Kero ya mawakala wa maegesho

Kero ya mawakala wa maegesho

neikia

Member
Joined
Feb 20, 2014
Posts
25
Reaction score
5
Leo nimepaki gari pembeni ya duka kununua bidhaa nimemaliza kununua kutoka tu nje nimekuta gari ya noah imejaa watu kibao wanadaai wao ni mawakala wa magesho ya magari eti nimepaki njiani natakiwa kulipa faini au waite break down waivute gari yangu,na hiyo barabara ni local road maeneo ya ukonga na faini yake eti ni sh 160,000.hivi kuna sheria km hiyo kiukweli wameniharibia siku.
 
Pole sana mkuu, ila faini ilitakiwa 50,000 tu. Mimi yalinikuta majuzi tuu nilikuwa natoka JKT Jitegemee pale getini naelekea mbagala, kuna mdada akaja kwenye gari langu anaburuza mguu anachechemea, akawa anaomba msaada. Akaniambia ameteguka mguu anahitaji msaada walau mpaka stendi ya daladala. Katika kumwuliza anakokwenda akasema anaenda kwa Azizi Ali, basi nikampa lifti kwa sababu tunaenda njia moja. Tulipofika kwa azizi ali, nikapaki gari kwenye parking ya daladala ili ashuke, ndani ya dakika moja, mdada wa watu anajaribu kushuka taratibu kwa sababu ya kuumwa mguu, jamaa wakapaki noah yao kuniblock. walinisumbua sana mpaka tukapelekana kwenye gereji yao kule keko, nikaishia kulipa 50,000.

Ila nimewanotice vizuri na mmoja wao nimegundua ananifahamu tunatoka sehemu moja, najua siku tukikutana kwenye anga zangu lazima nitalipiza.
 
Tatizo mkuu wakati mwingine ulikua na muda wa kwenda huko sasa mi nilikuo sooo busy wameningangania vibaya
 
Huu mradi,ila ipo siku watu watachoka,watatokea wenda wazim wawachomee lile gari moto ndio watatia akili.
We sehem hakuna alama,na parkings maalum hazipo.
Hili Jiji kila anaekaa linamshinda Meck yeye kazi kuukabia kupokea Viongozi tu lakini hamna kitu.
Watu wanajipangia wanavyotaka anaburuzwa tu.
Sasa we Angalia ukitaka kujua kama ni mradi wa wakuu,Faini gani haina kiwango kwa kosa moja.
Yaani mtu una bargain kwenye Faini?hii kali
 
Ukijumuisha na hao Tigo Fasta ndio kabisaaa,yaani wizi mtupu.
Mie walinikamata Pale Mbagala wakaniambai faini 60,000,ikafika hadi 15 wakaniachia.
Halafu hakuna risiti hapo na ukipewa basi feki
 
Leo nimepaki gari pembeni ya duka kununua bidhaa nimemaliza kununua kutoka tu nje nimekuta gari ya noah imejaa watu kibao wanadaai wao ni mawakala wa magesho ya magari eti nimepaki njiani natakiwa kulipa faini au waite break down waivute gari yangu,na hiyo barabara ni local road maeneo ya ukonga na faini yake eti ni sh 160,000.hivi kuna sheria km hiyo kiukweli wameniharibia siku.

loooo!
 

Attachments

  • 1409158177304.jpg
    1409158177304.jpg
    2.4 KB · Views: 163
Huu mradi,ila ipo siku watu watachoka,watatokea wenda wazim wawachomee lile gari moto ndio watatia akili.
We sehem hakuna alama,na parkings maalum hazipo.
Hili Jiji kila anaekaa linamshinda Meck yeye kazi kuukabia kupokea Viongozi tu lakini hamna kitu.
Watu wanajipangia wanavyotaka anaburuzwa tu.
Sasa we Angalia ukitaka kujua kama ni mradi wa wakuu,Faini gani haina kiwango kwa kosa moja.
Yaani mtu una bargain kwenye Faini?
 
Hii inakera sana siku watashikishwa adabu itakua funzo manake hata hizo faini sijui anapelekewa nani na ni mradi wa nani na ili iweje ni shidaaaaa
 
Yaani mkuu pole sana ndugu yangu. kiufupi mimi kila siku nasema hii mijitu ni mijizi sana na mijambazi sana. inakaba waz waz mchana kweupeee!!!! ila one day yes, wananchi tutachoka na kitakacho tokea...........!!!!
 
Back
Top Bottom