Khitma ya Saigon club ya Iddi Simba msikiti wa Mtoro

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,954
30,301
KHITMA YA SAIGON CLUB YA IDDI SIMBA MSIKITI WA MTORO

Msikiti wa Mtoro kwa baadhi yetu tuliokulia Dar es Salaam unatukumbusha wengi katika wapendwa wetu ambao wametangulia mbele ya haki.

Binafsi namkumbuka mzee wangu, baba yangu na rafiki yangu Sheikh Zubeir Said Chanzi ambae yeye kakua na baba yangu toka udogo wao Mtaa wa Kipata katika miaka ya 40.

Sheikh Zubeir alikuwa habanduki Msikiti wa Mtoro toka ule wa asili uliojengwa na Sheikh Mtoro Mwinyi Mangara hadi ulipovunjwa na kujengwa mara mbili na huu ujenzi wa tatu ukajengwa na Said Salum Bakhersa ambao ndiyo msikiti huu wa fahari uliokuwapo hivi sasa.

Wengi tuna kumbukumbu za Msikiti wa Mtoro wakati wa Sheikh Kassin bin Juma akiwa Imam Mkuu katika miaka ya 1980 wakati Waislam walipitia kipindi kigumu sana na kwa bahati nzuri au mbaya Rais wa Tanzania alikuwa Sheikh Ali Hassan Mwinyi.

Huu ulikuwa wakati wa Barua za Kiuchungaji na ulikuwa pia wakati wa Mihadhara ya Biblia na ulikuwa wakati Sheikh Kassim akitoa hotuba kali za Ijumaa zilizosisimua Waislam.

Huu ulikuwa wakati hata gazeti la Chama na Serikali Uhuru na Mzalendo na Daily News zikimshambulia Mwenyekiti wa chama chenyewe na Rais wa nchi.

Haya hayakupata kutokea wakati rais Nyerere yuko madarakani.

Haya ndiyo yaliyompa nguvu Sheikh Kassim Juma kutumia membar ya Msikiti wa Mtoro kutoa majibu.

Katika moja ya khutba nyingi alizopata kutoa hii moja iliniathiri sana mimi na nimeipa jina, ''Leo Nitataja Majina.''

Sheikh Kassim Juma siku ile alianza hotuba yake kwa kusema kuwa ''nitataja majina.''

Khutba hii Sheikh Kassim alitaja majina kama matatu, Rajab Diwani, Abdul Sykes na Maalim Mohamed Matar na kila mtu akimpa sifa zake alizostahili na uhusiano wake na Mwalimu Nyerere katika historia ya uhuru wa Tanganyika ukimtoa Maalim Matar.

Sheikh Kassim alikuwa bingwa wa kuzungumza na alikuwa akijua namna ya kugusa hisia ya hadhira yake.

Siku ile alimtaja Abdul Sykes siku ya maziko yake na vipi yeye na Mwalimu Nyerere walivyoshiriki katika maziko yale.

Sheikh Kassim siku ile kwa mara ya kwanza aliueleza umma akasema, ''Huyu Abdul Sykes alikuwa mtu wake sana Nyerere.''

Nimekaa pale msikitini mengi yaliyopitika pale yakinirudia.

Kwa hakika msikiti unavutia na Sheikh Mtoro wa Mangara ikiwa Allah atamuonesha msikiti wake ulivyo sasa ataukataa atasema msikiti wake haukuwa hivi msikiti wake ulikuwa kibanda cha udongo, fito, mawe na chokaa.

Nimekaa msikitini pale nakumbuka mengi yaliyopita.

Nakumbuka Iddi Simba pale msikitini akiswali safu ya mbele na akimsikiliza Sheikh Kassim akitoa zile hotuba ambazo kabla hazikupata kutolewa.

Wako wenzake wengi waliukimbia msikiti kwa hofu.

Iddi Simba hakuondoa alikuwapo wakati wote ametulia pale mbele akimsikiliza Sheikh Kassim.

Sheikh Kassim kakamatwa kawekwa jela.

Iddi Simba hakuacha kuja kuswali Mtoro.

Iko siku nikamuuliza kwa nini yeye bado yupo Msikiti wa Mtoro hajaukimbia kama wenzake.

Jibu alilonipa ni kuwa yapo mafunzo ya kujifunza na ipo faida kwa pande zote.

Nikiwa msikitini pale nilimtazama Mzee Mwinyi na nikawa nafikiria shida alizopata wakati wa utawala wake na nilifarajika sana kwa kumuona jinsi alivyokuwa ''relaxed,'' hakika kama nahodha ambae juu ya misukosuko ya bahari alikifikisha chombo salama bandarini.

