TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Katikamakala yake ndefu ya tarehe 22 Novemba 2013 mhariri mashuhuri BwanaAbsalom Kibanda aliandika wasifu wa Katibu Mkuu wa sasa wa Chama ChaMapinduzi Ndugu Abdulrahaman Kinana baada ya uteuzi wake, katikamakala hiyo aliyoipa anuani "Absalom Kibanda: Namuogopa Abdurahman Kinana."alinukuliwa katika miongoni mwa aya zake ikisema kuwa;
"..nimtu asiyejali au mpuuzi asiyejua vyema siasa za Tanzania anayewezaakasimama na kuudharau uteuzi uliofanywa na Rais Kikwete ambaye baadaya kushindwa mara kadhaa hatimaye amefanikiwa kumshawishi mmoja wawanasiasa makini na wakongwe, mtumishi wa umma wa muda mrefu,mwanadiplomasia na kanali mstaafu wa jeshi, ABDULRAHAMAN KINANA kuwakatibu mkuu wa CCM.."
Baadaya makala hiyo ambayo ilikosolewa, kubezwa na kukosolewa hasa naviongozi wa vyama, taasisi na mashirikisho yenye mlengwa wa upinzaninchini, hatimaye Kibanda aliondolewa kutoka kampuni yake iliyomuajiriya free media akiwa mhariri mkuu na baadae kuhamia kampuni nyingineya Habari Corporation, pamoja na kufikwa na masahibu kadha wa kadhayaliyopelekea kumpa ulemavu wa kudumu.
Lakinisi Kibanda pekee, bali mwanazuoni, mwanasiasa chipukizi aliyehamaCHADEMA na kujiunga na CCM Ndugu Juliana Shonza nae aliandika makalaambayo aliisambaza kwenye mitandao ya kijamii yenye anuani "HUYUNDIE KINANA NINAYEMFAHAMU, MWALIMU WA SIASA NA KIONGOZI MWENYEUPENDO" ambapo kwenye makala hiyo, Shonza alisifu na kupongezahatua mbalimbali za utendaji na ufanisi wa Katibu Mkuu huyo.
Makalayangu italenga kutoa ushuhuda wa ukweli wa waliyoyaandika wanataalumahao, nikilinganisha na hatua na mafanikio mbalimbali ambayo Chama ChaMapinduzi kimeyapata kwa muda mfupi tangu kuteuliwa kwa NduguAbdulrahaman Kinana kuwa katibu mkuu.
Kwanzakabisa ningeanza kukumbusha jambo ambalo pia lilikumbushwa na muasisiwa TANU na CCM Baba wa Taifa hili, marehemu Mwalimu Julius KambarageNyerere katika hotuba yake aliyoitoa katika ukumbi wa Chimwaga mwaka1995, alipowakumbusha wanaCCM juu ya asili ya kuundwa kwa CCM,aliwaambia kuwa Chama Cha Mapinduzi hakijawa chama cha matajiri,akawakumbusha kuwa msingi wa kuundwa TANU na baade CCM ni kuwasemea,kuwatetea na kuwasaidia wanyonge, masikini, wakulima na wafanyakaziwa nchi hii.
Kwa hali ilivyokuwa awali ni kama vile tayari wanaCCMhasa viongozi walianza kusahau msingi huu na jukumu hili lakimaumbile la CCM. Kinana ameirudisha CCM katika msingi na asili yakuundwa kwake, CCM ya leo chini ya Kinana ndio inayohakikisha kuwamatatizo ya wakulima wa nchi hii yanapatiwa ufumbuzi, kero zawafanyakazi zinatatuliwa na sauti ya wanyonge inapazwa na kusikikakupitia Chama Cha Mapinduzi, tumeona na kushuhudia katika ziara zakealizofanya kote nchini, Ndugu Kinana akiwa na wananchi wa kawaida,mabalozi wa nyumba kumi, wenyeviti wa mtaa na vitongoji wakila pamojana kujadili pamoja.
Lakini pia tumeshuhudia maduhuli, posho na malipoya walimu na wafanyakazi wa Serikali na Mashirika yakitolewa baada yasauti za wafanyakazi hao kubebwa na Katibu Mkuu huyo wa CCM,tumeshuhudia bei ya korosho, Mahindi, Ufuta na utaratibu wa manunuziukiboreshwa baada ya sauti ya wakulima kupazwa na Katibu Mkuu huyo waChama tawala.
Katikamambo ambayo yameendelea kumfanya Kinana aonekane kiongozi mwenyemaono na uwezo wa kipekee ndani ya Chama ni hatua yake ya kuamuakukirudisha Chama katika msingi wa utumishi kwa watu. Chama kimerudikuwatumikia wananchi, wanyonge na masikini wa nchi hii. Viongozi waChama Cha Mapinduzi leo wanaweza kusimama na kutembea kifua mbele kwamafanikio na kazi nzuri ambayo inaendelea kufanywa na viongozi waChama hicho ya kuisimamia Serikali.
