Kibiti: Wanafunzi wateketeza Shule, Serikali yaifunga

Ufunuo wa Yohana

JF-Expert Member
Oct 9, 2007
319
67

Sourse: Mtanzania ya leo
 
Nafikiri, kuribu mali ya shule na kuchoma kilichopo hata kidogo sio solution ya matatizo bali ni kuongezea, nafikiri umefika wakati ambao sasa vitendo vya aina hii vikemewe ili kujenga jamii inayothamini kidogo kilichopo, wangeweza kuchukua hatua nyingine nyingi zaidi ya kuchoma hadi vitabu library, this is terrible wakifungua watapata wapi vitabu japo kidogo.
 
haya... na waha wafukuzeni na muwafungie wasisome tena shule yeyote, na muwapeleke mahakamani....!@#$%#%^!&*#()....
 

kwa watoto hii lugha haipo kabisa, ni jukumu lako wee mkuu wa shule uweze kudili na hawa watoto, fujo zao ni reflection ya upungufu wa akili wa mkuu wa shule unaopelekea kuwa na maamuzi mabaya.
 
tatizo la viongozi wetu ni maneno mengi tu bila vitendo.bora wamechoma ili ifanyiwe ukarabati kuliko kupokea ahadi tu kila kukicha.
kuna hili tatizo la usiri ktk utendaji ambalo ndio kikwazo,kwani linapotokea jambo ndio utasikia serikali inakuja na kusema tulikuwa tunataka kufanya hivi na vile.hii yote inatokana na kuwa na viongozi wasiokuwa na maamuzi.
Ninapendekeza yafuatayo;
1,shule ziwe na bajeti zao kwa maana ya kupewa mgao wao kwa mwaka wa fedha.
2,wizara kazi yao ni kusimamia na kuangalia utekelezaji unakwenda kama ulivyopangwa.
3,shule zipewe jukumu la kuajiri waalimu kutokana na mahitaji ilikuondoa tatizo la walimu,badala ya kusubiri wizara kuwapangia.
4,mipango ya shule iwe wazi kwa wadau wote ilikuondoa migongano ktk jamii husika
 
"Yako matatizo ya msingi katika shule zetu na madai ya wanafunzi wa Kibiti yalikuwa ya msingi, lakini walikosa uvumilivu. Matatizo hayo hayakuanza leo, yanatatuliwa kwa njia ya majadiliano sio kuharibu mali za shule," alisema Mahiza.

Sasa yalianza lini? na kwa nini hayatatuliwi? Na kama ni ya msingi kwa nini yasishughulikiwe haraka?

....hatutachukua tena wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne. Itakuwa na kidato cha tano na sita kwa sababu wanafunzi wa madarasa ya chini wamekuwa vinara katika vurugu," alisema.
Yale yale ya Tambaza, lakini kumbuka mkoa wa Pwani unaupungufu wa shule za sekondari si kama Dar.
 
Ndiyo haya haya yanayoendelea mpaka chuo kikuu. Palikuwa na tatizo gani kukaa na wanafunzi na kuwaeleza kinachokusudiwa kufanywa kuhusu kero zao? Na baada ya hapo kuhakikisha kuwa zinatatuliwa mapema iwezekanavyo? Kuondoa hivyo vidato vya chini ndiyo kweli vitamaliza tatizo? Nina hakika hao wa vidato vya juu wakiona hali inaendelea vile ilivyo na watetezi hawapo nao watafanya haya haya! Cha muhimu ni kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa hii migongano.
 
Hawa wanafunzi ni ajabu sana, inawezekanaje ukasahau kilichokupeleka pale shuleni? kweli umekwenda kufanya uharibifu ama?
 
Hawa wanafunzi ni ajabu sana, inawezekanaje ukasahau kilichokupeleka pale shuleni? kweli umekwenda kufanya uharibifu ama?

wanawaiga kaka zao wa UDSM. Kwa vile tunashangilia ya kule basi tushangilie na haya. Mimi naungana na uongozi wa UDSM kuwachukulia hatua kali wanafunzi wote waliofanya fujo za aina yeyote pale chuo kikuu mlimani ili iwe fundisho kwa wengine wote wanaodhani kudai haki kwa kufanya fujo ndio kupata haki. Wadoo zetu mjifunze kuwa na busara wakati wa kuelezea matatizo yenu. Hii jazba na hasira mnayoiinza mkiwa wadogo mtaiendeleza mkikua. Hime wazazi tujadiliane na watoto wetu umuhimu wa uvumilivu hasa wakati wa matatizo.
 
Usipoziba ufa utajenga ukuta.

Hii migomo isipotafutiwa ufumbuzi thabiti haitakomea kwa wanafunzi tu.
Matatizo ya msingi yatatuliwe mapema siyo kusubiri migomo ambayo inaingiza hasara hasa kwa fedha ya walipa kodi.

