RaiaMbishi
JF-Expert Member
- Jan 18, 2012
- 252
- 134
Mwaka 2009, Kibanda wakati ule akiwa mhariri mtendaji wa gazeti la Tanzania Daima alianzisha mfululizo wa makala zenye kichwa kisemacho - Tuendako: Sio Ufisadi, Ni Urais 2015. Katika makala hizo, Kibanda alishambulia sana mtandao uliomwingiza Kikwete madarakani. Makala hizi zilileta mtikisiko mkubwa sana kwa walengwa hali ambayo iliweka maisha ya Kibanda hatarini lakini kilichokuwa kinamlinda Kibanda ni uwepo wake kwenye gazeti linalomilikiwa na mmoja wa viongozi wa Chadema (Freeman Mbowe, suala ambalo lilifanya iwe vigumu kwa mtu yoyote wa CCM kumdhuru Kibanda bila ya kuchafua hali ya hewa ambatyo ingepelekea CCM kudhoofika na Chadema kuzidi kupanda chati.
Ni makala hizi ndio zimemletea matatizo, na nina uhakika kwamba kwa vile vile mwenyezi mungu amemuokoa na umauti, siku atakapopata nafuu na kuamua kufunguka, atakuja kuthibitisha uhusiano wa makala zake hizi na janga lililompata. Ni muhimu kwa vyombo vya usalama kuunganisha makala hizi na ujasusi aliofanyiwa Kibanda, la sivyo itakuwa ni michezo ya kuigiza. Zifuatazo ni mfululizo wa makala husika - msomaji, kuwa makini zaidi na sehemu zilizopigwa rangi nyekundu.
-------------------------------------------------------------------------------------
Makala ya Kwanza
[TABLE="width: 915"]
[TR]
[TD][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]
Tuendako: Si ufisadi, ni urais 2015
Absalom Kibanda
Jumatano, 8 Aprili 2009[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]MAMBO ya ajabu na yanayostaajabisha yameanza kujitokeza katika nchi hii, katika siku na miezi ya hivi karibuni, kiasi cha kusababisha kuzuka kwa maswali mengi yasiyo na majibu.
Matukio ya hivi karibuni kabisa kisiasa yanayojumuisha kauli za kitatanishi zilizotolewa na wenyeviti wastaafu wa mikoa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kabla ya hapo matamshi makali ya Makamu Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho tawala, John Malecela, yanaonyesha dhahiri kwamba, kuna kasoro kubwa katika mwenendo mzima wa kiuongozi hapa nchini.
Kwa maneno rahisi kabisa, kitendo cha wazee hao wa CCM kujitokeza hadharani na kuchomeka hoja za kumtetea na kumsafishia njia Rais Jakaya Kikwete wakati wa kinyang'anyiro cha urais mwakani, ni kielelezo cha wazi cha kuwapo kwa tatizo kubwa zaidi nyuma ya kauli za wazee hao.
Ingawa ni kweli kwamba kauli za namna hii za kumsafishia njia Kikwete zilishapata kutolewa kabla ya hapo na watu wengine kadhaa wazito, akiwamo mfanyabiashara maarufu, Reginald Mengi na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, bado kuibuka kwake upya na tena kwa nguvu kubwa kunaweza kuashiria dalili za kuwapo kwa hali ya kukata tamaa katika jamii.
Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, wazee hawa wa CCM na watu wengine mashuhuri wa kabla yao na pengine wengine watakaoibuka baada yao, wanajitokeza leo, wakati dalili zimeshaanza kujionyesha wazi kwamba, ile hatari iliyokuwa ikimnyemelea Kikwete miezi au zaidi ya mwaka mmoja uliopita ya kumfanya awe rais wa kwanza ndani ya CCM kuongoza kwa muhula mmoja tu, ikiwa imeshaanza kutoweka.
