Date::10/4/2008
Hatima ya mafisadi wa EPA yakaribia ukingoni
Na Ramadhan Semtawa
HATIMAYE siku za kubaini mbivu na mbichi kwa kujulikana hatma ya mafisadi walioza zaidi ya sh 133 bilioni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT), zimewadia.
Awali ilikuwa ni miezi tangu Rais Jakaya Kikwete, kutangazia umma katika hotuba yake kupitia bunge hapo mwishoni mwa mwezi Agosti na kueleza kurejesha zaidi ya sh 53 bilioni, sasa zimebaki siku.
Maswali mawili makubwa yaliyopo katika 'mwezi huu wa EPA' ni kama Timu ya Rais itaweza kurejesha fedha zote zikiwemo sh 42.6 bilioni, ambazo zimeibwa na makampuni tisa ambayo taarifa zake nyingi ziko nje ya nchi na kiasi kingine katika sh 90.3 bilioni.
Swali la pili, baada ya makampuni na watuhumiwa kurejesha fedha hatua gani za kijania zitachukuliwa kwani tayari wanaharakati wametaka watuhumiwa wafikishwe mahakamani kwa makosa ya jinai, huku serikali ikiwa imewatega mafisadi hao.
Ufisadi wa EPA umegawanyika katika makundi mawili, ambayo ni wizi wa sh 90.3 bilioni zilizoibwa na makampuni 13 yaliyotumia nyaraka za kughushi na sh 42.6 bilioni zilizoibwa na makampuni tisa, ambayo uhalali wa malipo yake ndiyo wenye shaka.
Lakini, ukweli wa yote hayo unatarajiwa kujulikana katika kipindi cha siku 26 ambacho ni hapo Oktoba 31, kama ambavyo Rais alionya ambao hawatakuwa wamerejesha fedha katika kipindi hicho, Novemba mosi wawe mahakamani.
Hata hivyo, akizungumzia kwa kifupi uchunguzi huo unaondelea, Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Jenerali (IGP) Said Mwema, alionya kwamba hakuna fisadi wa EPA atakayepona.
IGP Mwema akisisitiza, alisema jeshi la siyo kweli kwamba uchunguzi huo amechiwa Rais, bali unaendelea kwa umakini.
"Uchunguzi bado unaendelea, ripoti kamili itatoka Novemba mosi, hatuja mwachia Rais jukumu hili bado liko mikononi mwetu tunalifanyia kazi," alionya IGP Mwema.
Onyo hilo la Mwema liko nyuma ya onyo la Amiri Jeshi Mkuu, ambaye katika hotuba hiyo alionya kwamba, ifikapo Novemba mosi wote watakaokuwa hawajaresha fedha walizoiba EPA, watafikishwa mahakamani Novemba mosi.
Rais akisisitiza hilo kwamba, watuhumiwa wa EPA wako katika hali mbaya ingawa wanapita mitaani na 'kupiga' tai shingoni, alisema hatakuwa na huruma na wote watakaokiuka hilo.
Onyo hilo la Rais linalotiwa nguvu na kauli ya IGP Mwema, linazidi kuweka Watanzania mkao wa kusubiri kuona utekelezaji kivitendo kwa watuhumiwa hao.
Hadi sasa Watanzania walio wengi, wnaonekana kukatishwa tamaa na hatua za serikali katika kushughulikia tuhuma hizo za ufisadi, ingawa imekuwa ikipongezwa na wafadhili wakiwemo Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).
Lakini, jambo kubwa ambalo hadi sasa linatia shaka katika fedha hizo, pia ni wapi zilipo kwani BoT haina akaunti hiyo, ingawa serikali yenyewe inasema zipo katika akaunti maalumu.
Uamuzi wa Rais kuongeza muda wa uchunguzi, kutoka miezi sita hadi Oktoba 31,umezingatia zaidi upatikanaji wa taarifa zinazohusu ufisadi wa sh 42.6 bilioni, ambazo sehemu kubwa ya makampuni yake yako nje na kutegemea taarifa za Polisi wa Kimataifa (Interpol).
Miongoni mwa makampuni ya nje yanayotajwa kuwa wadai halali lakini wakalipwa mengine ni Maruben na Toyota, ambayo taarifa za uhusiano wao kibiashara na waliolipwa fedha za EPA zikiwa ngumu kuzipata.