Nakumbuka wakati huu wa utawala wake baada ya kuwa anashambuliwa hata na vyombo vyake vyenyewe vya Chama na Serikali marehemu Ahmed Saleh Yahya alikuja Dar es Salaam kutoka London tukiwa tunakunywa chai, sambusa na kababu katika mgahawa mmoja katikati ya mji akaniomba kwa siri niandike makala ya kumtetea Rais Mwinyi.

Ahmed Saleh Yahya alikuwa Mhariri wa Africa Events jarida maarufu miaka ile.

Angalia picha iliyowekwa ya makala ambayo niliandika kueleza matatizo ya Tanzania katika kipindi kile.

Lakini haya yote yakapita kwa salama na leo imebakia historia.

Chembelecho Mzee Mwinyi anatuasa tuwe hadithi nzuri kusimuliwa pale tutakapoondoka duniani.

Iddi Simba ni hadithi inayopendeza katika kila sikio.

Allah akubali dua zetu ampokee mzee wetu Iddi Simba na atukutanishe pamoja nae Firdaus.

MWINYI CARICATURE.jpg
 
Ndugu zake wa karibu Marehemu Iddi Simba wapo kimya lakini Mohamed Said na kimbelembele chake kashindwa kujizuia yumo humu kutangaza utadhani Msemaji wa Familia. Ndiyo hiyohiyo misifa yake inayomfanya ajione na ajitwike kama yeye ndiyo mtetezi namba wani wa Waislamu wote Tanzania.
 
Ndugu zake wa karibu Marehemu Iddi Simba wapo kimya lakini Mohamed Said na kimbelembele chake kashindwa kujizuia yumo humu kutangaza utadhani Msemaji wa Familia. Ndiyo hiyohiyo misifa yake inayomfanya ajione na ajitwike kama yeye ndiyo mtetezi namba wani wa Waislamu wote Tanzania.
Ndjabu...
Mimi nimeombwa nizungumze si kuwa nimezungumza kwa kimbelembele changu.

Imekuwa kawaida kila panapokuwa na shughuli ya Waislam khasa ikiwa ni msiba huwa naombwa nimzungumze marehemu kama nilivyomfahamu.

Nimezungumza katika maziko ya Ally Sykes, Kitwana Kondo na hivi karibuni Iddi Simba.

Halikadhalika nimeandika taazia zao na za watu wengi maarufu wa Dar es Salaam kama Ahmed Rashad Ali, Mohamed Awadh (Chico), Zubeir Mtemvu, Tewa Said Tewa, Bi. Titi Mohamed, Abubakar Tambaza wengi tu.

Nimeandika pia taazia ya Mwalimu Julius Nyerere.

Ni bahati mbaya kuwa hili linakukera lakini nifanyeje na hawa ni ndugu zangu na mimi nimezaliwa Dar es Salaam na wote nikiwajua nani awaandike?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Idd Simba alikuwa Binaadamu kama wengine. Marehemu hasemwi kwa mabaya tuliusiwa! Mzee MS ungependa na 'fraud' za Mzee wetu tuziweke wazi

Ila nikikusoma vizuri Nyerere alikuwa kiongozi mahiri haijapata tokea Tanzani. Toka mazishi ya Sykes na namna alivyodhibiti migawanyiko Tanzania.

Naikubali pia busara ya Abdul Sykes baada ya Uhuru kutosema mengi yanayohusu kabla ya Uhuru. Najua kuna wakati unapitiliza kuongeza chumvi ila nina hakika angekuwepo asingependa hilo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndjabu...
Mimi nimeombwa nizungumze si kuwa nimezungumza kwa kimbelembele changu.

Imekuwa kawaida kila panapokuwa na shughuli ya Waislam khasa ikiwa ni msiba huwa naombwa nimzungumze marehemu kama nilivyomfahamu.

Nimezungumza katika maziko ya Ally Sykes, Kitwana Kondo na hivi karibuni Iddi Simba.

Halikadhalika nimeandika taazia zao na za watu wengi maarufu wa Dar es Salaam kama Ahmed Rashad Ali, Mohamed Awadh (Chico), Zubeir Mtemvu, Tewa Said Tewa, Bi. Titi Mohamed, Abubakar Tambaza wengi tu.

Nimeandika pia taazia ya Mwalimu Julius Nyerere.

Ni bahati mbaya kuwa hili linakukera lakini nifanyeje na hawa ni ndugu zangu na mimi nimezaliwa Dar es Salaam na wote nikiwajua nani awaandike?

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole Sana Maalim, jf kuna watu wa kila.aina wakati mwingine ni Bora kukaa.kimya kuliko kuwajibu.

Nime kupm.jambo toka last month please check pm yako.halafu unipe feed back tafadhali.