Wasomaji wa safu hii ni mashahidi wazuri kwamba, miezi kadhaa kabla ya azimio hilo lisilo rasmi la kuibuka kwa kutumwa kwa wazee hao, limekuja wakati tayari nikiwa mmoja miongoni mwa wadadisi wa mambo ambao nilieleza bayana kuhusu uhakika wa Kikwete kushinda kwa mara nyingine tena urais kwa muhula wa pili wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwakani.
Hata hivyo, napenda kueleza mapema kabisa kwamba, matukio yaliyosababisha kufunguka upya kwa njia ya Kikwete kuendelea na awamu yake ya pili ya utawala wake hakujasababishwa au kuchagizwa kwa namna yoyote ile na hatua zozote makini za kimaamuzi au za kiutawala alizochukua, bali matakwa na mahitaji, kama si nusura ya kimazingira yanayolikabili taifa kwa hivi sasa.
Kwa upande mwingine, naweza kusema pasipo shaka kwamba, nusura ya Kikwete ya kuondoka madarakani mwaka 2010 kwa kiwango kikubwa imechagizwa na kuyeyuka kwa namna isiyo na maelezo fasaha kwa upinzani dhidi yake ndani ya chama chake na nje ya CCM.
Wafuatiliaji wazuri wa siasa za nchi hii wanaweza wakawa mashahidi wazuri kwamba, kusambaratika kwa genge haramu la mtandao ndani ya CCM ambalo lilipigana kufa na kupona kuhakikisha Kikwete anashinda uteuzi na hatimaye urais mwaka 2005 likicheza rafu mbaya na za hatari kwa kiwango cha kutishia mustakabali wa umoja na mshikamano wetu kitaifa, ilikuwa ni dalili ya kwanza iliyoanza pole pole kumjengea msingi wa ushindi kiongozi huyo.
Msambaratiko huu ambao leo hii umewaweka katika kundi moja wana mtandao wa aina ya Edward Lowassa, Andrew Chenge, Rostam Aziz, Nazir Karamagi na wenzao wengine huku ukiwatenganisha na kuwakosanisha maswahiba wao wa zama zile wa aina ya, Samuel Sitta na Bernard Membe, kwa kiasi kikubwa ulimtenganisha Rais Kikwete na madhambi yote ya mtandao, ambao ulijenga maadui wengi ndani na nje ya CCM.
Kumeguka kwa genge hilo kulisababisha wana CCM wengine ambao awali hawakuwa sehemu ya wanamtandao kujikuta ama wakishikamana na kundi la kwanza na wengine wakajikuta wakiungana na kuunda mtandao mpya na kundi jingine jipya.
Katika mparaganyiko huu, Lowassa, Rostam, Karamagi na wenzao wakajikuta wakiwa majeruhi wa kwanza wa hali hii ambayo kwa upande mwingine iliwapandisha chati na kuwajengea ushujaa wana mtandao wenzao wachache wa aina ya Sitta na Membe.
Ufa huu wa kwanza uliomuacha Kikwete akiwa shuhuda, uliwaunganisha katika kundi moja kina Sitta na Membe na wanasiasa wenzao kadhaa ndani ya CCM wa aina ya Dk. Harrison Mwakyembe, Anne Kilango Malecela, William Shellukindo, Lucas Selellii, Christopher ole Sendeka na wenzao wengine wengi ambao leo wanajitambulisha na kutambulika kijamii kuwa wanaharakati wa vita dhidi ya ufisadi.
Kuundwa kwa kundi hili jipya ambalo lilijipatia nguvu kubwa kuanzia Februari mwaka jana kulifanikisha azima ya kiharakati ya CCM ya kuzima mapambano dhidi ya ufisadi yaliyokuwa yameanzishwa na kambi ya upinzani ndani ya Bunge yaliyokuwa yakiongozwa na kina Hamad Rashid Mohammed, Wilbrod Slaa, Zitto Kabwe, Halima Mdee, Habib Mnyaa na wenzao wengine wengi.