Miongonimwa mambo yaliyodhihirisha uwezo mkubwa aliokuwa nao Komredi Kinanani pamoja na ukweli kuwa Komredi amekabidhiwa Chama kikiwa na mpasukomkubwa wa kimakundi ambayo yalitishia kukizamisha Chama katikanyakati tofauti lakini kwa maoni na ufanisi wa hali ya juu KatibuMkuu huyo aliweza kuimaliza hatari kubwa iliyotokana na mpasuko huondani ya Chama, na sasa wanaccm ni wamoja, wenye mshikamano tenaimara na madhubuti kuliko awali.
Haliya uchumi wa Chama imeendelea kuimarika na maslahi ya watumishi waChama Cha Mapinduzi yameendelea kuboreshwa siku baada ya siku, ambapopamoja na kupanda kwa mishahara lakini pia viwango vya posho kwaviongozi, watumishi na watendaji wa Chama yameendelea kuboreshwa hatakwa watendaji na viongozi wa ngazi za chini kabisa kama makatibu wamatawi na wajumbe wa nyumba kumi ambao hapo awali hawakuwa katikautaratibu wa malipo.
Lakiniuimara huu wa Chama Cha Mapinduzi katika siasa za upinzani zinatoatafsiri moja kuu kuwa ni kudorora na kufifia kwa Upinzani nchini.Kila CCM inapozidi kuwa maarufu na kuendelea kuimarika kwenye mioyoya watanzania, ndipo kwa kasi hiyo hiyo upinzani unazidi kusahaulikana kufa kifo cha kawaida. Tumeshuhudia kupoteza mwelekeo kwa vyamavya upinzani nchini kukiongozwa na Chama kikuu cha Upinzani Chademaambapo viongozi wake wamekuwa wakihaha kukinusuru chama hicho ambachotayari kinachungulia kaburi.
Nadhaniwale ambao walibeza awali wameanza kumuelewa Kibanda hivi sasa,lakini wakati Bongo zao zikijitahidi kufanya tathimini ya uzito naukweli wa maneno ya Kibanda tayari wamejikuta katika mazingira ambayohawana tena utulivu na murua wa kufanya tafakuri jadidi ya kesho yaona vyama vyao. Huyu ndiye Kinana ambaye wanasiasa mashuhuri nawachambuzi wanamuogopa, nami naungana nao kwani sasa NIMEANZAKUMUOGOPA KINANA.
"..nimtu asiyejali au mpuuzi asiyejua vyema siasa za Tanzania anayewezaakasimama na kuudharau uteuzi uliofanywa na Rais Kikwete ambaye baadaya kushindwa mara kadhaa hatimaye amefanikiwa kumshawishi mmoja wawanasiasa makini na wakongwe, mtumishi wa umma wa muda mrefu,mwanadiplomasia na kanali mstaafu wa jeshi, ABDULRAHAMAN KINANA kuwakatibu mkuu wa CCM.."
Baadaya makala hiyo ambayo ilikosolewa, kubezwa na kukosolewa hasa naviongozi wa vyama, taasisi na mashirikisho yenye mlengwa wa upinzaninchini, hatimaye Kibanda aliondolewa kutoka kampuni yake iliyomuajiriya free media akiwa mhariri mkuu na baadae kuhamia kampuni nyingineya Habari Corporation, pamoja na kufikwa na masahibu kadha wa kadhayaliyopelekea kumpa ulemavu wa kudumu.
Lakinisi Kibanda pekee, bali mwanazuoni, mwanasiasa chipukizi aliyehamaCHADEMA na kujiunga na CCM Ndugu Juliana Shonza nae aliandika makalaambayo aliisambaza kwenye mitandao ya kijamii yenye anuani "HUYUNDIE KINANA NINAYEMFAHAMU, MWALIMU WA SIASA NA KIONGOZI MWENYEUPENDO" ambapo kwenye makala hiyo, Shonza alisifu na kupongezahatua mbalimbali za utendaji na ufanisi wa Katibu Mkuu huyo.
Makalayangu italenga kutoa ushuhuda wa ukweli wa waliyoyaandika wanataalumahao, nikilinganisha na hatua na mafanikio mbalimbali ambayo Chama ChaMapinduzi kimeyapata kwa muda mfupi tangu kuteuliwa kwa NduguAbdulrahaman Kinana kuwa katibu mkuu.
