Ndevu si Mzigo,
Uko sahihi mheshimiwa.
Wahenga walisema ''SIKIO LA KUFA HALISIKII''!
CCM wameamua KUJIMALIZA WENYEWE KI AINA.Kwa akili finyu waliyo nayo CCM na serikali yake wanafikiri kuwa WAKIWANYANG'ANYA CHADEMA MAJIMBO YOTE MUHIMU KWA NJIA YA MAHAKAMA BASI CHADEMA ITAPOTEZA NGUVU NA UMAARUFU ILIO NAO KWA WATANZANIA KWA SASA. This is a big mistake for Magambas!
Naweza ku-predict kuwa Jimbo la Ubungo linaweza kuwa wazi kuanzia leo baada ya Hukumu itakayosomwa na Jaji ambaye ni Kibaraka wa CCM.Naweza kuona kuwa hukumu ya kesi hii itakuwa kama ile ya G.Lema kule Arusha. Kwamba tayari hukumu ilishapangwa ya kumvua Ubunge J.J.Mnyika ili jimbo liwe wazi.
Tunajua tangu baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2010,CCM hawana raha na hawapati usingizi baada ya majimbo muhimu kwenye majiji ya Arusha mjini,Mwanza(Nyamagana na Ilemera),Dar(Ubungo na Kawe) na Mbeya. Kwa vile haya yalikuwa ni maeneo ambayo CCM walikuwa wakidhani ni ngome zao basi wameamua kutaka kuyarudisha mikononi mwao kwa hila kupitia mlango wa nyuma yaani MAHAKAMA!!!Kwa ujinga wao CCM wanafikiri wakifanya hivi basi wanaweza kushinda Chaguzi ndogo kwa kutumia RAFU/MCHEZO MCHAFU ili tu majimbo hayo yawe chini ya CCM! Wameshindwa kusoma alama za nyakati kwamba kwa sasa Watanzania HAWAWEZI TENA KUKUBALI USHINDI WA GHILBA. CCM ni mashuhuda wa kile kilichotokea Arumeru East. Tunajua waliweka kila mbinu na mikakati ya kutaka kuchukua jimbo hilo ikiwemo KUUA WATU,KUIBA KURA/KUGHUSHI NA HONGO, lakini bado Wananchi wakasema NO TO CCM!
Kwa hukumu hii ya leo tutegemee lolote.