Peace Be Upon You
 
KHITMA YA SAIGON CLUB YA IDDI SIMBA MSIKITI WA MTORO

Msikiti wa Mtoro kwa baadhi yetu tuliokulia Dar es Salaam unatukumbusha wengi katika wapendwa wetu ambao wametangulia mbele ya haki.

Binafsi namkumbuka mzee wangu, baba yangu na rafiki yangu Sheikh Zubeir Said Chanzi ambae yeye kakua na baba yangu toka udogo wao Mtaa wa Kipata katika miaka ya 40.

Sheikh Zubeir alikuwa habanduki Msikiti wa Mtoro toka ule wa asili uliojengwa na Sheikh Mtoro Mwinyi Mangara hadi ulipovunjwa na kujengwa mara mbili na huu ujenzi wa tatu ukajengwa na Said Salum Bakhersa ambao ndiyo msikiti huu wa fahari uliokuwapo hivi sasa.

Wengi tuna kumbukumbu za Msikiti wa Mtoro wakati wa Sheikh Kassin bin Juma akiwa Imam Mkuu katika miaka ya 1980 wakati Waislam walipitia kipindi kigumu sana na kwa bahati nzuri au mbaya Rais wa Tanzania alikuwa Sheikh Ali Hassan Mwinyi.

Huu ulikuwa wakati wa Barua za Kiuchungaji na ulikuwa pia wakati wa Mihadhara ya Biblia na ulikuwa wakati Sheikh Kassim akitoa hotuba kali za Ijumaa zilizosisimua Waislam.

Huu ulikuwa wakati hata gazeti la Chama na Serikali Uhuru na Mzalendo na Daily News zikimshambulia Mwenyekiti wa chama chenyewe na Rais wa nchi.

Haya hayakupata kutokea wakati rais Nyerere yuko madarakani.

Haya ndiyo yaliyompa nguvu Sheikh Kassim Juma kutumia membar ya Msikiti wa Mtoro kutoa majibu.

Katika moja ya khutba nyingi alizopata kutoa hii moja iliniathiri sana mimi na nimeipa jina, ''Leo Nitataja Majina.''

Sheikh Kassim Juma siku ile alianza hotuba yake kwa kusema kuwa ''nitataja majina.''

Khutba hii Sheikh Kassim alitaja majina kama matatu, Rajab Diwani, Abdul Sykes na Maalim Mohamed Matar na kila mtu akimpa sifa zake alizostahili na uhusiano wake na Mwalimu Nyerere katika historia ya uhuru wa Tanganyika ukimtoa Maalim Matar.

Sheikh Kassim alikuwa bingwa wa kuzungumza na alikuwa akijua namna ya kugusa hisia ya hadhira yake.

Siku ile alimtaja Abdul Sykes siku ya maziko yake na vipi yeye na Mwalimu Nyerere walivyoshiriki katika maziko yale.

Sheikh Kassim siku ile kwa mara ya kwanza aliueleza umma akasema, ''Huyu Abdul Sykes alikuwa mtu wake sana Nyerere.''

Nimekaa pale msikitini mengi yaliyopitika pale yakinirudia.

Kwa hakika msikiti unavutia na Sheikh Mtoro wa Mangara ikiwa Allah atamuonesha msikiti wake ulivyo sasa ataukataa atasema msikiti wake haukuwa hivi msikiti wake ulikuwa kibanda cha udongo, fito, mawe na chokaa.

Nimekaa msikitini pale nakumbuka mengi yaliyopita.

Nakumbuka Iddi Simba pale msikitini akiswali safa ya mbele na akimsikiliza Sheikh Kassim akitoa zile hotuba ambazo kabla hazikupata kutolewa.

Wako wenzake wengi walioukimbia msikiti kwa hofu.

Iddi Simba hakuondoa alikuwapo wakati wote ametulia pale mbele akimsikiliza Sheikh Kassim.

Sheikh Kassim kakamatwa kawekwa jela.
Iddi Simba hakuacha kuja kuswali Mtoro.

Iko siku nikamuuliza kwa nini yeye bado yupo Msikiti wa Mtoro hajaukimbia kama wenzake.

Jibu alilonipa ni kuwa yapo mafunzo ya kujifunza na ipo faida kwa pande zote.

Nikiwa msikitini pale nilimtazama Mzee Mwinyi na nikawa nafikiria shida alizopata wakati wa utawala wake na nilifarajika sana kwa kumuona jinsi alivyokuwa ''relaxed,'' hakika kama nahodha ambae juu ya misukosuko ya bahari alikifikisha chombo salama bandarini.

Nakumbuka wakati huu wa utawala wake baada ya kuwa anashambuliwa hata na vyombo vyake vyenyewe vya Chama na Serikali marehemu Ahmed Saleh Yahya alikuja Dar es Salaam kutoka London tukiwa tunakunywa chai, sambusa na kababu katika mgahawa mmoja katikati ya mji akaniomba kwa siri niandike makala ya kumtetea Rais Mwinyi.

