jamii01
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 1,988
- 1,437
MWENYEKITI wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Absalom Kibanda amewasili nchini Tanzania akitokea nchini Afrika Kusini alipokuwa amekwenda kwa matibabu baada kuvamia na kutekwa kisha kufanyiwa unyama wa kutisha.
Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006) Ltd, alifanyiwa unyama huo Usiku wa Februari 25, mwaka huu majira ya saa 09:00 usiku, Kibanda alivamiwa na watu walioingia kwenye uzio wa nyumba yao wakavunja kioo cha gari analotumia, lakini kioo kilipovunjwa alarm ilipiga kelele, Kibanda akatoka nje na watu hao wakakimbia.
Akiwa kwenye ardhi ya Tanzania Kibanda alitokwa machozi mengi baada ya kukutana na watu mbalimbali waliokwenda kumpokea,huku akitoa neno la shukrani kwa watu mbalimbali waliojitokeza kumpokea na hata wale waliokuwa naye karibu na waliokuwa wakimuombea siku zote za matibabu yake.
Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006) Ltd, alifanyiwa unyama huo Usiku wa Februari 25, mwaka huu majira ya saa 09:00 usiku, Kibanda alivamiwa na watu walioingia kwenye uzio wa nyumba yao wakavunja kioo cha gari analotumia, lakini kioo kilipovunjwa alarm ilipiga kelele, Kibanda akatoka nje na watu hao wakakimbia.
Akiwa kwenye ardhi ya Tanzania Kibanda alitokwa machozi mengi baada ya kukutana na watu mbalimbali waliokwenda kumpokea,huku akitoa neno la shukrani kwa watu mbalimbali waliojitokeza kumpokea na hata wale waliokuwa naye karibu na waliokuwa wakimuombea siku zote za matibabu yake.