Deni la EPA hadi mwaka 1999 lilifikia dola 623 milioni, ambazo kati ya hizo dola 325 milioni zilikuwa ni deni la msingi na dola 298 ni riba na kisha baadaye deni likaongezeka hadi kufikia dola 677 milioni.
Hata hivyo, chini ya Mpango wa Kununua Madeni (Debt Buy Back Scheme) wa mwaka 1994 kati ya serikali na Benki ya Dunia (WB), waliokuwa wanaidai BoT waliombwa wakubali kulipwa sehemu tu ya fedha wanazodai, wapo waliokubali na wengine kukataa na kuongeza hadi mwaka 2004 taarifa zinaonyesha jumla ya dola 228 zililipwa chini ya mpango huo.
Mpango huo baadaye ulileta matatizo ambayo yalibainika katika Ukaguzi wa Hesabu za BoT za mwaka 2005/06, ambao ulifanyika Agosti mwaka 2005, ambao ulionyesha matatizo katika ulipaji wa madeni kwa utaratibu huo wa idhini ya kulipwa wakala wa mdai katika akaunti ya EPA.
Kukatokea kutoelewana kati ya BoT na Mkaguzi Deloitte and Touche, aliyegundua tatizo hilo, ndipo serikali iliingilia kati na Desemba 4, 2006, ilimuagiza CAG kuhakikisha ukaguzi huo unafanyika kwa kina.
Mwaka 1985, EPA ilihamishiwa moja kwa moja BoT, na ndipo mwaka juzi kulipoibuka utata wa tuhuma za ufisadi katika akaunti hiyo kwa mahesabu ya mwaka 2005/06.
Januari mosi, Rais aliunda timu ya uchunguzi wa ufiasdi huo wa zaidi ya sh 133 bilioni, kumtimua kazi aliyekuwa Gavana marehemu Dk Daud Ballali, hata hivyo timu hiyo ilikabidhi ripoti yake Agosti 18 na Rais kuongeza muda hadi Oktoba 31.
Hatima ya mafisadi wa EPA yakaribia ukingoni
Na Ramadhan Semtawa
HATIMAYE siku za kubaini mbivu na mbichi kwa kujulikana hatma ya mafisadi walioza zaidi ya sh 133 bilioni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT), zimewadia.
Awali ilikuwa ni miezi tangu Rais Jakaya Kikwete, kutangazia umma katika hotuba yake kupitia bunge hapo mwishoni mwa mwezi Agosti na kueleza kurejesha zaidi ya sh 53 bilioni, sasa zimebaki siku.
Maswali mawili makubwa yaliyopo katika 'mwezi huu wa EPA' ni kama Timu ya Rais itaweza kurejesha fedha zote zikiwemo sh 42.6 bilioni, ambazo zimeibwa na makampuni tisa ambayo taarifa zake nyingi ziko nje ya nchi na kiasi kingine katika sh 90.3 bilioni.
Swali la pili, baada ya makampuni na watuhumiwa kurejesha fedha hatua gani za kijania zitachukuliwa kwani tayari wanaharakati wametaka watuhumiwa wafikishwe mahakamani kwa makosa ya jinai, huku serikali ikiwa imewatega mafisadi hao.
Ufisadi wa EPA umegawanyika katika makundi mawili, ambayo ni wizi wa sh 90.3 bilioni zilizoibwa na makampuni 13 yaliyotumia nyaraka za kughushi na sh 42.6 bilioni zilizoibwa na makampuni tisa, ambayo uhalali wa malipo yake ndiyo wenye shaka.
Lakini, ukweli wa yote hayo unatarajiwa kujulikana katika kipindi cha siku 26 ambacho ni hapo Oktoba 31, kama ambavyo Rais alionya ambao hawatakuwa wamerejesha fedha katika kipindi hicho, Novemba mosi wawe mahakamani.
Hata hivyo, akizungumzia kwa kifupi uchunguzi huo unaondelea, Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Jenerali (IGP) Said Mwema, alionya kwamba hakuna fisadi wa EPA atakayepona.
