Kibamba: Mwanasheria CCM anatapatapa

Kibamba: Mwanasheria CCM anatapatapa

R.B

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2012
Posts
6,296
Reaction score
2,578


[TD="bgcolor: #ffffff"]




MWENYEKITI wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Deus Kibamba amesema mwanasheria wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) anatapatapa kutokana na kutaka jukwaa hilo lifutwe kwa sababu linajishughulisha na siasa kinyume cha sheria.

Kauli hiyo imekuja baada ya Mwanasheria wa CCM, Godwin Kunambi kudai kuwa jukwaa hilo limevunja sheria ya mwaka 2002 kifungu cha 20 kinachokataza asasi za kiraia kujihusisha na masuala ya siasa.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Kibamba alisema hakushangazwa na kauli hiyo kwa sababu imetolewa kwa makusudi, ili kuupotosha umma wa wapenda demokrasia nchini.
Kibamba alisema anapingana na kauli ya mwanasheria huyo wa CCM kuwa jukwaa hilo limejiunga na muungano wa vyama vya siasa.
Alisema kilichofanywa na jukwaa hilo ni kuunga mkono umoja wa vyama vya siasa vilivyoko ndani ya Bunge kupinga kuburuzwa na CCM katika upitishwaji wa muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba.



[/TD]
[TD="width: 200, bgcolor: #FFFFFF, align: center"]
[/TD]
 
Kauli ya mwanasheria ni sahihi kabisa. Kibamba aanzishe chama cha siasa au jukwaa la katiba liwe chama cha siasa. Aache usanii
 
Kibamba akamatwe na polisi kwa kuvunja katiba ya nchi
 
safi sana kibamba.

mgema akisifiwa tembo ulitia maji; naona kibamba kalewa sifa kama balozi wa china; ajui kama anatumiwa mi nilishamuona kama si cuf basi chadema
 
Kibamba akamatwe na polisi kwa kuvunja katiba ya nchi

ni bora kuwa na wahamiaj haramu nchin kuliko kuwa na mtz mwenye mawazo mgando kama ww.

Huu utaratibu wa kukamata mbona haujawaona wauza unga,wafanya siasa makanisan/misikin,wamwagia watu tindikal,watesaji, waua tembo,mchina wa maccm,wez etc.

Suala la katiba ni la watanzania na si maccm (2millio) kuhodh mamlaka ya watu 45million.
 
Nilipomsikia huyo anaeitwa mwanasheria kupitia ITV, hakika nilisikitika sana, anyway, kichwani mwangu niliwaza hivi, eidha alikua anatuma message kwa Kibamba kwamba polisi wapo njiani kumkamata na au kuifungia kabisa hiyo NGO yao au ndio yale yale ya wasomi wetu walioko ccm, akili hua waziacha Lumumba na kutembea na vichwa vitupu! Kwa ufupi sikuelewa kabisa hoja yake ya NGO kuingilia siasa, hiyo taasisi ya akina kibamba inaitwa Jukwaa la Katiba, hivi siasa ni nini kama hakuna Katiba?
 
Watu wanaojielewa wametegua mtego mdhaifu wa ccm.
Watanzania ni wengi mara 10 ya wanachama wasiojulikana wa ccm.
 
NYIE MNAHANGAIKA BURE NA KIBAMBA HAO NDIO MAFISADI WENGINE. ALIMTISHIA WARIOBA ANAMPELEKA MAHAKAMANI.WARIOBA AKAMWAMBIA " WAHI HARAKA NI VIZURI PIA TUTAJUA HILI BARAZA LA KATIBA NI AKINA NANI NA LINAMILIKIWA NA NANI?" sasa nyie mnaompa sapoti huyo Kibamba jiulizeni alikwenda? kama hakwenda jiulizeni WHY. hii ni nchi ya kutafunwa tu na wajanja wajinga kama huyu Kibamba,hii ndio biashara ya ulaji bana Tz= UBABAISHAJI. watu wanaanzisha mabaraza kama haya na NGO kwa ulaji tu sio kumsaidia mwananchi. WATZ AMKENI MNALIWA NA WAJANJA WAJINGA
 
Maccm yamepaniki yanajua yanakalibia kuzimuni..
.....yanajua kukiwekwa mizania sawa kupitia katiba hayana chao,lkn yakae yakijua mabadiliko hayaepukiki....
..ni wakati wa watanzania kufurahia matunda ya uhuru na sio kama ilivyo hivi sasa wachache ndo wanaofaidi....
 
Hivi unawezaje kuijadili katiba na hapo hapo isionekane ni siasa?Vimetoa maoni vyama vya siasa wamelalamika "Vyama vinauteka mchakato wa katiba"
Haya amesema Kibamba "Oooh huyu ni mwanasiasa"

Sasa mnataka Kibamba agawe vyandarua ndio mjue hii ni NGO? Kwani lazima NGO zote zigawe vyandarua au kuona watoto wa mitaani ndio mkubali kuwa hio ndio NGO inayowapa raha...?

NGO ya Kibamba ni ya katiba, there is no way ikaacha kusema siasa. Its only unfortunate siasa yao ni ya haki na its not in the favor ya magamba. Kunambi ni lazima alalamike.

Poleni, sifa ya dawa nyingi na nzuri sio tamu. Ni chungu lakini zinaponyesha. Magamba tulieni mpewe dawa au wawaache maradhi yawaumbue kwa kifo.
 
Back
Top Bottom