Key ponits hotuba ya Jakaya kesho CCM Kirumba

Sangarara

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
13,100
5,649
1. Kuwasilisha malalamiko yake kutokana na mgomo wa Madaktari.
2. Kueleza masikitiko yake na kuvilaumu vyombo vya habari juu ya swala la Posho za wabunge zinavyoandikwa.
Hapa ataelezea namna posho za wabunge wa mabunge mengine zilivyo nono lakini wananchi hawalalamiki.
3. Kutoa pole kwa wahanga wa mafuriko Dar es Salaam na kuwaelekeza viongozi wa ccm mwanza kuandaa orodha
ya wananchi wote ambao walihathirika na mvua zilizonyeesha kwa muda mrefu mwishoni mwa mwaka jana ili na
wao wapatiwe misaada kama wale wa Dar.
4. kuelezea namna stimulus Package (3trilion) alizoapprove yeye kama mwenyekiti wa chama zilivyosaidia kilimo cha
pamba kisidhoofishwe na mtikisiko wa uchumi wa mwanza 2008
5. Kuagiza wanaccm wasiwe wanyonge sababu wao ndio wako madarakani.
6. Kuahidi Majimbo yote mawili ya Ilemela na Nyamagana kurudi CCM mwaka 2015.
7. Kuwaasa wanamwanza kujiepusha na ubaguzi kwa misingi ya imani za kidini na itikikadi za vyama.
8. Kuahidi ushindi wa kushindo kwa ccm kwenye uchaguzi mdogo uko Arumeru.
9. Kuelezea namna serikali yake inavyotekeleza ilani yake ya uchaguzi kikamilfu hasa katika uaandaaji wa katiba mpya
na kuwaasa wanaccm kushiriki kwa dhati bila uoga badala ya kuwaachia wana CDM (hapa ataitaja kwa umakini sana)
10. Kuwaasa wana mwanza kwamba maendeleo hayaji kwa maandamano.
11. Kuelezea namna mfumuko wa bei unavyoziathiri nchi nyingi zaidi duniani na tanzania tu.
12. Kuwaasa Madaktari wasimsikilize DR ulimboka sababu anatumiwa na wanasiasa (hapa ulimboka atashambuliwa vibaya sana)
13. n.k
 
ngoja tusubiri tuone

wanajf
Dondoo za hotuba ya jk kesho ccm kirumba ni kazi za wasaidizi wake na yeye mwenyewe. Kutayarisha hotuba ni kazi ya wasaidizi wake na yeye mwenyewe. Kama makundi yote mawili hayana cha kusema basi. Nawaombeni sana wana JF tusiruhusu na tusitoe nafasi ya kuwa-spoon-feed watu hawa. Tuendelee kuganga yale yanayotuhusu kama thinkers. Tuwaache wafu wazikane wenyewe.
 
Ni rahisi sana kukisia JK atasema nini kwasababu ya nature za hotuba zake,hazina mashiko.Mimi uwa nasema hotuba nyingi za wanasiasa wa sasa pamoja na JK mwenyewe hazina falsafa,na ndio maana haziishi(hazidumu kwenye fikra za watu),Mtu kama mwalimu Nyerere,Mandela,Lumumba nk walikuwa wanatoa hotuba zenye kujaa falsafa na sio matukio...Sasa JK mara nyingi uwa anatoa hotuba kulingana na matukio,na kwa hiyo hotuba zake uwa zinajaa malalamiko,uongo wa kufananisha mambo na nchi nyingine ili kuhalalisha uzembe wa serikali yake.Hotuba gani ya mwanasiasa ya masaa 2 haina hata nukuu ya mwanafalsafa hata mmoja,hata Quran ameshindwa kuinukuu? au Biblia?

Hotuba ya leo ni rahisi kukisia atasema nini,tena hata maneno atakayo tumia maana uwa hana falsafa zaidi ya kujaza matukio yaliopo.
 
Ni kweli kama mtu unaangalia hutuba zake mara kwa mara utajua ataongea nini! Msishangae akaongea yote hapo juu au sio chini ya saba kati ya kumi na moja hapo juu
 
Mawazo pevuka na ya kujenga hutolewa katika mazingira tulivu..hw are you expect our king to addres the issue which people touch almost eachone of us while the environment is not on his side.?our president hana utulivu kwani kila mtanzania ana asira nae hata atakaokuwa anawautubia utawaona nyuso zao...ni ngumu mtanzania wa leo kudanganywa na hotuba zisizokuwa na matumaini ya kesho kama mtanzania...people are after wayforward,solutions of their problems and not to hear complain...
 
1. Kuwasilisha malalamiko yake kutokana na mgomo wa Madaktari.
2. Kueleza masikitiko yake na kuvilaumu vyombo vya habari juu ya swala la Posho za wabunge zinavyoandikwa.
Hapa ataelezea namna posho za wabunge wa mabunge mengine zilivyo nono lakini wananchi hawalalamiki.
3. Kutoa pole kwa wahanga wa mafuriko Dar es Salaam na kuwaelekeza viongozi wa ccm mwanza kuandaa orodha
ya wananchi wote ambao walihathirika na mvua zilizonyeesha kwa muda mrefu mwishoni mwa mwaka jana ili na
wao wapatiwe misaada kama wale wa Dar.
4. kuelezea namna stimulus Package (3trilion) alizoapprove yeye kama mwenyekiti wa chama zilivyosaidia kilimo cha
pamba kisidhoofishwe na mtikisiko wa uchumi wa mwanza 2008
5. Kuagiza wanaccm wasiwe wanyonge sababu wao ndio wako madarakani.
6. Kuahidi Majimbo yote mawili ya Ilemela na Nyamagana kurudi CCM mwaka 2015.
7. Kuwaasa wanamwanza kujiepusha na ubaguzi kwa misingi ya imani za kidini na itikikadi za vyama.
8. Kuahidi ushindi wa kushindo kwa ccm kwenye uchaguzi mdogo uko Arumeru.
9. Kuelezea namna serikali yake inavyotekeleza ilani yake ya uchaguzi kikamilfu hasa katika uaandaaji wa katiba mpya
na kuwaasa wanaccm kushiriki kwa dhati bila uoga badala ya kuwaachia wana CDM (hapa ataitaja kwa umakini sana)
10. Kuwaasa wana mwanza kwamba maendeleo hayaji kwa maandamano.
11. Kuelezea namna mfumuko wa bei unavyoziathiri nchi nyingi zaidi duniani na tanzania tu.
12. Kuwaasa Madaktari wasimsikilize DR ulimboka sababu anatumiwa na wanasiasa (hapa ulimboka atashambuliwa vibaya sana)
13. n.k


sijaona la msingi hapo hata moja, ama kweli magamba yamefika kiunoni
 
Back
Top Bottom