Kuibuka kwa mwelekeo huo mpya wa mambo ndiko ambako wakati fulani kupitia katika safu hii nilikuelezea kuwa ni hatua mahususi ya makada wa CCM kuiteka nyara vita takatifu ya ufisadi kutoka katika himaya ya wapinzani na kuifanya ichukue sura tofauti na iliyoiweka chini ya himaya ya chama hicho tawala. Hii ilikuwa ni salama ya tatu ya Rais Kikwete.
Tukio la hivi majuzi la Serikali ya Marekani kumpa tuzo ya mwanamke jasiri, Mama Kilango, kwa namna alivyoweza kukabiliana na vitendo vya ufisadi, ni ushahidi mmojawapo na wa wazi wa namna CCM ilivyofanikiwa kuizima ndoto ya mafanikio ya kambi ya upinzani waliyojijengea miaka miwili ya mwanzo ya utawala wa Kikwete, ambayo ilianza kutoa dalili za kumfanya aonekane kuwa ni rais wa awamu moja tu.
Mafanikio haya ya awali ya kuwapora wapinzani turufu moja nzuri ya kisiasa dhidi ya chama tawala ndani ya Bunge, iliwawezesha makada mashujaa wa ndani ya CCM waanze kuimarisha msingi imara wa kujipanga kwa ajili ya safari ya kumrithi Rais Kikwete wakati atakapomaliza muhula wake wa uongozi.
Mtandao huu mpya wa ‘mashujaa' wa CCM, kwa umakini mkubwa walifanikisha azima yao ya kumtenganisha kikazi na kiharakati Kikwete na maswahiba wake wakuu wawili, Lowassa na Rostam, wakianza kwa kujijengea uhalali wa kimaadili machoni mwa wanachama wenzao wa chama tawala na kisha jamii kwa ujumla, kabla ya kubuni mbinu mbalimbali za kulainisha moyo wa rais na watendaji wengine wa serikali uwaelekee wao. Hii ilikuwa hatua ya nne ya kumjengea JK uhalali ulioanza kutokomea.
Mtandao huo mpya wa mashujaa wa ufisadi, ambao ulijumuisha watu waliokuwa wakijua mbinu za chini chini za kujijenga na kujilinda wakati wanapotaka kufanikisha ajenda zao za kimamlaka, ulilazimika kuongeza juhudi za kujiweka karibu zaidi ya Kikwete na serikali yake, baada ya kuanza kuona kuwapo kwa dalili za tishio la wazi na la siri kutoka katika kundi la majeruhi wa kisiasa wa ndani ya CCM, ambao kwa bahati mbaya walikuwa wakionekana kuwa ni watu wenye nguvu kubwa za kiuchumi.
Huku wakitambua ukweli huo, ajenda dhidi ya ufisadi iliyobebwa juu juu na kina Sitta, Membe, Kilango, Sendeka, Mwakyembe na wenzao ikajikuta ikipata baraka za kuungwa mkono waziwazi na mfanyabiashara maarufu anayemiliki mtandao wa vyombo vya habari, Reginald Mengi.
Ubia huo wa kiajenda kati ya mashujaa hao wa ufisadi wa ndani ya Bunge na mfanyabiashara huyo ulikuwa ni pigo baya zaidi kwa kundi la majeruhi wa vita ya ufisadi, kutokana na nguvu kubwa ya kihabari waliyoanza kujijengea kina Sitta, Kilango, Sendeka, Sellelii na wenzao wengine wa mtandao huo mpya.
Wafuatiliaji wazuri wa habari na makala katika magazeti, televisheni na redio wanaweza wakawa mashahidi wazuri wa namna habari zinazowahusu kina Sitta, Sendeka, Kilango, Shellukindo, Sellelii na wenzao wengine wengi zilivyoanza kuripotiwa kwa namna ya kuwabainisha kuwa wanaharakati wazuri wa vita dhidi ya ufisadi.