IGP Mwema akisisitiza, alisema jeshi la siyo kweli kwamba uchunguzi huo amechiwa Rais, bali unaendelea kwa umakini.
"Uchunguzi bado unaendelea, ripoti kamili itatoka Novemba mosi, hatuja mwachia Rais jukumu hili bado liko mikononi mwetu tunalifanyia kazi," alionya IGP Mwema.
Onyo hilo la Mwema liko nyuma ya onyo la Amiri Jeshi Mkuu, ambaye katika hotuba hiyo alionya kwamba, ifikapo Novemba mosi wote watakaokuwa hawajaresha fedha walizoiba EPA, watafikishwa mahakamani Novemba mosi.
Rais akisisitiza hilo kwamba, watuhumiwa wa EPA wako katika hali mbaya ingawa wanapita mitaani na 'kupiga' tai shingoni, alisema hatakuwa na huruma na wote watakaokiuka hilo.
Onyo hilo la Rais linalotiwa nguvu na kauli ya IGP Mwema, linazidi kuweka Watanzania mkao wa kusubiri kuona utekelezaji kivitendo kwa watuhumiwa hao.
Hadi sasa Watanzania walio wengi, wnaonekana kukatishwa tamaa na hatua za serikali katika kushughulikia tuhuma hizo za ufisadi, ingawa imekuwa ikipongezwa na wafadhili wakiwemo Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).
Lakini, jambo kubwa ambalo hadi sasa linatia shaka katika fedha hizo, pia ni wapi zilipo kwani BoT haina akaunti hiyo, ingawa serikali yenyewe inasema zipo katika akaunti maalumu.
Uamuzi wa Rais kuongeza muda wa uchunguzi, kutoka miezi sita hadi Oktoba 31,umezingatia zaidi upatikanaji wa taarifa zinazohusu ufisadi wa sh 42.6 bilioni, ambazo sehemu kubwa ya makampuni yake yako nje na kutegemea taarifa za Polisi wa Kimataifa (Interpol).
Miongoni mwa makampuni ya nje yanayotajwa kuwa wadai halali lakini wakalipwa mengine ni Maruben na Toyota, ambayo taarifa za uhusiano wao kibiashara na waliolipwa fedha za EPA zikiwa ngumu kuzipata.
Deni la EPA hadi mwaka 1999 lilifikia dola 623 milioni, ambazo kati ya hizo dola 325 milioni zilikuwa ni deni la msingi na dola 298 ni riba na kisha baadaye deni likaongezeka hadi kufikia dola 677 milioni.
Hata hivyo, chini ya Mpango wa Kununua Madeni (Debt Buy Back Scheme) wa mwaka 1994 kati ya serikali na Benki ya Dunia (WB), waliokuwa wanaidai BoT waliombwa wakubali kulipwa sehemu tu ya fedha wanazodai, wapo waliokubali na wengine kukataa na kuongeza hadi mwaka 2004 taarifa zinaonyesha jumla ya dola 228 zililipwa chini ya mpango huo.
Mpango huo baadaye ulileta matatizo ambayo yalibainika katika Ukaguzi wa Hesabu za BoT za mwaka 2005/06, ambao ulifanyika Agosti mwaka 2005, ambao ulionyesha matatizo katika ulipaji wa madeni kwa utaratibu huo wa idhini ya kulipwa wakala wa mdai katika akaunti ya EPA.
Kukatokea kutoelewana kati ya BoT na Mkaguzi Deloitte and Touche, aliyegundua tatizo hilo, ndipo serikali iliingilia kati na Desemba 4, 2006, ilimuagiza CAG kuhakikisha ukaguzi huo unafanyika kwa kina.
Mwaka 1985, EPA ilihamishiwa moja kwa moja BoT, na ndipo mwaka juzi kulipoibuka utata wa tuhuma za ufisadi katika akaunti hiyo kwa mahesabu ya mwaka 2005/06.
Januari mosi, Rais aliunda timu ya uchunguzi wa ufiasdi huo wa zaidi ya sh 133 bilioni, kumtimua kazi aliyekuwa Gavana marehemu Dk Daud Ballali, hata hivyo timu hiyo ilikabidhi ripoti yake Agosti 18 na Rais kuongeza muda hadi Oktoba 31.