khaa!hata mbele za watoto natetemeka!!

Ahsante sana bro...umenisaidia sana na mimi
Ubarikiwe!!

shule yako kiwango gani? huja wahi kuwa monita, au kilanja, au kufanya morning talk shuleni? vipi hujafanya hata ngojera, maigizo primary hadi secondari? au "John Kisomo"?
Wewe hata ukienda TSJ au British Council kwa sasa hautaweza sababu unaumwa unaitaji tiba.
Dawa ya muda mfupi..
1.soma kichekesho nenda kawaambie watu wako wa karibu, wakicheka, una andika point fanya hivyo anagalu mara 10, kwa watu tofauti vichekesho tofauti.!!
2. Tunga story (ukweli/uongo/matukio ya zamani ya shule) kisha simulia, wape mda watu wakuulize, waelewe, wacheke, kama ni kuchekesha au wasikitike kama ni ya kusikitisha. Unaweza zigawa katika makundi, za kufurahisha, na za kusitikitisha (usizitoe siku moja kwa kundi moja).
3. kama ni mwanaume ukiwa njiani kwenda au kurudi kazini, daladala au chombo chochote cha usafiri, hata kwa mguu msemeshe mwanamke (kama mwanamke msemeshe mwanaume) mfanye aongee nawewe, ( she has to pay attention on YOU) kwa sababu ndo unaanza unaweza ukaanza na maswali madogo madogo kama 5, kisha ukafikisha 50 kwa watu tofauti, ambao hujakutana nao kabla.
Tiba ya muda wa kati
1 .Soma hadithi kisha isimulie kwa kifupi bila kupoteza maana, fanya kila mtu avutiwe aweza kutaka kusikiliza!
2. Ongea peke yako ndani na kujirekodi video/audio kisha baada ya muda sikiliza je unaeleweka unavutia mtu kusikiliza? 3. Angalia filamu, chagua "role model" actor jinsi anavyo ongea kisha na wewe jaribu kumugiza....... ( ila za kibongo sikushauri, kidogo za kinegeria na za kimarekani ( hasa kama ofisi yako inatumia ng'eri)
Jaribu hizo kwanza kisha utaniambia.
wakatabahu!!
 
pole ndugu bt ukiwa tayari kwa mabadiliko it begins with u, mimi kichuochuo ukiniambia leo presentation ntaumwaje hadi zam yangu ipite, bt after that nkaanza jipya practise kila interview nimo hata kama najua cna lengo nayo hiyo kazi, nashukuru now afazali kidogo,jiambie naweza n anza pactise kwa kuongea na watu watu watatu , watano ,kumi na kuendelea
 
habarini,hivi
tatizo hili la kutetemeka na kushindwa kumaliza maelezo unapoongea
mbele ya mtu/watu linasababishwa na nini? na tiba yake ni nini?mi
mwezenu hata kama na hoja nzito huwa na shindwa kuielezea,nikijaribu
kuielezea huwa natetemeka mdomo pia maneno yanakuwa mazito inafikia
hatua na katisha maelezo hafu na kuwa kama sijaeleweka vile mbele ya
hadhira.Hii unitokea hata nikiwa naongea na watoto.


Anza kuongea na mtu yeyote atakaye kuwa karibu yako; hata ukiwa barabarani, kwenye foleni, kituo cha basi, supermarket wewe fungua tuu kinywa chako. Mwanzoni utaona noma lakini wewe endelea tuu, kwani hao ni binadamu wenzako hawata kudhuru kwa kuongea nao.

kwa kuanzia tuu salamu inatosha, hii itakufanya uone kuwa ni kawaida kuongea na watu. Baada ya kuona unajiamini kuongea na mtu yeyote ongeza maneno mawili matatu baada ya salamu ili kuwa na mazungumzo kidogo. Ukifanya mazungumzo na watu 10 usio wajua kwa siku utaona unaanza kujiamini kuongea na kadamnasi.

Ujanja wa kuonge mbele ya watu ni kuwaangalia wote kwa wakati mmoja, sasa kama wewe teyari umesaha jizoesha kuanzisha mazungumzo madogomadogo na watu mbalimbali itakuwa rahisi hata kuanza hotuba yako na zungumzo ili ukisha zoea hadhira unaendelea na ajenda yako.
 
