Kibiti: Wanafunzi wateketeza Shule, Serikali yaifunga

Ufunuo wa Yohana

JF-Expert Member
Oct 9, 2007
318
67
Wanafunzi wachoma moto shule ya Kibiti
na hamisa maganga

WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Kibiti iliyopo Mkoa wa Pwani, wameichoma moto shule hiyo na kusababisha uharibifu mkubwa wa majengo na mali za shule hiyo.

Kutokana na hali hiyo, serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, imeamua kuifunga shule hiyo kwa mwaka mmoja ili, pamoja na kuwasaka waliochochea vurugu hizo, kutoa nafasi ya kuifanyia ukarabati.

Hadi jana, moto ulikuwa ukiendelea kuteketeza moja ya bweni lililochomwa na wanafunzi hao, ambalo Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza, alisema limeteketea kabisa.

Mbali na bweni, wanafunzi hao waliokuwa na hasira, walichoma moto vyakula vilivyokuwa katika stoo kwa kutumia mafuta ya petroli ambayo haijulikani waliyatoa wapi. Pia waliingia katika maktaba ya shule na kuchoma moto vitabu vyote vilivyokuwamo. Waliharibu pia mfumo wa umeme shuleni hapo, huku wakitishia kuwaua walimu waliokuwa wakijaribu kuwazuia wasiendelee na vurugu hizo.

Vyakula vilivyochomwa moto ni pamaoja na sukari, unga na maharage. Inadaiwa kuwa asilimia kubwa ya waliofanya vurugu hizo kubwa ni wanafunzi wa kidato cha tatu ambao pamoja na mambo mengine, walikuwa wakilalamika kuwa na mwalimu dhaifu katika somo la fizikia.

Uamuzi wa kuifunga shule hiyo yenye wanafunzi 890, ulitangazwa jana jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri Mahiza, alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, makao makuu ya Wizara ya Elimu na Ufundi.

“Baada ya serikali kukaa chini na kutafakari vurugu hizo, imeamua kuifunga shule hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja na wanafunzi wote wanatakiwa kuwa wameondoka shuleni hapo ifikapo saa sita mchana wa leo (jana),” alisema Mahiza.

Kwa mujibu wa Mahiza, hatua hiyo itatoa mwanya kwa serikali kuifanyia matengenezo shule hiyo na kufanya tathmini ya hasara iliyotokana na vurugu hizo kubwa.

“Hadi sasa hatujui vurugu hizo zimesababisha hasara ya kiasi gani na kesho (leo) wataalamu wetu wanakwenda kutathmini gharama za mali iliyoharibiwa,” alisema.

Chanzo cha vurugu hizo ni malalamiko ya muda mrefu ya wanafunzi kuhusu ufundishaji usioridhisha wa baadhi ya walimu, akiwamo mwalimu wa fizikia kidato cha tatu, ukosefu wa maji safi na kutokuwepo kwa umeme wa uhakika.

Hadi jana, moto uliowashwa katika vurugu hizo ulikuwa ukiendelea kuteketeza moja ya mabweni ya shule hiyo kutokana na ukosefu wa maji ya kuuzima.

“Yako matatizo ya msingi katika shule zetu na madai ya wanafunzi wa Kibiti yalikuwa ya msingi, lakini walikosa uvumilivu. Matatizo hayo hayakuanza leo, yanatatuliwa kwa njia ya majadiliano sio kuharibu mali za shule,” alisema Mahiza.

Pamoja na hatua hiyo, Serikali imeiagiza Bodi ya Shule kukutana haraka na kubaini chanzo cha vurugu hizo na kuwataja wanafunzi wote waliohusika.

“Watakaobainika kuhusika sheria itachukua mkondo wake na watakaobainika kutohusika watatawanywa katika shule nyingine. Tukisha ikarabati shule hii iliyojengwa miaka 30 iliyopita kwa msaada wa serikali ya Cuba , hatutachukua tena wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne. Itakuwa na kidato cha tano na sita kwa sababu wanafunzi wa madarasa ya chini wamekuwa vinara katika vurugu,” alisema.

Shule hiyo iliyounganishiwa umeme wa jua mwaka jana kutokana na jenereta yake kuharibika, ilihitaji kufanyiwa ukarabati mkubwa uliohitaji zaidi ya Sh milioni 170, lakini serikali ikaahirisha ili kuifanyia ukarabati mwakani.

