Kesho ndio Kesho Ligi Kuu Tanzania (TPL).

Kingsmann

JF-Expert Member
Oct 4, 2018
4,448
16,314
KESHO WATAUANA LIGI KUU

Bingwa wa ligi kuu Tanzania bara msimu huu ameshajulikana, sasa hivi vita imehamia bondeni ambako timu zipo kwenye harakati za kuhakikisha zinabaki mwenye ligi kwa ajili ya msimu ujao.
.
Msimu huu timu mbili za chini (nafasi ya 19 na 20) zinashuka daraja moja kwa moja. Timu nyingine mbili zitakazomaliza (nafasi ya 17 na 18) zitacheza play-off na timu 4 (zilizomaliza nafasi ya 2 na 3 kwenye Kundi A na B) ligi daraja la kwanza.
.
Katika mechi za play-offs, timu mbili zitafuzu kucheza ligi kuu msimu ujao zikijumuika na mbili zilizofuzu moja kwa moja kutoka Kundi A na B za ligi daraja la kwanza.

Ni African Lyon pekee ndio timu ambayo tayari imeshuka daraja hadi sasa, kuna timu nyingine moja ambayo itaungana na Lyon halafu mbili zitakazomaliza nafasi ya 17 na 18 zitacheza play-off.
.
Ukiangalia msimamo, kuanzia nafasi ya 12 kushuka chini, kila timu haiko salama, ikitokea inapoteza mchezo wa mwisho basi inaweza kujikuta inacheza play-off kama wapinzani wake wanapata matokeo ya ushindi.
.
Ratiba inazikutanisha timu nyingi ambazo zinapigana kubaki kwenye ligi, wote wakiwa wanahitaji ushindi. Mechi zinazozihusisha timu ambazo zipo nafasi ya 12 hadi 19 zinamaana kubwa lakini utamu zidi unakuwa pale mechi zinakututanisha timu zote zinazotafuta nafasi ya kubaki kwenye ligi.

MECHI ZA MWISHO: #LigiKuuTanzaniaBara

Mtibwa Sugar vs Simba SC

Yanga SC vs Azam FC

Coastal Union vs Singida United

Mwadui FC vs Ndanda SC

JKT Tanzania vs Stand United

Ruvu Shooting vs Alliance FC

Mbeya City vs Biashara United

Mbao FC vs Kagera Sugar

Tanzania Prisons vs Lipuli FC

African Lyon vs KMC FC.

shaffihdauda_-20190527-0001.jpeg


Credit:Shaffihdauda
 
Sina wasiwasi na timu za mkoa wa Mbeya. Piga ua Tanzania prisons lazima atamzaba Lipuli fc. kazi ipo kwa Mecky Mexime na chama lake japokuwa Mexime anapaswa kubaki ili aendelee kuwashughulikia mikia.
kesho balaa kubwa litakuwa hasa hasa kwenye mechi mbili. JKT TANZANIA vs Stand united, pia Mbao fc vs Kagera sugar.
 
KESHO WATAUANA LIGI KUU

Bingwa wa ligi kuu Tanzania bara msimu huu ameshajulikana, sasa hivi vita imehamia bondeni ambako timu zipo kwenye harakati za kuhakikisha zinabaki mwenye ligi kwa ajili ya msimu ujao.
.
Msimu huu timu mbili za chini (nafasi ya 19 na 20) zinashuka daraja moja kwa moja. Timu nyingine mbili zitakazomaliza (nafasi ya 17 na 18) zitacheza play-off na timu 4 (zilizomaliza nafasi ya 2 na 3 kwenye Kundi A na B) ligi daraja la kwanza.
.
Katika mechi za play-offs, timu mbili zitafuzu kucheza ligi kuu msimu ujao zikijumuika na mbili zilizofuzu moja kwa moja kutoka Kundi A na B za ligi daraja la kwanza.

Ni African Lyon pekee ndio timu ambayo tayari imeshuka daraja hadi sasa, kuna timu nyingine moja ambayo itaungana na Lyon halafu mbili zitakazomaliza nafasi ya 17 na 18 zitacheza play-off.
.
Ukiangalia msimamo, kuanzia nafasi ya 12 kushuka chini, kila timu haiko salama, ikitokea inapoteza mchezo wa mwisho basi inaweza kujikuta inacheza play-off kama wapinzani wake wanapata matokeo ya ushindi.
.
Ratiba inazikutanisha timu nyingi ambazo zinapigana kubaki kwenye ligi, wote wakiwa wanahitaji ushindi. Mechi zinazozihusisha timu ambazo zipo nafasi ya 12 hadi 19 zinamaana kubwa lakini utamu zidi unakuwa pale mechi zinakututanisha timu zote zinazotafuta nafasi ya kubaki kwenye ligi.

MECHI ZA MWISHO: #LigiKuuTanzaniaBara

Mtibwa Sugar vs Simba SC

Yanga SC vs Azam FC

Coastal Union vs Singida United

Mwadui FC vs Ndanda SC

JKT Tanzania vs Stand United

Ruvu Shooting vs Alliance FC

Mbeya City vs Biashara United

Mbao FC vs Kagera Sugar

Tanzania Prisons vs Lipuli FC

African Lyon vs KMC FC.

View attachment 1109571

Credit:Shaffihdauda
Mkuu Kingsmann,FC maana yake ni Football Club na SC ni Sports Club, ya kwanza ikimaanisha ni Club ya Mpira wa Miguu na ya pili ikimaanisha Club ya Michezo yaani zaidi ya Mchezo Mmoja.
Swali ni je,katika Tanzania ni Vilabu vitatu pekee yaani Simba,Ndanda na Yanga vinavyojiendesha kwa michezo zaidi ya mmoja ambao ni mpira wa miguu?
Je,ni kweli Ndanda chama lao linamiliki michezo zaidi ya mmoja tuseme Volleyball,Basketball,Netball nk?
Mjuzi atuambie.
 
Back
Top Bottom