Kibiti, Pwani: Majambazi yaua Askari Polisi NANE(8)

Wanajesh wa tz walipofika Uganda wakati ule wa vita walipewa maji ya kunywa na chakula na wenyeji kisa ni lile tumaini kwamba nduli idd amin atang'olewa hivyo wanajesh watz walikuwa kama wakomboz wao vivyo hivyo hapa kwetu tz askari ndiyo ulinzi wetu lakini watu wanatekwa, wanateswa, wanapotea, miili inaokotwa imefungwa sandarusi na imewekewa mawe jeshi la polisi linasema halijahusika mbaya hata upelekez hawafanyi akati ni wajibu wao hivyo mtu akisikia polisi kapigwa risasi ukizingatia haohao ndo wamesema hawajui miili iliyookotwa ni akina nani nakwambia hata ukiwakemea watu wasifurahie kuuawa kwa polisi watanyamaza midomon ila siyo mioyoni hivyo msishangae watu kufurahia uvamizi dhidi ya polisi kwani ni mrejesho wa yale yanayotokea! Ukisema polisi akiuawa usalama wetu upo hatarini ni sawa lakini pia ukumbuke kuwa hata pokisi wasipo uawa bado hatupo salama ukitaka kujua hilo mtafute Dr. Ulimboka, Absalom Kibanda, Kondo tutindaga, kubenea, mwakyembe, saanane just to mention few, pamoja na kuwa wakati utesaji, utekaji unafanyika dhidi yao polisi walikuwa salama salmini lakini raia hawa wasio na hatia hawakuwa salama
 
Hii ni habari ya kusikitisha sana na ni matumaini yangu hata huko Bungeni watatumia mjadala kuzungumzia hili. Huko Mkuranga hii si habari ya kwanza kuhusiana na mauaji ya polisi kama ninavyokumbuka. Nini kinaendelea? Hawa ni mashujaa na Taifa linahitaji kuwaenzi ipasavyo pamoja na familia zao. Lakini pia ni muhimu sana kwa viongozi wa jeshi kuangalia ni namna gani baadhi ya mambo kama haya yanaweza kufanywa kwani kama kumbukumbu yangu inanijia vizuri aina hii imewahi kutokea tena huko nyuma ambapo wanaodhaniwa kuwa ni majambazi waliwategea polisi wakiwa wanabadilishana lindo
Mbona kutekwa wamekataa kujadili na huku si kutekwa wakauawa, isijadiliwe pia
 
Habari zilizotufikia hivi punde, zimeeleza kuwa, askari polisi watatu wameuawa na majambazi huko Mkuranga, Mkoani Pwani.

Habari hizo zinasema kuwa, askari hao wameuawa kwa kupigwa risasi na majambazi hao wakati wakijiandaa kuondoka kwenye lindo ambalo lilikuwa ni kizuizi cha barabarani ili warudi kituoni.

Imeelezwa kwamba majambazi hao waliwavamia ghafla polisi hao waliokuwa kwenye gari na kuwapiga risasi na kuwaua wote palepale eneo la tukio, kisha kutokomea kusikojulikana.

Global Publishers Twitter Page
:::::::::::::::::::::::::::::::::>>>>>
Mkuranga,Vikindu na Kibiti usalama wake haupo sawa.
Pole kwa wafiwa
Hiyo ni Bungu, mpaka sasa hakuna gari inayotebea. Kule hakufai ingawa kuna ulinzi mkali sana
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Habari zilizotufikia hivi punde, zimeeleza kuwa, Askari Polisi watatu wameuawa na majambazi huko Mkuranga, Mkoani Pwani.

Habari hizo zinasema kuwa, askari hao wameuawa kwa kupigwa risasi na majambazi wakati wakijiandaa kuondoka kwenye lindo ambalo lilikuwa ni kizuizi cha barabarani ili warudi kituoni.

Imeelezwa kwamba majambazi hao waliwavamia ghafla polisi hao waliokuwa kwenye gari na kuwapiga risasi na kuwaua wote palepale eneo la tukio, kisha kutokomea kusikojulikana.
 
Kwanza nitoe pole kwa familia za watanzania wenzetu ambao wamepoteza maisha wakiwa ktk kazi ya kutulinda.

Pili, usalama wa nchi unatokana na mwananchi mwenyewe na sio polisi au usalama. Kwakuwa hao wote wanapewa taarifa na wananchi/raia wema. Kwahio wananchi hatuna budi kuwaunga mkono.

Tatu, siasa zisitumike kutugawa ikiwa ni pamoja na kukebehi au kutoa dhihaka dhidi ya viongozi wetu wa serikali.

Nne, tusifurahie matatizo hasa yanapowapata walinzi wetu wa amani. Ukimuona mtu anashangilia kwa kuuawa askari wakiwa ktk kazi ya kuimarisha ulinzi basi huyo ni adui yetu. Kwa pamoja tuseme poleni wafiwa na pole jeshi la polisi
 
Wiki iliyopita nilishuhudia polisi wakiwapiga watu pale Mwenge, iliniuma sana
Waliwapiga wale wadada kama si wanadamu
Wao yakiwakuta sisi twawaonea huruma ila wao hawatuonei huruma pale tukoseapo
Yoyote anaefanyiwa kile kitendo huwa anawachukia sana hawa polisi wetu.
Ndio maana unaweza sikia polisi kafa na watu wakafurahia hii yote ni sababu ya tabia zao za kuonea watu, kusurubisha watu

Omba wasikukamate kwenye anga zao, utajuta kuwa hai

Ila polisi nao wajiulize kwanini wafanyiwe hivo
 
Polisi saba ni wengi sana kwenye ambush kupotea pamoja. Ila timing.

Jeshi la polisi limepoteza nguvu kazi kubwa sana, na sisi raia tumepoteza sehemu kubwa zaidi ya ulinzi. Karibu raia 7500-8000 wamepoteza ulinzi. Dah inaumiza sana. Why Mkuranga tu?

Ila hata kwenye uzinduzi wa SG niliona ulinzi tight sana zile outer ring za SS, it seems hali ya usalama pande hizo inajulikana. Iko kwenye alarming rate. Sijui wanasubiri nini...
 
Back
Top Bottom