Pole unahitaji msaada wa kiroho okoka kwa miezi sita tu tatizo litakwisha
 
shule yako kiwango
gani? huja wahi kuwa monita, au kilanja, au kufanya morning talk
shuleni? vipi hujafanya hata ngojera, maigizo primary hadi secondari? au
"John Kisomo"?
Wewe hata ukienda TSJ au British Council kwa sasa hautaweza sababu
unaumwa unaitaji tiba.
Dawa ya muda mfupi..
1.soma kichekesho nenda kawaambie watu wako wa karibu, wakicheka, una
andika point fanya hivyo anagalu mara 10, kwa watu tofauti vichekesho
tofauti.!!
2. Tunga story (ukweli/uongo/matukio ya zamani ya shule) kisha simulia,
wape mda watu wakuulize, waelewe, wacheke, kama ni kuchekesha au
wasikitike kama ni ya kusikitisha. Unaweza zigawa katika makundi, za
kufurahisha, na za kusitikitisha (usizitoe siku moja kwa kundi moja).
3. kama ni mwanaume ukiwa njiani kwenda au kurudi kazini, daladala au
chombo chochote cha usafiri, hata kwa mguu msemeshe mwanamke (kama
mwanamke msemeshe mwanaume) mfanye aongee nawewe, ( she has to pay
attention on YOU) kwa sababu ndo unaanza unaweza ukaanza na maswali
madogo madogo kama 5, kisha ukafikisha 50 kwa watu tofauti, ambao
hujakutana nao kabla.
Tiba ya muda wa kati
1 .Soma hadithi kisha isimulie kwa kifupi bila kupoteza maana, fanya
kila mtu avutiwe aweza kutaka kusikiliza!
2. Ongea peke yako ndani na kujirekodi video/audio kisha baada ya muda
sikiliza je unaeleweka unavutia mtu kusikiliza? 3. Angalia filamu,
chagua "role model" actor jinsi anavyo ongea kisha na wewe jaribu
kumugiza....... ( ila za kibongo sikushauri, kidogo za kinegeria na za
kimarekani ( hasa kama ofisi yako inatumia ng'eri)
Jaribu hizo kwanza kisha utaniambia.
wakatabahu!!

Sikuwahi kuwa kiongozi,nilikuwa siendi assemble nikijua ni zamu yangu kutoa morning speach, ASANTE SANA KWA USHAURI MZURI UBARIKIWE.
 
Sikuwahi kuwa kiongozi,nilikuwa siendi assemble nikijua ni zamu yangu kutoa morning speach, ASANTE SANA KWA USHAURI MZURI UBARIKIWE.

Okoka basi hata miezi 6 ukatupigia neno kwenye vituo vya daladala au ndani ya bus utakuwa umeiva
 
Hivi swali lisilo na matusi kwa nini lijibiwe na matusi? Ina maana wewe haujawai kushuhudia mtu mwenye tatizo kama hili?
Kama unategemea kigezo cha kuwa na kazi kama ushuhuda wa kutokuwa na tatizo, na kushauri utembee ili ujionee!

Kuna watu wana kazi nzuri na lakini bado wana hili tatizo, kusima mbele za watu wanashindwa na kuongea mbele za watu ni tatizo lakini ukimkuta ofisini anafanya kazi vizuri!
basi hyo kazi uliyonayo ni ya kutumia mwili ktk utendaji wake au uliipata kwa kuvua chupi au kutoa 0713......
 
Pole sana mkuu! Me kwangu naona hilo tatizo lako linatibika kabisa hata bila kwenda kwa wataalum,
*hebu jaribu kujiamini kwanza kwa kile unacho kiongea!

*jaribu kuwa unajitoa kuongea mbele za watu mara kwa mara nadhani tatizo ni uoga tuu!

Usijali ukisha jizoesha kuongea mbele za watu tatizo litakwisha bila wasi wasi!
 
basi hyo kazi uliyonayo ni ya kutumia mwili ktk utendaji wake au uliipata kwa kuvua chupi au kutoa 0713......

