Kero za Serikali hii

Ichwampaka

Senior Member
Nov 19, 2018
134
109
Wanaharakati,
Kuna inshu moja inanikera sana katika serikali ya awamu hii mpaka nataka nihamie vyama vya upinzani. Kila unapopita ni ujenzi wa miundombinu unaendelea hadi imekuwa kero. Leo najipitia njia ya makaburini Sinza mara pap imefungwa ujenzi unaendelea, nikazunguka njia ya Bagamoyo Mwenge, hovyo kabisa, ujenzi unaendelea, nikatoboa kimtindo njia ya Kijitonyama kule ujenzi unaendelea hivi ni haki kweli? kila mahali kunaboreshwa tu, wala wananchi hatujaombwa hata kuchangia.

Nikatokea njia ya Mtogole duu hawana hata aibu barabara haina hata mashimo ni lami tu unateleza, hivi ni sawa kweli? Kule ubungo kuna dudu moja la ajabu linajengwa sijawahi kuliona; hivyo haya sio matumizi mabaya ya fedha zetu kweli? Kwanza hizi hela mnapata wapi? Corporate tax ni ile ile tena sehemu nyingine mmepunguza hadi 25%, VAT ni ile ile, national budget support si nasikia kama haipo kabisa? mbona Rais haendi nje ''kutembeza bakuli'' mnapata pesa wapi watu nyie?

Nasikia hata huko porini nako hawalali ni kazi kwenda mbele, ndugu yangu yupo Sanga Sanga huko anasema hawalali eti ''Standi Geji''inajengwa, jamani tuoneeni huruma. Sasa funga kazi ni huko ''Stella Joji'' nasikia maji yanakusanywa ili kuzalisha umeme nasikia umeme utakuwa wa kumwaga hata sigara tutakuwa tunawashia umeme, taa, vibatari, majenerata yatapelekwa makumbusho.

Halafu hayo madege mabomba my dear hayo, na sijui mabasi ya angani (ea basi) ukiangalia angani kila dakika 20 yanapita, nyie serikali vibaya hivyo wenzenu hata jua hatulioni vizuri sababu ya anga kujaa hayo mabomba my dear na ea basi.

Serikali tunaomba mtuondelee hizi kero, nawakilisha
 
Soma hiyo
Screenshot_20190928-102901_Twitter.jpeg
 
Huo ndio ufisadi mkubwa unaopigiwa kelele na wapinzani! Hujasikia wanahoji trilioni moja nukta tano? Wanadai imeenda huko ulipopataja na inawakera sana!
 
Ningependa tu kufahamu mtoa mada kama unajitegemea au bado unaishi kwa wazazi wako. Na kama unaishi kwa wazazi, basi una kila sababu ya kuja na huu uzi wako.

Ila kama unajitegemea, unafanya kazi au shughuli yoyote ile halali ya kukuingizia kipato; basi utakubaliana na mimi ya kwamba unalipa kodi, na hivyo ni jukumu la kawaida kabisa kwa serikali yoyote ile kujenga miundombinu ya kila aina kwa ajili ya wananchi waliowachagua kupitia kodi zao wanazotozwa kila dakika/saa/siku/wiki/mwezi/mwaka, nk.

Hivyo ni vyema ukaachana na hiyo mbinu yako mpya ya kusifia vitu vya kawaida kabisa. Hakuna awamu iliyokuwepo madarakani na haikujenga hiyo miundombinu.
 
Umekuja kusifia kijanja boya wewe, mwambieni hivi baba yenu watu wanataka pesa mtaani mzunguko wa fedha uwe mzuri wapate mahitaji yao muhimu, food, clothing and shelter, waweze kusomesha, kujitibu, kupata huduma bora ya afya, elimu wao na familia zao, hata ajenge nini watu bila kupata mahitaji muhimu hawamwelewi labda nyinyi praise team.
 
Unaulizwa pesa zinatoka wapi?

Hujasikia maduka ya kubadilishia fedha kufungiwa kwa uda usiyojulikana...

Hujasikia wale wenye tuhuma za uhujumi nchi wanashinikizwa wakiri makosa yao na kurudisha pesa ili wasamehewe...




Cc: mahondaw
 
Ningependa tu kufahamu mtoa mada kama unajitegemea au bado unaishi kwa wazazi wako. Na kama unaishi kwa wazazi, basi una kila sababu ya kuja na huu uzi wako.

Ila kama unajitegemea, unafanya kazi au shughuli yoyote ile halali ya kukuingizia kipato; basi utakubaliana na mimi ya kwamba unalipa kodi, na hivyo ni jukumu la kawaida kabisa kwa serikali yoyote ile kujenga miundombinu ya kila aina kwa ajili ya wananchi waliowachagua kupitia kodi zao wanazotozwa kila dakika/saa/siku/wiki/mwezi/mwaka, nk.

Hivyo ni vyema ukaachana na hiyo mbinu yako mpya ya kusifia vitu vya kawaida kabisa. Hakuna awamu iliyokuwepo madarakani na haimujenga miundombinu.
Anaishi kwa wazazi au kwa shemeji?
 
Na vile ukichagua serikali ambayo haifanyi hayo? ndio utakuwa na ''strong'' mind?.. Acheni kujitoa ufahamu mbona nchi kibao hazifanyi hayo mambo na hata huko ng'ambo serikali zilizoendelea hujipiga kifua kwa mambo kama haya. Ukweli ni kuwa hawa jamaa wanatumia fedha zetu vizuri, makusanyo yale yale, vyanzo vile vile lakini mambo makubwa yanafanyika
 
Back
Top Bottom