Kwanzakabisa ningeanza kukumbusha jambo ambalo pia lilikumbushwa na muasisiwa TANU na CCM Baba wa Taifa hili, marehemu Mwalimu Julius KambarageNyerere katika hotuba yake aliyoitoa katika ukumbi wa Chimwaga mwaka1995, alipowakumbusha wanaCCM juu ya asili ya kuundwa kwa CCM,aliwaambia kuwa Chama Cha Mapinduzi hakijawa chama cha matajiri,akawakumbusha kuwa msingi wa kuundwa TANU na baade CCM ni kuwasemea,kuwatetea na kuwasaidia wanyonge, masikini, wakulima na wafanyakaziwa nchi hii.
Kwa hali ilivyokuwa awali ni kama vile tayari wanaCCMhasa viongozi walianza kusahau msingi huu na jukumu hili lakimaumbile la CCM. Kinana ameirudisha CCM katika msingi na asili yakuundwa kwake, CCM ya leo chini ya Kinana ndio inayohakikisha kuwamatatizo ya wakulima wa nchi hii yanapatiwa ufumbuzi, kero zawafanyakazi zinatatuliwa na sauti ya wanyonge inapazwa na kusikikakupitia Chama Cha Mapinduzi, tumeona na kushuhudia katika ziara zakealizofanya kote nchini, Ndugu Kinana akiwa na wananchi wa kawaida,mabalozi wa nyumba kumi, wenyeviti wa mtaa na vitongoji wakila pamojana kujadili pamoja.
Lakini pia tumeshuhudia maduhuli, posho na malipoya walimu na wafanyakazi wa Serikali na Mashirika yakitolewa baada yasauti za wafanyakazi hao kubebwa na Katibu Mkuu huyo wa CCM,tumeshuhudia bei ya korosho, Mahindi, Ufuta na utaratibu wa manunuziukiboreshwa baada ya sauti ya wakulima kupazwa na Katibu Mkuu huyo waChama tawala.
Katikamambo ambayo yameendelea kumfanya Kinana aonekane kiongozi mwenyemaono na uwezo wa kipekee ndani ya Chama ni hatua yake ya kuamuakukirudisha Chama katika msingi wa utumishi kwa watu. Chama kimerudikuwatumikia wananchi, wanyonge na masikini wa nchi hii. Viongozi waChama Cha Mapinduzi leo wanaweza kusimama na kutembea kifua mbele kwamafanikio na kazi nzuri ambayo inaendelea kufanywa na viongozi waChama hicho ya kuisimamia Serikali.
Miongonimwa mambo yaliyodhihirisha uwezo mkubwa aliokuwa nao Komredi Kinanani pamoja na ukweli kuwa Komredi amekabidhiwa Chama kikiwa na mpasukomkubwa wa kimakundi ambayo yalitishia kukizamisha Chama katikanyakati tofauti lakini kwa maoni na ufanisi wa hali ya juu KatibuMkuu huyo aliweza kuimaliza hatari kubwa iliyotokana na mpasuko huondani ya Chama, na sasa wanaccm ni wamoja, wenye mshikamano tenaimara na madhubuti kuliko awali.
Haliya uchumi wa Chama imeendelea kuimarika na maslahi ya watumishi waChama Cha Mapinduzi yameendelea kuboreshwa siku baada ya siku, ambapopamoja na kupanda kwa mishahara lakini pia viwango vya posho kwaviongozi, watumishi na watendaji wa Chama yameendelea kuboreshwa hatakwa watendaji na viongozi wa ngazi za chini kabisa kama makatibu wamatawi na wajumbe wa nyumba kumi ambao hapo awali hawakuwa katikautaratibu wa malipo.
Lakiniuimara huu wa Chama Cha Mapinduzi katika siasa za upinzani zinatoatafsiri moja kuu kuwa ni kudorora na kufifia kwa Upinzani nchini.Kila CCM inapozidi kuwa maarufu na kuendelea kuimarika kwenye mioyoya watanzania, ndipo kwa kasi hiyo hiyo upinzani unazidi kusahaulikana kufa kifo cha kawaida. Tumeshuhudia kupoteza mwelekeo kwa vyamavya upinzani nchini kukiongozwa na Chama kikuu cha Upinzani Chademaambapo viongozi wake wamekuwa wakihaha kukinusuru chama hicho ambachotayari kinachungulia kaburi.
Nadhaniwale ambao walibeza awali wameanza kumuelewa Kibanda hivi sasa,lakini wakati Bongo zao zikijitahidi kufanya tathimini ya uzito naukweli wa maneno ya Kibanda tayari wamejikuta katika mazingira ambayohawana tena utulivu na murua wa kufanya tafakuri jadidi ya kesho yaona vyama vyao. Huyu ndiye Kinana ambaye wanasiasa mashuhuri nawachambuzi wanamuogopa, nami naungana nao kwani sasa NIMEANZAKUMUOGOPA KINANA.