Naibu Waziri huyo pia alitumia fursa hiyo kuwaonya wanafunzi nchini kote kutojihusisha na vitendo vya uvunjifu wa amani na vurugu zinazosababisha uharibifu wa mali.

Sourse: Mtanzania ya leo
 
Nafikiri, kuribu mali ya shule na kuchoma kilichopo hata kidogo sio solution ya matatizo bali ni kuongezea, nafikiri umefika wakati ambao sasa vitendo vya aina hii vikemewe ili kujenga jamii inayothamini kidogo kilichopo, wangeweza kuchukua hatua nyingine nyingi zaidi ya kuchoma hadi vitabu library, this is terrible wakifungua watapata wapi vitabu japo kidogo.
 
haya... na waha wafukuzeni na muwafungie wasisome tena shule yeyote, na muwapeleke mahakamani....!@#$%#%^!&*#()....
 
Nafikiri, kuribu mali ya shule na kuchoma kilichopo hata kidogo sio solution ya matatizo bali ni kuongezea, nafikiri umefika wakati ambao sasa vitendo vya aina hii vikemewe ili kujenga jamii inayothamini kidogo kilichopo, wangeweza kuchukua hatua nyingine nyingi zaidi ya kuchoma hadi vitabu library, this is terrible wakifungua watapata wapi vitabu japo kidogo.

kwa watoto hii lugha haipo kabisa, ni jukumu lako wee mkuu wa shule uweze kudili na hawa watoto, fujo zao ni reflection ya upungufu wa akili wa mkuu wa shule unaopelekea kuwa na maamuzi mabaya.
 
tatizo la viongozi wetu ni maneno mengi tu bila vitendo.bora wamechoma ili ifanyiwe ukarabati kuliko kupokea ahadi tu kila kukicha.
kuna hili tatizo la usiri ktk utendaji ambalo ndio kikwazo,kwani linapotokea jambo ndio utasikia serikali inakuja na kusema tulikuwa tunataka kufanya hivi na vile.hii yote inatokana na kuwa na viongozi wasiokuwa na maamuzi.
Ninapendekeza yafuatayo;
1,shule ziwe na bajeti zao kwa maana ya kupewa mgao wao kwa mwaka wa fedha.
2,wizara kazi yao ni kusimamia na kuangalia utekelezaji unakwenda kama ulivyopangwa.
3,shule zipewe jukumu la kuajiri waalimu kutokana na mahitaji ilikuondoa tatizo la walimu,badala ya kusubiri wizara kuwapangia.
4,mipango ya shule iwe wazi kwa wadau wote ilikuondoa migongano ktk jamii husika
 
"Yako matatizo ya msingi katika shule zetu na madai ya wanafunzi wa Kibiti yalikuwa ya msingi, lakini walikosa uvumilivu. Matatizo hayo hayakuanza leo, yanatatuliwa kwa njia ya majadiliano sio kuharibu mali za shule," alisema Mahiza.

Sasa yalianza lini? na kwa nini hayatatuliwi? Na kama ni ya msingi kwa nini yasishughulikiwe haraka?

....hatutachukua tena wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne. Itakuwa na kidato cha tano na sita kwa sababu wanafunzi wa madarasa ya chini wamekuwa vinara katika vurugu," alisema.
Yale yale ya Tambaza, lakini kumbuka mkoa wa Pwani unaupungufu wa shule za sekondari si kama Dar.
 
Ndiyo haya haya yanayoendelea mpaka chuo kikuu. Palikuwa na tatizo gani kukaa na wanafunzi na kuwaeleza kinachokusudiwa kufanywa kuhusu kero zao? Na baada ya hapo kuhakikisha kuwa zinatatuliwa mapema iwezekanavyo? Kuondoa hivyo vidato vya chini ndiyo kweli vitamaliza tatizo? Nina hakika hao wa vidato vya juu wakiona hali inaendelea vile ilivyo na watetezi hawapo nao watafanya haya haya! Cha muhimu ni kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa hii migongano.
 
Hawa wanafunzi ni ajabu sana, inawezekanaje ukasahau kilichokupeleka pale shuleni? kweli umekwenda kufanya uharibifu ama?
 
