VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Ilisemekana kuwa Dr.Stephen Ulimboka aliudhi watawala wa juu.Akatekwa,akateswa,akatupwa na siku ya pili akaokotwa Msitu wa Mabwepande. Sinema yake bado haijaisha.
Leo,'ametekwa' na kuteswa Ndugu yangu kiuandishi Absalom Kibanda. Sasa ameshatua Afrika Kusini kwa matibabu zaidi baada ya kukosekana huduma stahiki Muhimbili na hospitali nyinginezo za Dar es Salaam.Naye ana majeraha kichwani na jichoni.Ameumizwa vibaya na yuko katika hali mbaya.
Absalom Kibanda alikuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima linalosemekana kumilikiwa na CHADEMA(sina uhakika wa umiliki).Baadaye,akajiunga na New Habari Corporation kama Mhariri Mtendaji.New Habari Corporation inamilikiwa kwa kiasi kikubwa na Rostam Aziz.
Ni juzi tu,Kibanda aliandika makala ya kumsifu Abdurahman Kinana akichagiza kuteuliwa kwa Kinana kuwa Katibu Mkuu mpya wa chama cha Mapinduzi. Nimjuavyo Kibanda,ni mwandishi nguli na mahiri. Ni msema anachokiamini.
Kitendo cha kushambuliwa leo kinaacha maswali mengi. Kibanda amemuudhi nani tena? Kwanini sasa tabia ya kuteka na kutesa inaonekana kama ni dawa ya kuwakomesha wasemakweli?
Uchunguzi wa kina unahitajika hapa;tena haraka. Amasivyo,kila mtu atajilinda kwa namna anayoiona inafaa. Serikali ifanye kazi yake ya kuhakikisha ulinzi wa raia wake.
Leo,'ametekwa' na kuteswa Ndugu yangu kiuandishi Absalom Kibanda. Sasa ameshatua Afrika Kusini kwa matibabu zaidi baada ya kukosekana huduma stahiki Muhimbili na hospitali nyinginezo za Dar es Salaam.Naye ana majeraha kichwani na jichoni.Ameumizwa vibaya na yuko katika hali mbaya.
Absalom Kibanda alikuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima linalosemekana kumilikiwa na CHADEMA(sina uhakika wa umiliki).Baadaye,akajiunga na New Habari Corporation kama Mhariri Mtendaji.New Habari Corporation inamilikiwa kwa kiasi kikubwa na Rostam Aziz.
Ni juzi tu,Kibanda aliandika makala ya kumsifu Abdurahman Kinana akichagiza kuteuliwa kwa Kinana kuwa Katibu Mkuu mpya wa chama cha Mapinduzi. Nimjuavyo Kibanda,ni mwandishi nguli na mahiri. Ni msema anachokiamini.
Kitendo cha kushambuliwa leo kinaacha maswali mengi. Kibanda amemuudhi nani tena? Kwanini sasa tabia ya kuteka na kutesa inaonekana kama ni dawa ya kuwakomesha wasemakweli?
Uchunguzi wa kina unahitajika hapa;tena haraka. Amasivyo,kila mtu atajilinda kwa namna anayoiona inafaa. Serikali ifanye kazi yake ya kuhakikisha ulinzi wa raia wake.