Kesi ya Kitilya, Sioi na Shose Sanare kutajwa tena June 02, 2016

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Ndugu wanaJF

Ile kesi inayo wakabili aliyekuwa kamishna mkuu Mstaafu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya sambamba na Waliokuwa Wafanyakazi wa Benki ya StanBic Tanzania, ndugu Sioi Sumari na Bi.Shose Sanare

Leo imepangwa kutajwa June 2 2016 na watuhumiwa wamerudishwa tena rumande kusubiri kesi hiyo itakaposomwa tena.

a0ce5c61-206e-446c-b9f8-6e41c7155421.jpeg


Ikumbukwe kabla ya leo: Washitakiwa hao wanaokabiriwa na mastaka nane likiwemo la utakatishaji Fedha kiasi cha Dola za Marekani milioni 6, ili kufanikisha mkopo kutoka Benki ya Stanbic kwenda Serikalini, walifikishwa Mahakamani hapo leo kusikiliza keshi yao, na hapo siku za nyuma washitakiwa hawa walifanikiwa kufutiwa Shitaka moja la kutakatisha Fedha kati ya nane yaliyokuwa yakiwakabili, ambapo Washitakiwa hao walisomewa kufutwa kwa shitaka hilo kwa madai ya kukosa Vidhibitisho.

Baada ya kufutiwa shitaka hilo, DPP aliwasilisha hati ya mapendekezo ya kukata rufaa ya kupinga uamuzi wa kufuta shitaka namba nane la utakatishaji Fedha linalowakabili watuhumiwa hao, ambapo zoezi la dhamana liligonga mwamba na Washitakiwa hao wamerudishwa rumande.
 
Maskini lowassa na kundi lake hapa jela mi mia kwa mia
 
Maskini lowassa na kundi lake hapa jela mi mia kwa mia


hapo siku za nyuma washitakiwa hawa walifanikiwa kufutiwa Shitaka moja la kutakatisha Fedha


☝☝☝☝☝☝☝☝hapo ndo ulikuwa msingi wa kesi ndo mana dpp anahangaika jela inaota mbawa hapo wanamvuta mtu golini kes haipo ndugu.
 
Mmh DPP yupo serious, naona amedhamilia kuwafunga hawa jamaa, walao huyo binti wangemtoa wakati wanaendea na mjadala wao wa kisheria, binti wa watu wanamzeesha bure jamani
 
Mmh DPP yupo serious, naona amedhamilia kuwafunga hawa jamaa, walao huyo binti wangemtoa wakati wanaendea na mjadala wao wa kisheria, binti wa watu wanamzeesha bure jamani
wanamzeesha nini wakati kupiga dili anataka. wacha anyee debe ndio wengine waogope ufisadi.
 
Dhamana ni haki ya mtuhumiwa.kuendelea kuwanyima dhamana ni kukiuka haki za msingi za washtakiwa.
 
wawafunge maisha tu wameiba pesa nyingi sana zilitosha kununua madawa hospitalini
 
hawa wametolewa kama scape goats tu.

Watoaji na wapokeaji wapo nje ila facilitators ndo wanakaziwa.

Anyways maisha bila unafiki hayaendi.
 
Ndugu wanaJF

Ile kesi inayo wakabili aliyekuwa kamishna mkuu Mstaafu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya sambamba na Waliokuwa Wafanyakazi wa Benki ya StanBic Tanzania, ndugu Sioi Sumari na Bi.Shose Sanare

Leo imepangwa kutajwa June 2 2016 na watuhumiwa wamerudishwa tena rumande kusubiri kesi hiyo itakaposomwa tena.

a0ce5c61-206e-446c-b9f8-6e41c7155421.jpeg


Ikumbukwe kabla ya leo: Washitakiwa hao wanaokabiriwa na mastaka nane likiwemo la utakatishaji Fedha kiasi cha Dola za Marekani milioni 6, ili kufanikisha mkopo kutoka Benki ya Stanbic kwenda Serikalini, walifikishwa Mahakamani hapo leo kusikiliza keshi yao, na hapo siku za nyuma washitakiwa hawa walifanikiwa kufutiwa Shitaka moja la kutakatisha Fedha kati ya nane yaliyokuwa yakiwakabili, ambapo Washitakiwa hao walisomewa kufutwa kwa shitaka hilo kwa madai ya kukosa Vidhibitisho.

Baada ya kufutiwa shitaka hilo, DPP aliwasilisha hati ya mapendekezo ya kukata rufaa ya kupinga uamuzi wa kufuta shitaka namba nane la utakatishaji Fedha linalowakabili watuhumiwa hao, ambapo zoezi la dhamana liligonga mwamba na Washitakiwa hao wamerudishwa rumande.
haki ichukue mkondo wake
 
Back
Top Bottom