Baadaye watafuatia wafanyakazi wakiwamo wahadhiri wa vyuo vikuu, walimu wa sekondari na shule za misingi,watafuata wamiliki wa mabasi makubwa na daladala,watafuata wananchi waishio karibu na migodiya dhahabu na tanzanite na itafikia kwamba hao wanaodhibiti migomo nao watagoma(polisi,jeshi na vyombo vingine vya usalama) ndipo nchi haitakalika.Ndiko tunakoelekea kwa kuwa matatizo ya msingi hata kwa hao wana usalama wa Taifa itafikia nao hawatatuliwa kwa uchumi huu tulio nao sasa umepwaya.
 
sioni tatizo la kuwaumu wanafunzi,kwalichokifanya ndio upeo wao wa kuelewa.serikali ndio inalea matatizo yote haya na sisi tunabaki kunyoosheana vidole eti wanafunzi hawana adabu,huku ni kupotoka kimaono na kuona maisha ya mtanzania yahaitaji kilicho bora ila kwa viongozi tu.
 
Nafikiri SERIKALI lazima ijaribu kutatua migogoro ya wanafunzi kabla hali haijawa mbaya.Hivi karibuni wanafunzi mbalimbali wamefanya fujo,mfano
1.CHIDYA SEKONDARI
2.BAGAMOYO SEKONDARI
3.KIBITI SEKONDARI
4.UDSM
Wanafunzi sasa wanajua habari za MAFISADI wanaokula nchi na serikali imekaa chini inawaogopa wakati wao wanaendelea kupata tabu
Nafikiri SERIKALI isipoangalia wataendelea kufunga shule/vyuo na kufukuza wanafunzi lakini hiyo sio suluhisho
Watafute chanzo kwa nini wanafunzi wanafanya fujo ili waweze kuzizuia zisitokee
 

Wawe na busara gani tena? wameandika barua nyingi tu kwa uongozi wa chuo kuhusu madai yao na hayatatuliwi je, wakae nayo tu? Hivi unafikiri kwa nini watu hupigana vita duniani do you think hawana akili wote..NO..ni kwa sababu dulu za mazungumzo zimeshindikana. Actually adhabu kali si suluhisho...suluhisho ni kusolve matatizo yao.
 
“Yako matatizo ya msingi katika shule zetu na madai ya wanafunzi wa Kibiti yalikuwa ya msingi, lakini walikosa uvumilivu. Matatizo hayo hayakuanza leo, yanatatuliwa kwa njia ya majadiliano sio kuharibu mali za shule,” alisema Mahiza.

Kumbe Serikali inakiri kuwa Matatizo yao ni ya muda mrefu,sasa kwa nini walikuwa hawayatatui wanafanya nao mazungumzo gani hayo??


Wao siyo CUF wanaoendelea kuchezewa danadana kwenye kusaini Muafaka, kila siku mazungumzo-mazungumzo..wale ni wasomi pevu na wala siyo watoto wadogo...nadhani kilichochangia zaidi ni hiyo hali ya kuibuka kwa Mijizi ambayo kila pesa inapotajwa, inakuwa ni Mipesa, EPA, BOT, Chenge, mara Yona wakati nyie mnaambiwa mazungumzo. we utaacha kuwa na hasira kweli.

Hii italeta ushawishi kwa Serikali kuwa inatimiza kile ilichokiahidi kwa wakati. Ooh! Serikali haina pesa, mpaka mwaka ujao wa fedha 2009/2010. Za kupeleka kwenye Mabenki ya Ulaya zipo.

Naunga mkono hoja!
 

Serikali ya ccm imeshindwa kufanya chochote katika nchi hii na haya ni matokeo yake.
 

Wewe ndiye kichwa mgando kweli kweli. haki ya wananchi huwa haingoji kesho. Ukiona haki yako inapotea basi unadai papo hapo bila kuchelewa.
 
kaka Mgaya, punguza hasira, watu tunapishana uelewa kutokana na makuzi, elimu na taaluma.Mhandisi lugha yake ni tofauti na Doctor, pia Mchungaji/ Shekh lugha yake ni tofauti na Wanasiasa

Inaonyesha wewe ulicheza Skauti ama Mgambo, Maana hukawii kumpa mtu adhabu! Isije ikawa jana ndiyo ulirejea kutokea Comoro, kama ni hivyo karibu nyumbani

Wewe ndiye kichwa mgando kweli kweli. haki ya wananchi huwa haingoji kesho. Ukiona haki yako inapotea basi unadai papo hapo bila kuchelewa.

Jaribu kutoa elimu zaidi iliaelewe
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…