Hawa wanafunzi ni ajabu sana, inawezekanaje ukasahau kilichokupeleka pale shuleni? kweli umekwenda kufanya uharibifu ama?

wanawaiga kaka zao wa UDSM. Kwa vile tunashangilia ya kule basi tushangilie na haya. Mimi naungana na uongozi wa UDSM kuwachukulia hatua kali wanafunzi wote waliofanya fujo za aina yeyote pale chuo kikuu mlimani ili iwe fundisho kwa wengine wote wanaodhani kudai haki kwa kufanya fujo ndio kupata haki. Wadoo zetu mjifunze kuwa na busara wakati wa kuelezea matatizo yenu. Hii jazba na hasira mnayoiinza mkiwa wadogo mtaiendeleza mkikua. Hime wazazi tujadiliane na watoto wetu umuhimu wa uvumilivu hasa wakati wa matatizo.
 
Usipoziba ufa utajenga ukuta.

Hii migomo isipotafutiwa ufumbuzi thabiti haitakomea kwa wanafunzi tu.
Matatizo ya msingi yatatuliwe mapema siyo kusubiri migomo ambayo inaingiza hasara hasa kwa fedha ya walipa kodi.

Baadaye watafuatia wafanyakazi wakiwamo wahadhiri wa vyuo vikuu, walimu wa sekondari na shule za misingi,watafuata wamiliki wa mabasi makubwa na daladala,watafuata wananchi waishio karibu na migodiya dhahabu na tanzanite na itafikia kwamba hao wanaodhibiti migomo nao watagoma(polisi,jeshi na vyombo vingine vya usalama) ndipo nchi haitakalika.Ndiko tunakoelekea kwa kuwa matatizo ya msingi hata kwa hao wana usalama wa Taifa itafikia nao hawatatuliwa kwa uchumi huu tulio nao sasa umepwaya.
 
sioni tatizo la kuwaumu wanafunzi,kwalichokifanya ndio upeo wao wa kuelewa.serikali ndio inalea matatizo yote haya na sisi tunabaki kunyoosheana vidole eti wanafunzi hawana adabu,huku ni kupotoka kimaono na kuona maisha ya mtanzania yahaitaji kilicho bora ila kwa viongozi tu.
 
Nafikiri SERIKALI lazima ijaribu kutatua migogoro ya wanafunzi kabla hali haijawa mbaya.Hivi karibuni wanafunzi mbalimbali wamefanya fujo,mfano
1.CHIDYA SEKONDARI
2.BAGAMOYO SEKONDARI
3.KIBITI SEKONDARI
4.UDSM
Wanafunzi sasa wanajua habari za MAFISADI wanaokula nchi na serikali imekaa chini inawaogopa wakati wao wanaendelea kupata tabu
Nafikiri SERIKALI isipoangalia wataendelea kufunga shule/vyuo na kufukuza wanafunzi lakini hiyo sio suluhisho
Watafute chanzo kwa nini wanafunzi wanafanya fujo ili waweze kuzizuia zisitokee
 
wanawaiga kaka zao wa UDSM. Kwa vile tunashangilia ya kule basi tushangilie na haya. Mimi naungana na uongozi wa UDSM kuwachukulia hatua kali wanafunzi wote waliofanya fujo za aina yeyote pale chuo kikuu mlimani ili iwe fundisho kwa wengine wote wanaodhani kudai haki kwa kufanya fujo ndio kupata haki. Wadoo zetu mjifunze kuwa na busara wakati wa kuelezea matatizo yenu. Hii jazba na hasira mnayoiinza mkiwa wadogo mtaiendeleza mkikua. Hime wazazi tujadiliane na watoto wetu umuhimu wa uvumilivu hasa wakati wa matatizo.

Wawe na busara gani tena? wameandika barua nyingi tu kwa uongozi wa chuo kuhusu madai yao na hayatatuliwi je, wakae nayo tu? Hivi unafikiri kwa nini watu hupigana vita duniani do you think hawana akili wote..NO..ni kwa sababu dulu za mazungumzo zimeshindikana. Actually adhabu kali si suluhisho...suluhisho ni kusolve matatizo yao.
 
“Yako matatizo ya msingi katika shule zetu na madai ya wanafunzi wa Kibiti yalikuwa ya msingi, lakini walikosa uvumilivu. Matatizo hayo hayakuanza leo, yanatatuliwa kwa njia ya majadiliano sio kuharibu mali za shule,” alisema Mahiza.