Unaonekana ni bingwa wa kufanya hayo uliyoorodhesha hapo!!wewe ni punguani!!namaanisha pumbavu flani lisilo na adabu wala lisilojitambua,kama anafanya kazi ya zege ulitegemea apewe interview ipi? Je kama mwajiri wake karidhika na mtazamo na cv yake na kuamua kumwajiri bila interview wewe ni nani hadi uhoji jambo lisilokuhusu?umeniharibia siku kabisa kwa utumbo ulioandika hapo!!mods nao sijui wako wapi.
 
habarini,hivi
tatizo hili la kutetemeka na kushindwa kumaliza maelezo unapoongea
mbele ya mtu/watu linasababishwa na nini? na tiba yake ni nini?mi
mwezenu hata kama na hoja nzito huwa na shindwa kuielezea,nikijaribu
kuielezea huwa natetemeka mdomo pia maneno yanakuwa mazito inafikia
hatua na katisha maelezo hafu na kuwa kama sijaeleweka vile mbele ya
hadhira.Hii unitokea hata nikiwa naongea na watoto.Leo nimelazimika
kuomba msaada humu kutokana kwamba kazini nimepewa kitengo ambacho
kinahitaji kuzungumza kwenye vikao nilitaka kukataa lakini nikashindwa
kukataa nilikaa kimya ingawa moyoni sikupenda kabisa hilo jukumu sasa
hata kazi naiona chungu.ushauri wako tafadhali.


no options get ganja and get go, ushauri mwingine nje ya huu ni upuuzi.
 
Matatizo ya kununua vyeti. kila kitu unajishtukia. Ushauri kwanza jaribu kuelewa issues.

Andika kwenye karatasi kile unachotaka kuongea. Pangilia issues.
Pitia makabrasha ya mikutano mapema na kuekewa nini kitaongelewa.

Tafuta kijiwe weekend uwe unashinda hapo unapiga story
 
Mwana, usiwasikilize baadhi ya vichaa humu ndani. Mimi niko chuo nafanya kazi kwenye research institute maarufu US. Haya mambo sio ajabu. Inaitwa anxiety/panic attack. Soma hapa kwa maelezo zaidi: Panic attack - Wikipedia, the free encyclopedia

Mimi ni mtu ambaye nimefaulu vizuri na siku zote niliambiwa kuwa nina akili sana. Lakini mpaka leo hii bado nakuwa anxious hata kama naongelea jambo dogo tu mbele ya watu wawili watatu. Cha ajabu utakuta pengine najua kuhusu kitu fulani kuliko mtu yoyote na bado huwa nakuwa anxious. Nimekuwa nikiongea mbele ya watu kwa miaka mingi tu (tokea utotoni). Muda mwingine watu wanashangaa maana wanafikiri labda ni ugonjwa mbaya. Usihofu, duniani kuna watu wengi tu wanashida kama yako (IMDb: Celebrities with a history of depression and/or anxiety - a list by johanna-khristina). Ili mradi unajua kuwa hauna cha kuhofia, basi shikilia usukani na kaza mwendo. Mimi mwenyewe juzi nilikuwa naongelea thesis yangu mbele ya watu. Kama kawaida dakika tano za mwanzo moyo ulikuwa unapiga resi balaa na nilikuwa natetemeka. Ila baada ya muda huwa natulia halafu kila kitu kinakuwa shwari. Hebu sikiliza hii talk ya huyu professor wa harvard kuhusu shida alizopitia kama zako tu: Amy Cuddy: Your body language shapes who you are - YouTube. Ukicheki hapo mwishoni, unaambiwa kuwa, weka pose ya kuwa assertive. Kabla ya kufanya talk yoyote, nenda bafuni halafu utanue mikono huku ukijiangalia kwenye kioo. Ukifika kwenye talk yenyewe, usifikirie sana kuhusu your body language. Just TALK!
 
Mwana, usiwasikilize baadhi ya vichaa humu ndani. Mimi niko chuo nafanya kazi kwenye research institute maarufu US. Haya mambo sio ajabu. Inaitwa anxiety/panic attack. Soma hapa kwa maelezo zaidi: Panic attack - Wikipedia, the free encyclopedia Mimi ni mtu ambaye nimefaulu vizuri na siku zote niliambiwa kuwa nina akili sana. Lakini mpaka leo hii bado nakuwa anxious hata kama naongelea jambo dogo tu mbele ya watu wawili watatu. Cha ajabu utakuta pengine najua kuhusu kitu fulani kuliko mtu yoyote na bado huwa nakuwa anxious. Nimekuwa nikiongea mbele ya watu kwa miaka mingi tu (tokea utotoni). Muda mwingine watu wanashangaa maana wanafikiri labda ni ugonjwa mbaya. Usihofu, duniani kuna watu wengi tu wanashida kama yako (IMDb: Celebrities with a history of depression and/or anxiety - a list by johanna-khristina). Ili mradi unajua kuwa hauna cha kuhofia, basi shikilia usukani
mashaallah!
 