Wakati hayo yakiendelea, kwa bahati mbaya sana, vita takatifu ya ufisadi iliyoanzia katika vyombo vya habari kabla ya kuingizwa bungeni na wabunge wa upinzani kabla ya kutekwa nyara na kupindishwa na ‘mashujaa' hao wa CCM ikaanza taratibu kugeuka na kuchukua mkondo tofauti kabisa na ule uliolenga kuubomoa kabisa mfumo wa kifisadi uliojistawisha ndani ya serikali kupitia katika chama tawala.
Haraka haraka, mashujaa hao feki wa CCM wakafanikiwa kukisafisha chama chao na kumuepusha kabisa rais na viongozi wengine wa juu wa chama hicho katika tuhuma za kifisadi na kulifanya suala hilo lianze kuonekana kuwa ni matendo binafsi ya kikundi cha watu wachache walafi ambao waliamua kutumia fursa zao za kimamlaka kujinufaisha wao wenyewe.
Hali ilipofikia hatua hiyo, ndipo ghafla taifa likashuhudia watuhumiwa kadhaa wakifikishwa mahakamani wakihusishwa na vitendo vya ufisadi kupitia kashfa ya wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), Alex Stewarts, na kisha Richmond. Hiyo ilikuwa hatua ya tano iliyosaidia kuisafisha nyota ya Kikwete iliyoanza kufifia.
Wakati haya yote yakitendeka, leo hii taratibu, siri imeanza kufichuka kwamba, nyuma ya pazia, baadhi au majemedari wote wa mtandao mpya wa vita dhidi ya ufisadi, walikuwa wameamua kuyatumia mapambano haya kama mbinu mahususi ya kuzima kile kilichoanza kuonekana kuwa ni dalili za wazi za kumuandaa Lowassa kuwa mrithi wa Kikwete ama mwaka 2010 au 2015.
Kufichuka kwa siri hii ambayo wanasiasa wengi wa ndani ya CCM hawataki kuiweka wazi, kumesababisha ghafla majna ya watu wanaotajwa kuingia katika orodha hiyo ya urais kuongezeka kila kukicha, ikiwataja Membe, Masha, Mengi, Lowassa, Nchimbi na wengine wengi ama kwa kupotosha lengo na wakati mwingine kubainisha ukweli.
Tukutane wiki ijayo wakati tutakapoanza kufichua siri hizi hatua kwa hatua.[/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]-----------------------------------------------------------------
makala hii pia inapatikana katika tovuti ifuatayo:
Si ufisadi, ni urais 2015[/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Ni makala hizi ndio zimemletea matatizo, na nina uhakika kwamba kwa vile vile mwenyezi mungu amemuokoa na umauti, siku atakapopata nafuu na kuamua kufunguka, atakuja kuthibitisha uhusiano wa makala zake hizi na janga lililompata. Ni muhimu kwa vyombo vya usalama kuunganisha makala hizi na ujasusi aliofanyiwa Kibanda, la sivyo itakuwa ni michezo ya kuigiza. Zifuatazo ni mfululizo wa makala husika - msomaji, kuwa makini zaidi na sehemu zilizopigwa rangi nyekundu.
-------------------------------------------------------------------------------------
Makala ya Kwanza
[TR]
[TD][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]
Tuendako: Si ufisadi, ni urais 2015
Absalom Kibanda
Jumatano, 8 Aprili 2009[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]MAMBO ya ajabu na yanayostaajabisha yameanza kujitokeza katika nchi hii, katika siku na miezi ya hivi karibuni, kiasi cha kusababisha kuzuka kwa maswali mengi yasiyo na majibu.
Matukio ya hivi karibuni kabisa kisiasa yanayojumuisha kauli za kitatanishi zilizotolewa na wenyeviti wastaafu wa mikoa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kabla ya hapo matamshi makali ya Makamu Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho tawala, John Malecela, yanaonyesha dhahiri kwamba, kuna kasoro kubwa katika mwenendo mzima wa kiuongozi hapa nchini.
Kwa maneno rahisi kabisa, kitendo cha wazee hao wa CCM kujitokeza hadharani na kuchomeka hoja za kumtetea na kumsafishia njia Rais Jakaya Kikwete wakati wa kinyang'anyiro cha urais mwakani, ni kielelezo cha wazi cha kuwapo kwa tatizo kubwa zaidi nyuma ya kauli za wazee hao.
Ingawa ni kweli kwamba kauli za namna hii za kumsafishia njia Kikwete zilishapata kutolewa kabla ya hapo na watu wengine kadhaa wazito, akiwamo mfanyabiashara maarufu, Reginald Mengi na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, bado kuibuka kwake upya na tena kwa nguvu kubwa kunaweza kuashiria dalili za kuwapo kwa hali ya kukata tamaa katika jamii.
Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, wazee hawa wa CCM na watu wengine mashuhuri wa kabla yao na pengine wengine watakaoibuka baada yao, wanajitokeza leo, wakati dalili zimeshaanza kujionyesha wazi kwamba, ile hatari iliyokuwa ikimnyemelea Kikwete miezi au zaidi ya mwaka mmoja uliopita ya kumfanya awe rais wa kwanza ndani ya CCM kuongoza kwa muhula mmoja tu, ikiwa imeshaanza kutoweka.
Wasomaji wa safu hii ni mashahidi wazuri kwamba, miezi kadhaa kabla ya azimio hilo lisilo rasmi la kuibuka kwa kutumwa kwa wazee hao, limekuja wakati tayari nikiwa mmoja miongoni mwa wadadisi wa mambo ambao nilieleza bayana kuhusu uhakika wa Kikwete kushinda kwa mara nyingine tena urais kwa muhula wa pili wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwakani.
Hata hivyo, napenda kueleza mapema kabisa kwamba, matukio yaliyosababisha kufunguka upya kwa njia ya Kikwete kuendelea na awamu yake ya pili ya utawala wake hakujasababishwa au kuchagizwa kwa namna yoyote ile na hatua zozote makini za kimaamuzi au za kiutawala alizochukua, bali matakwa na mahitaji, kama si nusura ya kimazingira yanayolikabili taifa kwa hivi sasa.
Kwa upande mwingine, naweza kusema pasipo shaka kwamba, nusura ya Kikwete ya kuondoka madarakani mwaka 2010 kwa kiwango kikubwa imechagizwa na kuyeyuka kwa namna isiyo na maelezo fasaha kwa upinzani dhidi yake ndani ya chama chake na nje ya CCM.
Wafuatiliaji wazuri wa siasa za nchi hii wanaweza wakawa mashahidi wazuri kwamba, kusambaratika kwa genge haramu la mtandao ndani ya CCM ambalo lilipigana kufa na kupona kuhakikisha Kikwete anashinda uteuzi na hatimaye urais mwaka 2005 likicheza rafu mbaya na za hatari kwa kiwango cha kutishia mustakabali wa umoja na mshikamano wetu kitaifa, ilikuwa ni dalili ya kwanza iliyoanza pole pole kumjengea msingi wa ushindi kiongozi huyo.
Msambaratiko huu ambao leo hii umewaweka katika kundi moja wana mtandao wa aina ya Edward Lowassa, Andrew Chenge, Rostam Aziz, Nazir Karamagi na wenzao wengine huku ukiwatenganisha na kuwakosanisha maswahiba wao wa zama zile wa aina ya, Samuel Sitta na Bernard Membe, kwa kiasi kikubwa ulimtenganisha Rais Kikwete na madhambi yote ya mtandao, ambao ulijenga maadui wengi ndani na nje ya CCM.
Kumeguka kwa genge hilo kulisababisha wana CCM wengine ambao awali hawakuwa sehemu ya wanamtandao kujikuta ama wakishikamana na kundi la kwanza na wengine wakajikuta wakiungana na kuunda mtandao mpya na kundi jingine jipya.
Katika mparaganyiko huu, Lowassa, Rostam, Karamagi na wenzao wakajikuta wakiwa majeruhi wa kwanza wa hali hii ambayo kwa upande mwingine iliwapandisha chati na kuwajengea ushujaa wana mtandao wenzao wachache wa aina ya Sitta na Membe.
Ufa huu wa kwanza uliomuacha Kikwete akiwa shuhuda, uliwaunganisha katika kundi moja kina Sitta na Membe na wanasiasa wenzao kadhaa ndani ya CCM wa aina ya Dk. Harrison Mwakyembe, Anne Kilango Malecela, William Shellukindo, Lucas Selellii, Christopher ole Sendeka na wenzao wengine wengi ambao leo wanajitambulisha na kutambulika kijamii kuwa wanaharakati wa vita dhidi ya ufisadi.
Kuundwa kwa kundi hili jipya ambalo lilijipatia nguvu kubwa kuanzia Februari mwaka jana kulifanikisha azima ya kiharakati ya CCM ya kuzima mapambano dhidi ya ufisadi yaliyokuwa yameanzishwa na kambi ya upinzani ndani ya Bunge yaliyokuwa yakiongozwa na kina Hamad Rashid Mohammed, Wilbrod Slaa, Zitto Kabwe, Halima Mdee, Habib Mnyaa na wenzao wengine wengi.
Kuibuka kwa mwelekeo huo mpya wa mambo ndiko ambako wakati fulani kupitia katika safu hii nilikuelezea kuwa ni hatua mahususi ya makada wa CCM kuiteka nyara vita takatifu ya ufisadi kutoka katika himaya ya wapinzani na kuifanya ichukue sura tofauti na iliyoiweka chini ya himaya ya chama hicho tawala. Hii ilikuwa ni salama ya tatu ya Rais Kikwete.
Tukio la hivi majuzi la Serikali ya Marekani kumpa tuzo ya mwanamke jasiri, Mama Kilango, kwa namna alivyoweza kukabiliana na vitendo vya ufisadi, ni ushahidi mmojawapo na wa wazi wa namna CCM ilivyofanikiwa kuizima ndoto ya mafanikio ya kambi ya upinzani waliyojijengea miaka miwili ya mwanzo ya utawala wa Kikwete, ambayo ilianza kutoa dalili za kumfanya aonekane kuwa ni rais wa awamu moja tu.
Mafanikio haya ya awali ya kuwapora wapinzani turufu moja nzuri ya kisiasa dhidi ya chama tawala ndani ya Bunge, iliwawezesha makada mashujaa wa ndani ya CCM waanze kuimarisha msingi imara wa kujipanga kwa ajili ya safari ya kumrithi Rais Kikwete wakati atakapomaliza muhula wake wa uongozi.
Mtandao huu mpya wa ‘mashujaa' wa CCM, kwa umakini mkubwa walifanikisha azima yao ya kumtenganisha kikazi na kiharakati Kikwete na maswahiba wake wakuu wawili, Lowassa na Rostam, wakianza kwa kujijengea uhalali wa kimaadili machoni mwa wanachama wenzao wa chama tawala na kisha jamii kwa ujumla, kabla ya kubuni mbinu mbalimbali za kulainisha moyo wa rais na watendaji wengine wa serikali uwaelekee wao. Hii ilikuwa hatua ya nne ya kumjengea JK uhalali ulioanza kutokomea.
Mtandao huo mpya wa mashujaa wa ufisadi, ambao ulijumuisha watu waliokuwa wakijua mbinu za chini chini za kujijenga na kujilinda wakati wanapotaka kufanikisha ajenda zao za kimamlaka, ulilazimika kuongeza juhudi za kujiweka karibu zaidi ya Kikwete na serikali yake, baada ya kuanza kuona kuwapo kwa dalili za tishio la wazi na la siri kutoka katika kundi la majeruhi wa kisiasa wa ndani ya CCM, ambao kwa bahati mbaya walikuwa wakionekana kuwa ni watu wenye nguvu kubwa za kiuchumi.
