- Nicky Ngonyani
- Orest Kawau
Kisha Na Yeye Mwenyewe KIBWANA DACHI Kupitia Radio Yake Hiyo Hiyo Anayoifanyia Kazi Ya Magic FM Na Kwa Ukubwa Na Umuhimu Ule Ule ATUOMBE RADHI Sisi WAKATOLIKI Wote Nchini Tanzania Kabla Na Sisi Hatujachafua Hali Ya Hewa Kuanzia Kwa Dini Yake ( Ambayo Tunaijua ), Alichokifanya Mzee Wake Wakati Akiwa Afisa Mwandamizi Wa Jeshi La Polisi, Maisha Yake Binafsi Na Bila Kusahau Na AFYA YAKE Kiujumla.
AMETUDHALILISHA KULIKOTUKUKA SISI WAKATOLIKI WOTE NCHINI TANZANIA Na DUNIANI KWA UJUMLA. Na Najua Humu JF Yupo Na Hata Hao Mabosi Zake Niliowataja Hapo Na Wafayakazi Wenzake Wapo Humu Naomba Wamtaarifu Na ATUTAKE RADHI UPESI Na HARAKA Kabla Watu HATUJAFUNGUKA Na KUFUNGUKA Juu Yake Kwa Tunayoyajua.
====
JAMIIFORUMS: Tumepokea ujumbe kutoka kwa Kibwana Dachi kuhusiana na hili suala. Ujumbe wenyewe ni huu hapa;
Mimi Kibwana Dachi wa Magic Fm, katika kipindi cha Morning Magic cha leo tarehe 16/07/2015 nakubali kwamba nilifanya kosa la msingi la kuzungumzia jambo linalohusu uchawi na kulihusisha Kanisa Katoliki, kwanza naomba radhi kwa usumbufu niliousababisha kwa watanzania wenzangu hususan wale waamini wa dhehebu hilo, ukweli nilichotaka kusema ni kwamba, Kanisa hilo lina idara maalum ambayo inatafiti uwepo wa uchawi duniani.
Idara hii ipo Vatican na nia yake ni kujua ukweli na si vinginevyo, lakini kutokana na hilo wengi wanahusisha uwepo wa tukio la kuwepo Moshi mweusi au mweupe wakati wa kumchagua PAPA ni tukio linalotokana na "utafiti huo", ukweli kinachosababisha hilo ni maombi ya dhati yanayofanywa na maaskofu na mapadri wakati wa mchakato wa kumpata Papa mpya haina uhusiano na utafiti huo narudia tena.
Hivyo nawaomba radhi wale wote niliowakwaza kwa kuwa najiamini mimi ni mtu makini ila wakati mwingine nafanya makosa ya kibinadamu.