poleni kwa tatizo lako,kabla ya kuongea panga point kwenye paper , wakatiwa kuongea soma point harafu ndiyo anzakuongea , pia ongea kwa polepole na kwa msisitizo , ongea kwa kujiamini. Honera sana inaonekana unahekima na busara kwani unashukuru kwa kila moja hata walio changia kwa matusi na kejeli. mungu amekupa busara kubwa sana lakini amekunyima kujiamini yakupasa uanzekujiaminisha wewe mwenyewe mungu hawezi kukupa kila kitu . Hatamimi ninatatizo kama lakwako , nimejifunza na ninapambana nalo na ninaamini nitafanikiwa tu.
 
Pole kwa tatizo na najua jinsi linayokusmbua.
Kuna vitu katika hai uliyo nayo kama personality disorder na self esteem. Hakika ni mada ndefu sana ambazo haziwezi kuelezeka kwa kurasa moja au mbili.

Ninachotaka uelewe ni kuwa katika personality disorder kuna wengine ambao hutaka kuwa sahihi (perfectionist). Ingawa wao ni tofauti nawewe nao pia wanasehemu yao ya usumbufu kama ilivyo kwako.

Ningekushauri baadhi ya mambo
1. Jenga hali ya juiamini na kuamini kuwa unachokifanya ni sahihi.
Amini kuwa hata kama s sahihi bado una nafasi ya kusahihisha.
Kwa mfano, ukionge na watoto jiamini kuwa wewe ndiye mzazi na unajua kuliko wao. Kama ukikosea hata kuomba samahani ni sehemu ya wewe kuwafundisha wao tabia njema na hivyo kila utakachofanya kiwe sawa au si sawa bado una nafasi ya kukifanya sawa.

2. Usiogope na kuhisi kuwa utakapokuwa unafanya au unasema jambo fulani utaudhi watu. Jiaminishe kuwa lugha yako na uwezo wako wa kujenga hoja ni kwa mujibu wa uelewa wako, na kwamba wenzako wana mitizamo tofauti ambayo haiwafanyi wawe sahihi bali kila mtu yu sahihi.

3. Tulia uwe composed and calm ukijua kuwa unachotaka kuongea umekifanyia tathmini na ni sahihi.

4. Jaribu sana kuingiza utani mzuri (humour) kabla ya kuongea jambo. Usiwe rigid kwamba unataka kuongea kitu muhimu kila wakati. Kabla ya kuongea fanya utani kidogo ili mwili uwe relaxed.
Utani huo wa ku relax body sio ofisini tu hata nyumbani mbele ya watoto.
Mfno, ita mtoto wako na kabla hujaeleza hoja yako mtafutie kitu cha kiutani. Waambie wakati wa kupitia homework umefika, kila mmoja aje mahakamani na kidhibiti kuwa amemaliza homework.......
baada ya hapo utakuwa na nafasi ya kujenga hoja unayoikusidia.
 
Habari wakuu,

Nina tatizo la kutetemeka na kushindwa kumaliza maelezo unapoongea mbele ya mtu/watu linasababishwa na nini? na tiba yake ni nini? Mi mwezenu hata kama na hoja nzito huwa na shindwa kuielezea, nikijaribu kuielezea huwa natetemeka mdomo pia maneno yanakuwa mazito inafikia hatua na katisha maelezo hafu na kuwa kama sijaeleweka vile mbele ya hadhira.

Hii unitokea hata nikiwa naongea na watoto.Leo nimelazimika kuomba msaada humu kutokana kwamba kazini nimepewa kitengo ambacho kinahitaji kuzungumza kwenye vikao nilitaka kukataa lakini nikashindwa kukataa nilikaa kimya ingawa moyoni sikupenda kabisa hilo jukumu sasa hata kazi naiona chungu.ushauri wako tafadhali.
Ni PM namba yako, natoa training ya Public speaking na jinsi ya kucope na situation uliyonayo.
 
Back
Top Bottom