Kumbe Serikali inakiri kuwa Matatizo yao ni ya muda mrefu,sasa kwa nini walikuwa hawayatatui wanafanya nao mazungumzo gani hayo??

Wanafunzi sasa wanajua habari za MAFISADI wanaokula nchi na serikali imekaa chini inawaogopa wakati wao wanaendelea kupata tabu
Nafikiri SERIKALI isipoangalia wataendelea kufunga shule/vyuo na kufukuza wanafunzi lakini hiyo sio suluhisho
Watafute chanzo kwa nini wanafunzi wanafanya fujo ili waweze kuzizuia zisitokee

Wao siyo CUF wanaoendelea kuchezewa danadana kwenye kusaini Muafaka, kila siku mazungumzo-mazungumzo..wale ni wasomi pevu na wala siyo watoto wadogo...nadhani kilichochangia zaidi ni hiyo hali ya kuibuka kwa Mijizi ambayo kila pesa inapotajwa, inakuwa ni Mipesa, EPA, BOT, Chenge, mara Yona wakati nyie mnaambiwa mazungumzo. we utaacha kuwa na hasira kweli.

Hii italeta ushawishi kwa Serikali kuwa inatimiza kile ilichokiahidi kwa wakati. Ooh! Serikali haina pesa, mpaka mwaka ujao wa fedha 2009/2010. Za kupeleka kwenye Mabenki ya Ulaya zipo.

Naunga mkono hoja!
 
tatizo la viongozi wetu ni maneno mengi tu bila vitendo.bora wamechoma ili ifanyiwe ukarabati kuliko kupokea ahadi tu kila kukicha.
kuna hili tatizo la usiri ktk utendaji ambalo ndio kikwazo,kwani linapotokea jambo ndio utasikia serikali inakuja na kusema tulikuwa tunataka kufanya hivi na vile.hii yote inatokana na kuwa na viongozi wasiokuwa na maamuzi.
Ninapendekeza yafuatayo;
1,shule ziwe na bajeti zao kwa maana ya kupewa mgao wao kwa mwaka wa fedha.
2,wizara kazi yao ni kusimamia na kuangalia utekelezaji unakwenda kama ulivyopangwa.
3,shule zipewe jukumu la kuajiri waalimu kutokana na mahitaji ilikuondoa tatizo la walimu,badala ya kusubiri wizara kuwapangia.
4,mipango ya shule iwe wazi kwa wadau wote ilikuondoa migongano ktk jamii husika

Serikali ya ccm imeshindwa kufanya chochote katika nchi hii na haya ni matokeo yake.
 
wanawaiga kaka zao wa UDSM. Kwa vile tunashangilia ya kule basi tushangilie na haya. Mimi naungana na uongozi wa UDSM kuwachukulia hatua kali wanafunzi wote waliofanya fujo za aina yeyote pale chuo kikuu mlimani ili iwe fundisho kwa wengine wote wanaodhani kudai haki kwa kufanya fujo ndio kupata haki. Wadoo zetu mjifunze kuwa na busara wakati wa kuelezea matatizo yenu. Hii jazba na hasira mnayoiinza mkiwa wadogo mtaiendeleza mkikua. Hime wazazi tujadiliane na watoto wetu umuhimu wa uvumilivu hasa wakati wa matatizo.

Wewe ndiye kichwa mgando kweli kweli. haki ya wananchi huwa haingoji kesho. Ukiona haki yako inapotea basi unadai papo hapo bila kuchelewa.
 
kaka Mgaya, punguza hasira, watu tunapishana uelewa kutokana na makuzi, elimu na taaluma.Mhandisi lugha yake ni tofauti na Doctor, pia Mchungaji/ Shekh lugha yake ni tofauti na Wanasiasa

Inaonyesha wewe ulicheza Skauti ama Mgambo, Maana hukawii kumpa mtu adhabu! Isije ikawa jana ndiyo ulirejea kutokea Comoro, kama ni hivyo karibu nyumbani

Wewe ndiye kichwa mgando kweli kweli. haki ya wananchi huwa haingoji kesho. Ukiona haki yako inapotea basi unadai papo hapo bila kuchelewa.

Jaribu kutoa elimu zaidi iliaelewe
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom