Kero malipo ya Mtihani NECTA kwa M-Pesa

Kero malipo ya Mtihani NECTA kwa M-Pesa

Ziltan

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2011
Posts
2,709
Reaction score
6,947
Nimefanya malipo NECTA kwa ajili ya mtihani wa PC CSEE mwaka huu lakini nikijaribu kufanya Online registration sytem inagoma na kusema receipt no and refference no does not match.

Watu wa NECTA na VODACOM (M PESA ) rekebisheni hilo tatizo kwan ni la tangu mwaka jana.

Mpaka sasa sijapata huduma na hela zishakatwa.
 
Ziltan Mfumo wa MPESA wakati mwingine unasumbua hata kwenye manunuzi ya LUKU. Usipoteze muda wako nenda ofisi za Voda/Mpesa ya karibu ukiwa na kumbukumbu zako nawe urudishiwe pesa zako ili uende ukalipie Posta kama watahiniwa wa kujitegemea wenzako wanavyofanya.

Sioni kosa la NECTA hapo maana kama kosa lingekuwa ni katika mfumo wa usajili wa NECTA wote wangeathirika. Mimi juzi kati nimelipia namba rejea ya mtoto wa shangazi yangu kupitia POSTA na ameshajisajili bila tatizo lolote.
 
grafani 11 hawa voda tangu mwaka jana wameonesha udhaifu mkubwa sana kwa hii huduma.
Waifute kwa hawawezi.
 
grafani 11 hawa voda tangu mwaka jana wameonesha udhaifu mkubwa sana kwa hii huduma.
Waifute kwa hawawezi.
Mkuu usipoteze muda mfumo ukafungwa bure, kinachosumbua hapo ni malipo nenda kachukue pesa zako ukalipie Posta ili uende na muda wa usajili. Kwani upo mkoa gani?
 
Ziltan

Utapoteza hela zako bure tumia ofisi za Shirika la kitanzania la Posta, unapata receipt ya kuthibitisha malipo yako na hapo hapo unafaidisha taifa lako na jamii yako. zaidi ni ule uhakika wa hela yako kuwa umelipa na hapo baadae uwe na uthibitisho.
 
Last edited by a moderator:
HIVI UKISHALIPA POSTA KUNA HAJA YA KWENDA KWENYE WEBSITE YA NECTA kufanya registration?
 
HIVI UKISHALIPA POSTA KUNA HAJA YA KWENDA KWENYE WEBSITE YA NECTA kufanya registration?

Ndiyo mkuu, hapo utakuwa umefanya malipo tu na kuifanya namba rejea yako iwe hai (Ref. Number Activated).
Unaweza kutumia cafe za Posta hapohapo ili ukikwama wakuelekeze au unaweza kutumia hata laptop yako kujisajili kupitia www.necta.go.tz
Necta haina longolongo mzazi, ingekuwa taasisi zote za Umma zinafanya kazi kama hao jamaa tungekua hii nchi ingekuwa mbali kiuchumi, kimichezo, utamaduni, elimu nk.
Halafu Katibu Mtendaji wa sasa Dk. Msonde ni mkweli na muwazi mno yupo karibu na wateja wake sio kama yule Ndalichako kila kitu kilikuwa siri hata visivyostahili kuwa siri kama kukokotoa alama za watoto wetu.
 
Back
Top Bottom