Huku wakitambua ukweli huo, ajenda dhidi ya ufisadi iliyobebwa juu juu na kina Sitta, Membe, Kilango, Sendeka, Mwakyembe na wenzao ikajikuta ikipata baraka za kuungwa mkono waziwazi na mfanyabiashara maarufu anayemiliki mtandao wa vyombo vya habari, Reginald Mengi.
Ubia huo wa kiajenda kati ya mashujaa hao wa ufisadi wa ndani ya Bunge na mfanyabiashara huyo ulikuwa ni pigo baya zaidi kwa kundi la majeruhi wa vita ya ufisadi, kutokana na nguvu kubwa ya kihabari waliyoanza kujijengea kina Sitta, Kilango, Sendeka, Sellelii na wenzao wengine wa mtandao huo mpya.
Wafuatiliaji wazuri wa habari na makala katika magazeti, televisheni na redio wanaweza wakawa mashahidi wazuri wa namna habari zinazowahusu kina Sitta, Sendeka, Kilango, Shellukindo, Sellelii na wenzao wengine wengi zilivyoanza kuripotiwa kwa namna ya kuwabainisha kuwa wanaharakati wazuri wa vita dhidi ya ufisadi.
Wakati hayo yakiendelea, kwa bahati mbaya sana, vita takatifu ya ufisadi iliyoanzia katika vyombo vya habari kabla ya kuingizwa bungeni na wabunge wa upinzani kabla ya kutekwa nyara na kupindishwa na ‘mashujaa' hao wa CCM ikaanza taratibu kugeuka na kuchukua mkondo tofauti kabisa na ule uliolenga kuubomoa kabisa mfumo wa kifisadi uliojistawisha ndani ya serikali kupitia katika chama tawala.
Haraka haraka, mashujaa hao feki wa CCM wakafanikiwa kukisafisha chama chao na kumuepusha kabisa rais na viongozi wengine wa juu wa chama hicho katika tuhuma za kifisadi na kulifanya suala hilo lianze kuonekana kuwa ni matendo binafsi ya kikundi cha watu wachache walafi ambao waliamua kutumia fursa zao za kimamlaka kujinufaisha wao wenyewe.
Hali ilipofikia hatua hiyo, ndipo ghafla taifa likashuhudia watuhumiwa kadhaa wakifikishwa mahakamani wakihusishwa na vitendo vya ufisadi kupitia kashfa ya wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), Alex Stewarts, na kisha Richmond. Hiyo ilikuwa hatua ya tano iliyosaidia kuisafisha nyota ya Kikwete iliyoanza kufifia.
Wakati haya yote yakitendeka, leo hii taratibu, siri imeanza kufichuka kwamba, nyuma ya pazia, baadhi au majemedari wote wa mtandao mpya wa vita dhidi ya ufisadi, walikuwa wameamua kuyatumia mapambano haya kama mbinu mahususi ya kuzima kile kilichoanza kuonekana kuwa ni dalili za wazi za kumuandaa Lowassa kuwa mrithi wa Kikwete ama mwaka 2010 au 2015.
Kufichuka kwa siri hii ambayo wanasiasa wengi wa ndani ya CCM hawataki kuiweka wazi, kumesababisha ghafla majna ya watu wanaotajwa kuingia katika orodha hiyo ya urais kuongezeka kila kukicha, ikiwataja Membe, Masha, Mengi, Lowassa, Nchimbi na wengine wengi ama kwa kupotosha lengo na wakati mwingine kubainisha ukweli.
Tukutane wiki ijayo wakati tutakapoanza kufichua siri hizi hatua kwa hatua.[/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]-----------------------------------------------------------------
makala hii pia inapatikana katika tovuti ifuatayo:
Si ufisadi, ni urais 2015[/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]