Kesi za EPA................

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Hukumu ya Maranda na EPA yaiva


na Happiness Katabazi


amka2.gif
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, imesema Aprili 29 mwaka huu itatoa hukumu ya kesi ya wizi wa sh bilioni 1.8 katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kwenye Benki Kuu ya Tanzania (BoT), inayomkabili Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rajabu Maranda na mpwa wake, Farijala Hussein.
Jopo la mahakimu wakazi linaloongozwa na Saul Kinemela, Focus Bambikya na Elvin Mugeta, lilisema limefikia uamuzi huo baada ya wakili wa utetezi Majura Magafu kuiambia mahakama hiyo kuwa wamefunga ushahidi wao na Naibu Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, Stanslaus Boniface na Ben Lincoln kueleza kazi iliyobaki ni kwa mahakama kutoa hukumu yake.
Hakimu Kinemela alisema kesi hiyo ilifunguliwa rasmi Novemba 4 mwaka 2008, jopo hilo limeweza kusikiliza ushahidi uliotolewa na pande zote mbili na kwamba hivi sasa wanaenda kuandaa hukumu yake.
Kwamba kesi hiyo itakuja kutajwa Februari 25 na Aprili 29 mwaka huu, ndiyo jopo hilo litatoa hukumu yake.
Hiyo ndiyo kesi pekee ambayo imekaribia kufikia hatua ya hukumu kuliko kesi nyingine za EPA zilizofunguliwa mfululizo Novemba 4, mwaka 2008.
 
Hizi kewsi jamii kamwe haitazielewa kama zinalenga ya kutenda haki kama watendaji wakuu kwenye hayo mabenki hawashitakiwi kwa uzembe na kwa kutowajibika...........................tunataka kuona nyangumi ndiyo wanatinga mahakamani na wala siyo dagaa..............
 
Back
Top Bottom