Ahmed Saleh Yahya alikuwa Mhariri wa Africa Events jarida maarufu miaka ile.

Angalia picha iliyowekwa ya makala ambayo niliandika kueleza matatizo ya Tanzania katika kipindi kile.

Lakini haya yote yakapita kwa salama na leo imebakia historia.

Chembelecho Mzee Mwinyi anatuasa tuwe hadithi nzuri kusimuliwa pale tutakapoondoka duniani.

Iddi Simba ni hadithi inayopendeza katika kila sikio.

Allah akubali dua zetu ampokee mzee wetu Iddi Simba na atukutanishe pamoja nae Firdaus.
Wengi wa msikiti wa kwa mtoro walitoka Mtaa mmoja maarufu huko Bujumbura- Burundi ukiitwa Chibitoke. Isie na wewe ukawa ni mrundi kama marehemu idd simba, ponda, Zitto na wote waletao vurugu ya kidini hapa Tanzania
 
Ndjabu...
Mimi nimeombwa nizungumze si kuwa nimezungumza kwa kimbelembele changu.

Imekuwa kawaida kila panapokuwa na shughuli ya Waislam khasa ikiwa ni msiba huwa naombwa nimzungumze marehemu kama nilivyomfahamu.

Nimezungumza katika maziko ya Ally Sykes, Kitwana Kondo na hivi karibuni Iddi Simba.

Halikadhalika nimeandika taazia zao na za watu wengi maarufu wa Dar es Salaam kama Ahmed Rashad Ali, Mohamed Awadh (Chico), Zubeir Mtemvu, Tewa Said Tewa, Bi. Titi Mohamed, Abubakar Tambaza wengi tu.

Nimeandika pia taazia ya Mwalimu Julius Nyerere.

Ni bahati mbaya kuwa hili linakukera lakini nifanyeje na hawa ni ndugu zangu na mimi nimezaliwa Dar es Salaam na wote nikiwajua nani awaandike?

Sent using Jamii Forums mobile app
Umesoma hii:

 
Idd Simba alikuwa Binaadamu kama wengine. Marehemu hasemwi kwa mabaya tuliusiwa! Mzee MS ungependa na 'fraud' za Mzee wetu tuziweke wazi

Ila nikikusoma vizuri Nyerere alikuwa kiongozi mahiri haijapata tokea Tanzani. Toka mazishi ya Sykes na namna alivyodhibiti migawanyiko Tanzania.

Naikubali pia busara ya Abdul Sykes baada ya Uhuru kutosema mengi yanayohusu kabla ya Uhuru. Najua kuna wakati unapitiliza kuongeza chumvi ila nina hakika angekuwepo asingependa hilo

Sent using Jamii Forums mobile app
Platozoom,
Sijaelewa inakuwaje unaniuliza mimi swali hilo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umesoma hii:

Njinjo,
Umesoma hii?:

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maelezo ya hitma ya maisha ya mtu, yanatolewa na mtu - mwanahistoria anayejua umuhimu wa tarehe- aliyeombwa kutoa maelezo, hayana hata tarehe ya kuzaliwa kwa marehemu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kiranga,
Nina namna yangu ya kuandika na kuhadhiri tofauti sana na watu wengine.

Mimi hupenda kuandika na kueleza yale ambayo wengi hawajui.

Haya kwa kawaida hushikwa na watu kuliko tarehe ya kuzaliwa, ana watoto wangapi na maelezo mfano ya hayo.

Nimeanza kumueleza Iddi Simba akiwa mazikoni nyumbani kwa Bi. Mruguru bint Mussa mama yake Ally Sykes kakaa kwenye jamvi na Ally Sykes na Zuberi Mtemvu.

Ally Sykes analaumu nchi imeharibika hakuna mchele wala mafuta ya kupikia.

Zuberi Mtemvu anamjibu kwa kejeli kuwa asilalamike hayo kayataka mwenyewe.

Ally Sykes akamjibu anauliza, "Nyie Congress kumbe hatukuwamaliza bado mpo."

Ally Sykes, Abdul Sykes na Julius Nyerere walikuwa TANU na Mtemvu chama chake Congress.

Kufika hapa nikamleta Iddi Simba kupitia kinywa cha Mtemvu alipomuuliza Ally Sykes, "Huyu Nani?"

"Humjui huyu?" Ally Sykes kashangaa.
"Huyu ni Iddi Simba."

Hii ndiyo staili yangu na wengi wanaipenda.

Baada ya hapo nikaja Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Muslim School aliposoma Iddi Simba nk.


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom